Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Salute sana mkuu
 
Tatzo la pogba hajui hata namba anayoweza kuimudu yupo yupo tu uwanjani kama shoga
 
Man City na Mpira Pesa.

Manchester City ndio kikosi kilichotengenezwa kwa kiasi kikubwa cha fedha katika Historia ya soka baada ya kutumia kiasi cha Euro Milioni 878 katika soko la usajili, kwa mujibu wa taarifa mpya za matumizi ya fedha.

Orodha iliyochapishwa na CIES Football Observatory inaonyesha kikosi cha Pep Guardiola ambao ni vinara wa Ligi kuu ya Soka ya Uingereza, wametumia kiasi kikubwa cha fedha zaidi ya klabu yoyote ile katika ligi kuu tano bora barani Ulaya, baada ya usajili wa mwezi huu Januari wa Pauni Milioni 57 wa beki Aymeric Laporte.

Uwekezaji wa City , umeupiku ule wa Paris Saint-Germain ambao umegharimu kiasi cha Euro Milioni 805, zaidi ya robo ya matumizi hayo yametumika kumsajili Neymar kwa rekodi ya usajili ya Euro Milioni 222 kutoka Barcelona.

Manchester United wanashika nafasi ya tatu katika orodha hiyo wakiwa wametumia kiasi cha Euro Milioni 747, juu ya Barcelona ambao wametumia Euro Milioni 725, Chelsea Euro Milioni 592 na Real Madrid ni Euro Milioni 497.

Kuna vilabu sita kutoka ligi kuu ya soka ya Uingereza katika orodha ya 20 bora vikiwemo vilabu vya , :

( Liverpool (€461m), Arsenal (€403m), Everton (€365m), Tottenham (€358m), Southampton (€229m) and Crystal Palace (€225m). )

Na wastani wa matumizi wa ligi kuu ya soka ya Uingereza upo kwenye thamani ya Euro Milioni 291, mbele ya Hispania , Euro Milioni 131, Serie A Euro milioni 124, Bundesliga Euro Milioni 113 na Ligi ya Ufaransa Euro Milioni 91.
 
Tumia pesa na wewe upate ubingwa issue za kusajiri kuna lindorf hizo ni za kijinga ndyo maana unakuja kulalamika ovyo Mara pesa
 
Arsenal huyo hahaha kashindwa hata kujibu
Nilikuwa majukumuni mkuu,mimi najikubali na chama langu hili hata tukienda comference naenda nalo mimi sio kama wale washabiki wa JIJI LA MANCHESTER wasaka ushindi....hahahahahaha
 
Naona unajisahaulisha ya jana kwa history za tangu uhuru hahahahahahahhh NEWCASTLE nyie hatari sana dah
 
Naona unajisahaulisha ya jana kwa history za tangu uhuru hahahahahahahhh NEWCASTLE nyie hatari sana dah

Mkuu baada ya kukujua utokako endelea kujiachia hapa ntakuunga mkono kwa kila post mana nafasi uliyopo inahitaji kufarijiwa droo 6 ushindi 6 ukishinda 6 ukipigwa 6 mkuu staki uzeeke mapema tufurahi
 
Hii picha ya kukata tamaa kabisa yani daa pogba young best player in europe 2013 and young Upcoming talented midfielder wa world cup 2014 tutampoteza tusipokuwa makin.
Mkuu pogba akijitambua akaacha kukata tamaa atakuwa mchezaji mkubwa mno ifike mahali mou amchezeshe tu namba 10
 
Hii picha ya kukata tamaa kabisa yani daa pogba young best player in europe 2013 and young Upcoming talented midfielder wa world cup 2014 tutampoteza tusipokuwa makin.

Lengo La Kuipost Hiyo Picha Ni Kuonesha Hapo Kuwa:-

• Ukimwangalia Hapo Utaona Kama Anaangalia Mpira, Lakini Ukimtazama Kwa Lakini utagundua Kuwa Yupo Kimwili tu hapo lakini Kiroho na Kiakili hayupo kabisa! Yuko mbali yani.

• Ukweli ni Kwamba Appearance yako hapo inaonesha Kuwa thare is something going on in his mind! Jamaa kuna Kitu kichwani bado kinaonesha Kumchanganya.

• Na Kinachomchanganya ni Wazi Kuwa kinaanza Kumuathiri Kwa Kumuondoshea Confidence awapo uwanjani kwani unaona Wazi Kuwa ni Miguu yake tu Ndiyo inayocheza Mpira lakini akili yake haichezi Mpira Wala haipo hasa Katika Mpira.
Tuache Chuki pembeni! Nibukweli usiofichika Pogba Hawezi Fichwa uwanjani na Dembele (vs Spurs) au Jonjo (vs NEWCASTLE)...

Mtazamo wangu:
√ Kubwa linalozungumzwa ni Kuwa Ujio Wa Sanchez's umemuathiri sana Kwenye Swala la Kimaslahi (Anataka awe na Salary Kubwa Kuliko Sanchez).

Lakini Kwa Maoni Yangu Mimi Najipa imani Zaidi Kuwa Jambo Linalo Mchanganya Ni Kuwa Haridhishwi na Roles and Responsibilities anazopewa na Mourinho uwanjani.
Ni Wazi Kuwa Angelifurahi apewe Majukumu Yaleyale alivyokuwa kakabidhiwa Juventus Kama ni "Creator".

Ni Wazi Kuwa Haridhishwi Kucheza Nyuma ya Wachezaji Wanne (Lukaku, Lingard, Martial and Sanchez) kwa mfano
Mfumo Wa 4-2-3-1.

Huenda ikawa Anapenda Arudishiwe Majukumu Aliyokuwanayo Juventus ambayo ni Sawa na Alivyokuwa nayo Coutinho Liverpool. Yani Mbele Yake Kusiwe na Watu Zaidi ya Wawili au Mmoja ili aweze Kuattack Zaidi Golini Kuliko Kuwa Central Playmaker.

Kama Hujanifahamu ni kuwa hi!
Coutinho alipokuwa Liverpool Kwenye Mfumo Wa 4-3-3 utakutia Kuwa Mbele ya Pana Watu Watatu → Salah - Firmino - Mane. Lakini hajawahi Kucheza Nyuma Salah Wala Alikuwa Hachezi Nyuma ya Mane! Bali alikuwa Akicheza Nyuma Ya Firmino tu! Kwahiyo Alikuwa Mipira Nusu anatengeza Chance kwa Washambuliaji (mostly Firmino), na Nusu Anajaribu Mwenyewe Golini ndiyo Mana Kaondoka Akiwa na Magoli 7 ya EPL huku akikosa Michezo tele kwa injury.

Tofauti na Pogba ambaye Anacheza Nyuma ya Sanchez, Lingard, Lukaku na Martial Jambo ambalo linamnyima Uhuru Wa Kuattack na Kuishia Kuwachumia Wao Wakiyakosa.

Huwenda Kuwa Anapenda Awe Nyuma ya Lukaku au Lukaku na Lingard tu.

"NI MTAZAMO TU"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…