dah! hii heshima ulionipa ni nzito kuliko ndevu za lionel messi.
ujio wa
pochettino na faida zake kwa mtazamo wangu.
- ana uzoefu na ni muumini wa mpira wa kisasa ambao tumekuwa tukiulilia kwa muda mrefu
- ni muumini wa kuwapa nafasi wachezaji vijana na hili tumelishuhudia kwa wachezaji tofauti.
- ana rekodi nzuri sana kwenye suala la kusajili wachezaji, ukiangalia wachezaji wengi aliowasajili tokea yupo southampton hadi tottenham hotspurs wameendelea kufanya vizuri na wengi wao ni wale aliyowasajili kwa fedha chache.
athari yake kubwa ninayoiona ni kurudi tena kwenye zama za kuachana na falsafa, misingi na utamaduni wa klabu iliojengwa miaka mingi iliopita, naamini kama
pochettino atawasili msimu ujao hatopendelea kuchaguliwa benchi lake la ufundi hivyo basi atakuja na timu yake ya ufundi, inamaana tutaanza tena upya kama alivyofanya
david moyes, LVG na
jose mourinho.
halafu pia siamini kama
pochettino atadumu kwa muda mrefu klabuni bila ya kuwa na fikra za kurudi tena spain kufundisha
kwa uoni wangu sioni dalili yoyote ya kuondolewa
ole gunnar solskjaer mwishoni mwa msimu hata kama atashindwa kupata nafasi ya nne, kuna nguvu tatu zina mlinda kwa sasa ambazo ni legends aliocheza nao kwa mafanikio makubwa, waliyopendekeza apewe nafasi baada ya kuona jahazi linazama na nguvu ya mwisho ni ya mashabiki wale wa karne ya 20 ambao bado wanaendelea kumuona ni shujaa aliyetakasika kwa kile alichokifanya pale nou camp.
silaha yake nyengine kubwa aliyokuja nayo ni kurudisha utamaduni wa manchester united wa kucheza mpira wenye kueleweka, makocha waliopita kila mmoja alikuja na falsafa yake isiyoendana na damu ya manchester united, wakati wa
jose mourinho tulishinda mechi nyingi sana chini yake kuliko mwalimu yoyote yule lakini nidhamu yetu ya ushindi ilikuwa ni ya kiwango cha chini sana.
hata ukiangalia benchi lake la ufundi ni uthibitisho tosha jinsi gani klabu imeshajiandaa kuishi na OGS kwa sababu limejaza watu wanaoendana na utamaduni wa manchester united, siamini kama ujio wa
mike phelan ni kwa muda wa miezi sita tu halafu atafute mlango wa kutokea.
kama ishu ni kuwapa nafasi majina makubwa basi klabu tayari imeshapitia hatua hiyo lakini bado tuko pale pale, ukiangalia upande wa pili imemchukua miaka mitatu jurgen klopp kuifikisha liverpool hatua iliopo muda huu cha umuhimu ni kuwepo uaminifu.
Solskjaer, Phelan, Karrick na McKenna ni timu ambayo inahitaji kutafutiwa mwanadamu mwenye uelewa mkubwa wa soka la kisasa na hii ndio kazi ya kwanza anayopaswa aifanye ed woodward.
nasubiria majibu yake siku ya jumapili baada ya kupoteza alama mbili kwa mara ya kwanza tokea awe mwalimu wetu,
leicester city ni kipimo chengine cha ukweli.
kuna mlevi mwenzangu ameniuliza hapa hivi
ole gunnar solskjaer aliikuta manchester united ikiwa nafasi ya nne?