Manchester United (Red Devils) | Special Thread


Guys, kilichotokea MUFC sio Galactico signings, binafsi sijaona wachezaji walokuja MUFC ndani ya miaka sita tangu aondoke Ferguson ambao unaweza kusema kuwa ni wachezaji moto. wachezaji waliokuja ni wazuri ila sio wakupewa sifa ya ki galactico.

Mkuu, kwa mimi (Nazungumzia mfano ningekuwa manager) wote wa 50 na 12 million, si expect waje kuflop. Yaani mmoja akiflop, regardless of their price tag ujue basi kuna tatizo, ama hakustahiki kununuliwa kwa pesa izo na alikuwa over priced ama nimeshindwa kumdevelop, ama nimebuma mimi kumnunua mchezaji sie. Ata Fergie makosa haya yalimkuta.

Tatizo letu tumekuwa tunanunua wachezaji for the sake of signings.

Sipingi kuleta vijana kuja MUFC, lakini tunampa mkataba Young na kumuacha herrera, miaka nenda miaka rudi tumeona Jones na smalling hawatufai ila bado wamebaki Club!.

Halafu inawezekana hamukunielewa, mnafikiria kama mimi nataka tununue ma stars tu, mimi nataka wachezaji wenye experience na wanaojua kazi zao. Mtizameni Pep alivojenga timu, mpe milioni miliono 100 atakuletea wachezaji wawili ambao in a very short time wanakuwa tishio.
 
Mkuu sidhani Kama mazoezi anapanga kocha mkuu, timu Kama man U kunakuwa na jopo la zaidi ya watu 10 ambao Kila mmoja ana specialize kwenye kitu chake.

Na kitu kimoja ambacho mashabiki naamini tunaafiki ni kwamba timu yetu haipo fiti, wanahitaji kuwa fit zaidi kuliko kitu chengine chochote, mtu kama phelan naamini ana uzoefu na knowledge ya kutosha ku oversee Jambo Kama Hilo.

Tumuachie kocha afanye kazi yake maana yeye ndio mtaalamu, hao waandishi wa habari wanapenda tu kuandika vitu negative ili wapate attention,
 
Unapokuwa unatuambia "Your Manager" unakuwa kama unatutukana..as if sisi ndo tuliomuappoint..

Stop that man
Nyie ndio mlie msapoti since day one, you were so busy singing Ole's at the wheel when he was beating relegation folders.
 
Youri tielemans amereja jumla Leicester kwa pauni mil 40..... jamaa alikuwa decent sana, deal zetu sijui huwa zinakwama wapi...... Inafika kipindi naomba hata hao waingereza waje tu huenda tukalamba dume la kupata Carrick mpya na Lampard mpya......
 
Sioni shida kwenye hilo

Msimu uliopita wakati wa Jose, United ilikuwa top 5 ya timu zilizokimbia kidogo uwanjani/wavivu. Kiufupi physically hawakuwa fit

Unadhani ni wakati gani kocha atautumia kuwaweka wachezaji wake timamu kimwili? Ligi itakapoanza?

Kuna zaidi ya mwezi wa timu kujiandaa, lazima kuna wakati timu itafanya mazoezi ya kucheza mpira, kufanyia kazi formation n.k.

Kukosoa kila kitu hakutasaidia timu. Timu ameshapewa OGS, tumpe benefit of the doubt. Aliomba sana pre season, sasa wakati wake ni sasa. Mwisho wa msimu tuone kama ametusogeza mbele, tupo pale pale au ameturudisha nyuma

Yote haya yanategemeana pia na wachezaji atakaopatiwa na Ed
 
VVD hana pace????sio hana pace sema ni mara chache inatokea yeye kuhitaji kukimbia kutokana na defense yake nzuri.Na pia si kawaida kuona beki wa kati anakimbia kimbia maana wao ni watu wa mwisho zaidi kubaki nyuma timu inapopanda sasa wakimbizane kwenda wapi.
Unachotakiwa kujua tu ni kwamba VVD msimu wa UEFA ulioisha yeye ndio aliongoza kwa sprint yenye kasi zaidi.
 
Walisajiliwa wakina Di Maria , falcao waliifanyia nini timu licha ya majina yao Makubwa??
 
Katika kipindi cha hiyo miaka nane taja idadi ya mabeki waliosajiriwa ...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…