Baada ya kutanguliwa kufungwa goli mbili na City Mourihno hakuwa na jinsi zaidi ya kuiruhusu timu kucheza/kushambulia zaidi kuliko kuizuia City kama ilivyokuwa kipindi cha kwanza, kwa kubadili mfumo na kumsogeza mbele Pogba nyuma ya Lukaku creativity ya timu iliongezeka, na tuliona Pogba alichokifanya, Sachenz.
Mourihno akiamua kubadilika kimfumo na kucheza mpira nadhani tuna timu nzuri kuliko timu yeyote EPL.
Kikosi cha Man United kina mseto mzuri mno tatizo ni Kocha na Falsafa zake.
Hii imepelekea wachezaji wengi kucheza chini ya kiwango, tumeona kushuka kwa kiwango kwa Martial, Rashford n.k.
Kuna aina flan ya mpira tunaikosa pale Old Trafford, tunakosa consistency match baada ya match, tunashinda kwa bahati na si kwa soka.
Timu inakosa Creativity pale mbele ingawa tuna Pogba, Sanchez, Matic na Super Herera.
Sisi tunaolalamikia kocha shida yetu ni kocha kubadilika kifalsafa, kimbinu n.k ili wachezaji wawe huru uwanjani na kutupa matokeo tarajiwa.
Tukumbuke mifumo yote huanzia katika eneo la Kiungo, sioni matumizi sahihi ya Matic tofauti na msimu uliopita.
Binafsi niliamini kuifunga City kwao, rekodi za Mou ni ngumu kumfunga nje ndani, mara chache sana.