Bonny
JF-Expert Member
- Feb 21, 2013
- 13,370
- 29,990
Unachokizungumza ni sahii mkuu ila napingana na wewe kwenye swala la kusema OGS ni muoga Imagine alikua na week 3 tu toka ateuliwe akaingia kwenye transfer windowMkuu hapa mimi ni mmoja wapo, tena wala si kitu cha kuchekesha..!!
Tena hapa nikiri ni mmoja wa tuliomtaka kwa udi na uvumba Mr Mourinho, ila si kama kocha wa kudumu bali wa muda mfupi kwaajili ya kurejesha heshima ya timu baada ya kuflop kwa miaka minne mfululizo kipindi cha Mr Macho na LVG. Sote tunajua Mou ni mtu anayetengezeza timu ya mafanikio kwa muda mfupi na kamwe si kwa muda mrefu.. ni bahati mbaya kwamba Bodi ilimuongezea mkataba baada ya mafanikio kwenye Europa.
Nikija kwa Poch,
Poch ni mjenzi wa timu haswa... ni mkufunzi wa mpira wa kushambulia falsafa ambayo Man u ndio mpira wetu. Ni Meneja ambae mafanikio yake yameonekana wazi tangu akiwa huko Southampton mpk hii leo hapo Tot.. tumeona kwa miaka minne namna ambavyo Tot wamekuwa washindani wa kweli kwenye league na hata Ucl tena kwa bajeti ndogo na ya kawaida tu, ni bahati mbaya wamekosa vikombe kipindi chote hicho nadhani ni uzoefu tu ndio unawasumbua na hili tunaliona hata kwa kocks kwenye league.
Kwa OGS (naheshimu sana kazi yake)
Lakini simuoni kama ni kocha wa kudumu wa Man u, Ogs amechukua timu kipindi ambacho kila mchezaji alishamchoka kama si kugombana na Mou, Morali ya timu ilikuwa chini kupita maelezo... ilifikia kipindi hata Man u ikicheza na Crystal palace mtu unaangalia mpira kwa kutetema kwa hofu ya kufungwa muda wowote.. Hili Ogs amelitumia kama fulsa ya kuinyanyua timu.. So ni kama Ogs amewaruhusu tu wachezaji kufanya wanachokita uwanjani.. lakini kwahakika mpaka leo bado hajapandikiza zile mbinu za kocha ambazo kila mtu ataona hapa bila kocha flan pengine tusingeshinda.. ama tungefungwa.
Ukitaka kuliona hili kwa uwazi hebu angalia pale man inapocheza na timu za top 5 kwenye league na mechi mbili za psg. Utaona wazi kwamba licha ya kwamba timu inashinda lakini inapata shida sana kuupata ushindi huo kitu ambacho hakikuzoeleka kipindi cha babu feggie.. unajua kama tunataka timu ifanye vizuri tusimpimie Ogs na hawa kina Macho,Lvg na Mchonga.. kipimo sahihi kwa Ogs kiwe kwa Feggie. Ogs mpaka sasa bado hajafanya usajiri wowote licha ya hapo January kuwepo kwa dirisha la usajili na namna timu ilivyokuwa sote tunafahamu. So kwa namna nyingine namuona ni muoga anaogopa lawama.
Nikisema haya si kwamba simuheshimu OGS wala kwamba nampinga ila nabaki palepale kwenye point yangu kwamba ninaona si kocha sahihi kulinganisha na Poch haya ni maoni yangu mkuu nadhani hata wewe unamtazamo wako... tusilewe sana na huu upepo wa muda mfupi... tukumbuke kunakipindi matokeo ya upepo hupita zinabaki hali ngumu.... sioni shabiki wa kusimama na Ogs pindi tutapopata labda sare tatu mfululizo na vichapo kadhaa... (nyakati hizi zipo) ni kweli tutaendelea kumuunga mkono? Au tunaangalia hapa..... bila kuona kuleeee....
UNITED WE STAND
Sent using Jamii Forums mobile app
Unahis kama ni kocha sahihi ni bora ukanunue mchezaji wakat team yako bado hujaisoma vizur au mapungufu yao ni yap na wap kwa kuongeza
Before OGS kila mtu alikua anasema Linderlof sio beki mzur ila baada ya kuja Linde ameonyesha kwamba anaweza kufanya kazi vzur tu akiamniwa
For my end naona maamuz ya kutosajili yalikua sahihi kwanza atengeneze team yale plus kurudsha confidence ya wachezaj iliypotea
Just imagine game na PSG kwa crisis ile ya.majeruh ingekua enzi za Jose tungesemaje sidhan kama kuna mtu angejisumbua kwenda hata kuangalia.
So OGS ametengeza team yake Inshallah akipewa contract July atakua ameshajua mapungufu ni yap na wap kwa kusajili