Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Nimekuelewa sana halafu unaandika bila jazba wala lugha za kuudhi heshima kwako mkuu kutumia lugha ya kuudhi si kwamba ujumbe wako unafika ni kujichoresha tu

 
Timu inacheza vizur tu
 
Hebu nipe mambo makuu matano ambayo ameyafanya Hazard na team ya Chelsea iko vibaya.


Halafu naomba uniwekee orodha ya mashabiki wa Chelsea wanaohitaji hazard auzwe. Labda watakuwa mashabiki wa ileje huko ila shabiki anaetumia medula yake vizuri hawezi thubutu kuinua mdomo wake na kusema kiumbe huyo kutoka Belgium auzwe. Labda akili za Mpuuzi Mou ndio zinaweza kufanya maamuzi hayo ya kipuuzi.


Hebu cheki hizo takwimu za hazard halafu usikie kuna mpuuzi anataka kumuuza kwa sababu zisizo na kichwa wala miguu.


Niliwahi sema humu kuwa Njia pekee ya kiburi cha kocha yoyote kufanya maamuzi kama ya kumuweka mtu kama Pogba benchi ni KUSHINDA TU. Maamuzi yako yataoneka ya maana kama ukiwa unashinda Baaaaaasi, ila ukiwa na maamuzi ya hovyo na matokeo hupati lazima utimuliwe.


Hivi unamkumbuka Haya Toure unadhani Man city wangekuwa wanafungwa kama Manchester , wale Die hard fans wa City wangekuwa wanamuonaje Gurdiola kwa maamuzi yake Magumu ya Kumuuza Nguli hili la soka kutoka Ivory Coast. Lazima angepigwa chini ila matokeo ya uwanjani yamembeba Guardiola. Same situation anayopitia Sergio Aguero. Hivi ni vitu anavyokosa mou; ana mabifu na wachezaji halafu hana lolote kimbinu na team inaishia kuwa na Goal difference 0 yaani sifuri. Halafu MTU mzima Kama wewe huoni ni Jambo la Kishetani team yenye hadhi kama united mpaka msimu wa xmass kuwa na 0 goal difference.




Halafu acheni kukaririshwa, Amini nakwambia Ferguson kama angekuwa mpaka Leo asingekuwa na jeuri ile ya kuuza watu hovyo. Zamani ulikuwa ukiangalia duniani unakutana na lundo la washambuliaji. Leo pitia pitia ligi zote uone natural namba 9 ni wangapi??... Hapo Manchester tu asilimia 50 ya mabeki sio natural defenders unadhani kipi kimefanya hivyo na usajiri ulikuwa unafanywa kama kawaida.


Ashely Young ni namba tatu ila kiasili ni winger. Valencia kiasili ni namba 7 ila Leo ni namba 2. Unajua sababu ni nini????



 
Weka na statistics za pogba tangu alipofika Man U hadi sasa ili uwe na legality ya kuongea hayo.
 
Weka na statistics za pogba tangu alipofika Man U hadi sasa ili uwe na legality ya kuongea hayo.
Naona umechange Gia angani kwa speed ya DCM za Kwenda Mbagala. Nimekuwekea takwimu maridhawa za Hazard na unijibu baadhi ya maswali matokeo yake unakuja upewe statistics za Paul Labine Pogba.








Unatembea kifua mbele kuwa Manchester united tuna ndoo ya Europa, sio ???? .. Goli la kwanza alifunga Paul Pogba na kukufanya ukenue huku umma ukishuhudia meno yako yote 67. Hiyo ndio "Hidden statistic" ya Double P.

Zingine naamini unazielewa ila umeamua kunipima
 
Line up ya ole haijatoka?
Tujue kama tutashambulia au tunapaki basi
 
mkuu umezidisha ni 32 hizo sio pip
 
Wala sikubadilikia angani ulileta takwimu za hazard ambae kwa kiasi kikubwa ni tegemeo la Chelsea na yeye ndiye anayeifanya Chelsea iwe na sura tofauti. Ila si kwamba yeye ni tegemeo kwa kuwa na sura nzuri au kuwa na chenga nyingi, hapana bali pamoja na makandokando yake kwa kiasi kikubwa anajituma na timu kweli amejitwisha yeye. Sasa huyu Double P kwa sasa huwezi simama mbele ya mtu ukasema huyu Double P ni mchezaji Wa kipekee kiasi kwamba ni tegemeo la timu. Badala yake utapaswa kusema huyu Double P ni mchezaji mwenye kipaji kikubwa ila anai cost sana timu. Au wewe unamuongelea Pogba gani ambaye anaibeba timu kiasi kwamba kuwekwa benchi kwake na Liverpool kukasababisha timu ifungwe 3-1? Na kuhusu EUROPA unadhani ni kwa nini pamoja na kufunga hilo goli unalosema bado hakuwa man of the match? Basi tumsifu aliyekuwa MAN OF THE MATCH "ANDER HERRERA" Unajua kwa nn alipewa hiyo? Ni kwa sababu alijituma sanaaaa!!!Mchezaji anapaswa ajitume siyo akatae kujituma eti kwa madai kocha hamsikilizi jinsi anavyotaka apangwe.
 
Hizo laini nilizopigia msitari ziko very contradicting, hebu soma uone kama unapata logic.





Anyway it's a time for our Game.... Hahahaha Kama nakuona ulivyofura kwa kumuona Double P akiingia moja kwa moja kwenye first eleven baada ya kuchomeshwa mahindi na Ibilisi yule wa kireno.


NB: Ni Mgonjwa wa Milembe tu ndio anaweza kumuweka benchi Double P.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…