severinembena
JF-Expert Member
- Jun 2, 2018
- 2,435
- 2,397
Daaa hao wahuni wana zali sanaMapacha wa Tatu wa Mr.Nice Guy.
Jose Moja ya kocha ambaye sjawahi kuwa muumini wa Soka lake(Soka la Uoga),Japo naheshimu Mafanikio yake dimbani.
Juzi alivyokuwa akihojiwa aliongea jambo la Msingi sana Ukiwa Ukiwa Mr nice guy sahau kapata mafaniko makubwa dimbani,kama ukiweza kuweka walau uwiano sawa Mr nice guy vs Ruthless(devil May care )itafaaa zaiidi.
A Ruthless SAF hakuwa na utani kidogo,siku Moja aliwahi kuulizwa na shabiki wa Man U,
Mbona sjawahi ona tabasamu lako Uwanjani..?
SAF akajibu sipo hapa kutoa tabasamu,Tabasamu utapewa na mkewe...nipo hapa kutoa burudani na kupata Ushindi.
Wakina Mr nice guy Giggs watapa wakati mgumu kupata mafanikio makubwa dimbani.
Mr nice guy Mwinyi,Bwana Mashirika a.k.a Nyerere alimwambia wewe bwana ni Mwema sana,Mtu safi lakini kama kiongozi wewe ni dhaifu.
(Uongozi na Hatima yetu by Nyerere ).
Sosha anauthubutu kuwaondoa wachezaji Mizigo,wavivu,Uwezo mdogo Uwanjani kama alivyowahi kutamba na kauli zake...?
Au ni bwana asiyeweza kusimamia maneno yake...?
Nani top six Epl aweza kutoa mkataba miaka Mitatu kwa Jones Plus £120K....? mechi tano yupo gereji... (Labda bodi ya Man u wanamijihela tele)
Sosha aweza kufanya mabadiliko makubwa na kutuvusha mbali au twajivika Upofu wa Imani..
Nyota njema itaonekana Majira ya joto,Pamoja na madhaifu ya Uendeshwaji wa club(Glazzer & Ed)kocha lazima uwajibike kwa kazi yako..Japo Jose Ni kocha asiyependa kuwajibika anahamisha lawama kama aina ya viongozi wengi wa Africa.
Karata kubwa ya sosha iliyobakia ni Ulenged wa Man United Fc (Uvumilivu wa Mashabiki).
Inasemekana Jose alitaka kuwaondoa mizigo na wavivu wote ndani ya timu msimu wa pili,ghafla akiitwa na bwana Mapesa (Bank teller)Ed Woodward,
Ed akasema wewe bwana shida yako nini..? si ni pesa..? chukua fedha hii hapa,Hao uwaitao mizigo ni asset,Mishahara tunagharamia sisi.
Mchezaji anaweza kukaaa man u miaka mitatu hachezi lakini kalidhika anakula posho,anajimwayamwaya katika Jacuzzi wala hana hata presha...mfano Darmian.
Sosha anamlima Mrefu sana,kama atatangulizi Ujasiri ,Umafia akiongozwa na falsafa yake ya soka (Hata sjui huyu bwana kama kweli anafalsafa ya soka) ndio vitamvusha,la sivyo kichwa chake kabla ya mwana wa adamu kuzaliwa huko Bethlehem kitatolewa sadaka ya Kuteketezwa.View attachment 1099767View attachment 1099769View attachment 1099771
Wewe jamaa nadhani hunijui vizuri kwenye huu Uzi wa timu yangu pendwa kutoka mitaa ya Great Manchester pale Jijini Manchester.Nilichogundua we ni haters wa Mourinho, hapa ninajadili na mtu mweny chuki na mtu fulani, Et Mou ni kocha mwenye uwezo mdogo, kocha yupo kwenye top five ya makocha bora af unamwita vitu vya kipuuzi......we vip, kwanza ukitaja jina la Jose lazima utaje jina la Guardiola mana ndo the only one anayemyumbisha jamaa, uwanjan na kwenye mataj, tuchukulie Guardiola asingekuwepo Man city, EPL last season angechukua nani? Pochetno???..
Wakat Jose anafukuzwa kazi wote tulimunyoshea kdole kwamba tatizo ni yeye, ila sa hv nan anamnuoshea kidole jamaa, wengi sa hv wameturn back kuinyoshea kidole board na players, ni kweli watu wengi tuna dislike mbinu zake uwanjani, lakn tatzo la man u ni zaid ya Jose na hili yeye alilisema waz,....Ko kumbe tatzo la Man u sio mbinu za kocha tuu ni accumulation of problems...
Pote inajulikana kuwa ukimwajir Mou timu yako itakuwa ya kupak basi, sasa kwa nin usimpe support ya kutosha atimize malengo yake badala yake unaanza kumnanga ili afeli umfukuze kazi, Na ulimwajir ukijua hilo, huo si ni unafiki.....
Msimu wa kwanza Guardiola alisajili wachezaji wanane, na hakupata chochte zaid ya kuingia top 4, Rumours za kufukuzwa kazi zilikuwa nje nje lakn board ilimpa full support, msimu wa kwanza pesa iliyotumika ni Pound 186Mill,....Tafta ya Mou alitumia sh ngap...Mou akachukua Europa nafkli na FA
Msimu wa pili Guardiola alspend Pound 276Mill,....akachukua ndoo ya EPL, Tafta uone Mou alispend sh ngap....akaishia nafas ya pili, .....
Jose alijua kabisa mapungufu yaliyopo hvyo kuingia msimu wa tatu alihtaj kukiongezea nguvu kikosi ili kukabili kasi ya Man city na Liver....kilichofanyika tunakijua, akaonekana anafuja hela, ooh mbinu yake ya kupaki basi, kwanza kaishia nafs ya pili msimu uliopita na mengne mengi...
Guardiola akamwaga tena Pesa Pound mill 63, Sjui hata United ilitumia sh ngap....alaf mtu anademand matokeo mazur uwanjani how comes? unaweza kufight na best managers kama Klopp na Guardiola wenye kila aina ya silaha wanayotaka, huku ww silaha unazozitak hupati, unaletewa Pogba na Sanchez, et lengo wanakuforce ubadili mbinu ucheze mpira wa kuintertain mana wachezaji hao sio wa kupaki basi, et una rashford na Lingard huo si utani kabisaa...anyway mambo ni meng na mda ni mchache...
Kwa misimu miwili tu Guardiola alitumia zaid ya pound mill 525,....
Mou amespend pound 390 Mill in total....
Wewe ni mcheza FOREX mzuri sana, na njia hyo ya kujipatia kipato imekufikisha hapo ulipo japo wengine wanakudharau kwa kusema FOREX ni utapeli. ko usimdharau Mou kwa style yake ya kupaki basi, ndo ilipomfikisha hapo alipo, na akienda timu yyte lazima aondoke na vikombe, sa unaanzaje kumwita kocha kama huyo uwezo mdogo.... Jamaa ana mapungufu yake ndio, ila sio kumshusha hadhi kias hcho aisee....
Ha ha haaa...mkuu nitafasirie neno "wahedi wewe" limeniacha junction isjekuwa tusi ndug....Wewe jamaa nadhani hunijui vizuri kwenye huu Uzi wa timu yangu pendwa kutoka mitaa ya Great Manchester pale Jijini Manchester.
Ambacho kimenishangaza zaidi ni tabia zako za "Kimwajuma mwajuma" kuleta mambo ya Forex kwenye kabumbu la wanaume wa shoka. Sasa basi kwasababu umekuja "Kijuma lokole" Mimi huwa siungi mkono huo ujio wa namna hiyo.
Na kwasababu umeamua kuhamisha mjadala kutoka kuwa mjadala wa kikabumbu na kuufanya mjadala kuwa wa mashambulizi binafsi dhidi yangu, nakuomba kabla sijaandaa makombora ya Ballistic missile kuja kukusasambua ufanye yafuatayo;
1. Naomba unitake radhi kwa kunihusisha Mimi na forex katika Uzi wangu huu pendwa
2. Nakuomba ufute kauli yako kwamba mimi nimewahi kusema Forex ni utapeli
3. Nakuomba ufute kauli yako kuwa Mimi Nina chuki binafsi na Mourinho ..
Nimejijengea heshima kubwa katika forum hii , sitakubali "Mpuuzi " yoyote Mwenye akili za "Kimilembe milembe" , kwasababu tu ya kumiliki smartphone na bundle la chuo anichafue. Sitakubali.
Sasa mimi ninaweka notification on ili nisubiri utakachoandika ili nikubalase kisawasawa mpaka utakapokuwa unaona hii ID uwe unasema "Shikamoo" .
Wahedi wewe.
Brother umepotea kitambo sana! Nilizani umebadili ID
Tulikuwa na 'Ole's at the wheel' ha ha ha
Kama ni mambo ya kuanza upya bila kutegemea wachezaji wakubwa,tungembakisha van gaal,huyu ole sioni mahali akitupeleka kwa kikosi kisichokuwa na uzoefu.
Zaha anafaa kurudi
Wachezaji wa kiingereza sijui kwanini wanakuwa na bei zisizo halisi na ubora wao. Tutafute league 1 na dutch league 1 kuna talent kibao na kwa bei chee.Crystal palace wanataka paun mil 100 mkuu na Binafsi sidhan kama Zaha anastahili pauni mil 100 hata 70 yenyewe zaha haitendei haki.....
Zaha , lingard , martial wote hali Moja tuZaha anafaa kurudi
Hawana nia ya kumuuza.Wilfried Zaha anataka kuondoka crystal palace. Cha ajabu ni kua Crystal palance wanataka £100m kwa klabu inayomtaka zaha.
Waingereza watamfukuzisha kazi Ole.Ole kwangu mm sio kocha bora na nadhani timu yetu itamshinda kama haiijamshinda bado.
Ole hana plan uwanjani hajui timu inacheza vipi watu wanacheza tu uwanjani ovyoovyo kama vile hawajawai kucheza pamoja. Hana tactic yoyote uwanjani jamaa anaonekana kabisa hana experience yoyote. Klop anatumia high press..na fast buildup kwenye kushambulia..pep anatumia constant pressure kwenye kukaba na high possiesion kwenye attack..nk nk nk. Ukija kwa kocha wetu ole haijulikani anacheza mfumo upi yupoyupo tu anategemea miujiza na vibe la wachezaji kushinda.
Pili jamaa yuko poor sana kuselect wachezaji wa kuanza mechi na nadhani ana ubaguzi flani kweye kuselect first eleven kuna kipind unaona kabisa lingard anazingua lakini kila siku utamuona ndani anacheza kila saa anamweka nje mtu kama lukaku amabae anainekana kabisa anapambana anapanga watu wasiojituma kina rashford(yaan huyu dogo kocha hawez kumkanya kabisa..dogo anajiona ronaldo sijui ni mchoyo balaa anataka kupiga kila saa anakaa na mpira mpaka anapoteza analalamika mno uwanajani kuna mda mpaka anazira mpira aisipopewa faulu. Kocha mzuri angeshamnyoosha dogo toka kitambo) kila siku tunaona tabia ni ileile haibadiliki ata
Tatu jamaa anazingua kwenye kuongeza mikataba ya wachezaji. Yaaani ni uingereza tu umemjaa waingereza wabovu wanapewa mikataba mizuri na kuongezewa mpunga na bado wapambanaji wakina herera wanaachwa kusepa kisa kuongezewa pesa tu kidogo.
Yaan anaonesha ubaguz wa wazi kabisa unamuongezea mshahara martial asiejituma herera akiomba kumuongezea pesa unagoma??? Daah
Nne jamaa kwenye sub ni mbovu sana yaan unaona timu inazingua toka mda tu yeye katulia tu anasubir sijui mpak dakika ya 70 au mpaka mpigwe goli ndo anajifanya kushtuka na kufanya sub zake mbovu fasta. Unakuta lukaku ndo kacheza vizuri anamtoa anamwacha rashford aliekuwa anacheza fyongo. Rashford kacheza fyongo sana na jamaa alikuwa hamtoi hata iweje naona juzi ndo kaanza kumpiga sub dogo
Mwisho jamaa anaonekana kabisa sio mkali kwa wachwzaji na kuna wwachezaji anawaogopa mfano pogba..jamaa anawez zingua mechi anapoteza pasi hakab nk ila atampiga sub fred anaecheza vizuri. Huu upendeleo wa wazi ndio unaopunguza morali ya timu.Tatizo la kuchukua nakocha wadogo ndio hili kocha hawez kumwambia chochote star wa timu unadhani ole anaweza kumkaripia pogba au martial wakabe?? Ndio maana timu letu linacheza kivivu tu
Hao kina mourinho pep na fergie ni wakali ndio maaana wanamafanikio na timu zao huyu kocha wetu mselamsela sidhan kama ataweza irudisha timu kuwa bingwa tena.
Posibility ya kurudi ni kubwa Sancho anagoma kuja United sabubu haiko Champions leagueZaha anafaa kurudi
Tunamhitaji Umtiti, Dyabala, Ayoze Perez na Eriksen.Posibility ya kurudi ni kubwa Sancho anagoma kuja United sabubu haiko Champions league
OGS alimfundisha Zaha Cardiff City alivyocheza kwa mkopo na alikuwa anamsifia sana
Tunamhitaji Umtiti, Dyabala, Ayoze Perez na Eriksen.
Zaha ni mua Ivory CoastWachezaji wa kiingereza sijui kwanini wanakuwa na bei zisizo halisi na ubora wao. Tutafute league 1 na dutch league 1 kuna talent kibao na kwa bei chee.
Man united material hapo ni mmoja tu Eriksen.Tunamhitaji Umtiti, Dyabala, Ayoze Perez na Eriksen.