Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Damn..tuna kazi kubwa sana ya kuifanya kurudi hata kidogo tu kwenye ubora
 
Kilichomfanya jose apoteze pambano (kama unavyodai) ni ule ukweli wake, jose sio mtu wa kupindisha na kumung'unya maneno, kama ni nyeusi anasema hii ni nyeusi kama ni nyeupe anasema hii ni nyeupe.

Pogba anajiona mkubwa kuliko Manchester that's why anafanya anachojisikia na jose alipojaribu kuwafungua macho madhaifu ya pogba media na mashabiki kindaki ndaki wakamjia juu, saizi taratibu wanaanza kuelewa.

Alichokua anakiongea jose kuhusu board ya timu hadi wengine wakawa wanadai anamtumia Woodward kama scapegoat hapo juzi tu LvG kakiongea, leo hii wale mashabiki uchwara wameanza kuelewa.

Alishawahi kusema kumaliza nafasi ya pili kwa hiki kikosi chetu ilikua ni moja ya mafanikio yake makubwa sana kwenye kazi yake ya ukocha, but kuna watu wakawa wanam-mock na kusema ana lower expectations, nadhani soon hata hili mtajua alikua anamaanisha nini.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakuonea huruma huwezi ku-handle matusi na kejeli za so called top reds, wao uki criticize mchezaji/ kocha wao kipenzi wanakuona sio shabiki wa kweli.

Nakushauri we endelea kuvaa miwani ya mbao na ku assume timu yetu haina mapungufu/madhaifu yyte hapo ndio utaenda nao sawa.
hahahahaaaaa mkuu nilituma maombi ya kuwa mwanachama wa kundi la kumpinga OGS cha ajabu mpaka leo hujanijibu, au unahofia nitakuwa napuliza pande zote mbili kama kawaida yangu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tazama leo tunavyomgaragaza Briton city uko.. Hiz ni dalili za mapema kabisa za Ole kuishia no.6

Sent using Jamii Forums mobile app
rasmi tumerudi nafasi ya sita.
sijui tottenham ataendelea kupoteza tena mechi?
sijui arsenal ugonjwa wao wa kudondosha points ovyo utarudi upya?
sijui chelsea watarudisha tena sintofahamu yao juu ya sari masigara?

bado sijakata tamaa na top 4 msimu huu.
 
Ninachojua kwenye swala la usajili watu wengi tulikua nyuma ya Mou, ndio maana mashabiki walikodi ndege ,wakarusha ile banner ya ED OUT kama sikosei. Hata uwanjani siku tukifugwa watu walikuwa wanamshangilia Mou.

Haya tunarudi sasa, kwanini tulitaka Mou haondoke? Sababu Mou hakufaa kuwa kocha wa Man U. Toka siku ya kwanza mashabiki wengi hatukupenda Mou awe manager wa Man u.

Sent using simu mbovu
 
May be my memory is down, nani anakumbuka the time your favorite coach anachukua timu tulikua nafasi ya ngapi? And what an improvement he has made so far?
View attachment 1062242

Sent using Jamii Forums mobile app
Ok hajafanya improvement yoyote, but alipokuwa anachukua timu tulikuwa points 11 kutoka nafasi ya nne ,kwa sasa tuko points 3(5) kutoka position hiyo.

Sent using simu mbovu
 
So according to you, moving from 6th to 6th is an improvement?

From what i know we moved from winning trophies almost every year to losing thrice against wolves in a single season. I hope also this we can call it an achievement.
Ok hajafanya improvement yoyote, but alipokuwa anachukua timu tulikuwa points 11 kutoka nafasi ya nne ,kwa sasa tuko points 3(5) kutoka position hiyo.

Sent using simu mbovu

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Hakuna kitu nisichounga Mkono kwenye soka kama kuombea timu nyingine zifanye vibaya hili nafasi yako iwe vizuri, nakumbuka tulijadili baada ya kupangwa mechi za robo Final ya UEFA kwamba ni bora tujikite kugombea nafasi ya nne na si UEFA
Tuombe bahati iwe kwa timu ifanikiwe kumaliza nne bora
 
Ok hajafanya improvement yoyote, but alipokuwa anachukua timu tulikuwa points 11 kutoka nafasi ya nne ,kwa sasa tuko points 3(5) kutoka position hiyo.

Sent using simu mbovu
tatizo si kocha tulienae bali ni wachezaji wanaounda timu yetu wengi wao wanatabirika kiuchezaji, kama hoja ni udhaifu wa makocha ndani ya miaka 6 tumewapa mikataba makocha wawili wenye cv nzito kuliko great wall lakini bado lengo kuu la kuundwa kwa timu hatujalifikia.
mbona mechi tano za mwanzoni za ujio wake tulikuwa tunacheza vizuri sasa ile morali imekwenda wapi?





josep guardiola aliyerithi timu yenye mafundi kama david silva, de bruyne, toure yaya, otamendi, aguero, sterling, fernandinho ndani ya misimu miwili anafanya mabadiliko kama yanavyojionyesha hapo juu.


kwa ushahidi wa hapo juu kama guardiola angeliwakuta wachezaji aina ya smalling, jones, majeruhi rojo, valencia, lingard, darmian, young angeliwaondosha baada ya msimu mmoja lakini cha ajabu kwetu sisi tunawapa mikataba unaoanzia malipo ya paundi laki moja.
 
JOSE ALVAREZ, one of the most reliable Spanish source who has a very good reputation with transfers regarding the 2 Manchester clubs, is today reporting that, ANDER HERRERA has agreed a 5 year deal with Paris Saint Germain and will leave Manchester United at the end of the season.

kama klabu imeamua kubadili mfumo wake wa uendeshaji kuanzia ushughulikiaji wa mikataba ya wachezaji muhimu, mipango bora ya usajili wa wachezaji wenye ubora kwa kuangalia umri wa mchezaji husika basi watakuwa wapo sahihi kutokubaliana na madai ya ander herrera ya kutaka mshahara wa paundi 200000 kama taarifa zinavyoeleza.

lakini kama ujinga huu anafanyiwa ander herrera peke yake halafu inatokezea mchezaji kama rashford anapewa mkataba wenye thamani ya paundi laki mbili kwa wiki pindi atakaposaini mkataba mpya tutakuwa tumefanya dhambi kubwa sana ya kimaamuzi.

kwa umri wa herrera ni muda muafaka kiupande wake kutafuta sehemu itakayompa maslahi makubwa pasina kuangalia ubora wa klabu na historia yake.
ghafla nimejikuta naikumbuka hadithi ya claudio makele dhidi ya real madrid

Good luck in the future Ander Herrera​
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…