Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kocha wa Manchester United, Jose Mourinho amedaiwa kuwa katika mipango kabambe ya kutaka kuwasajii nyota wawili wa Barcelona, Samuel Umtiti na Sergi Roberto.

Habari zinasema kuwa kocha huyo raia wa Ureno anadhani watu hao watasababisha timu yake iwe na ushindani mkubwa kuanzia Januari. Habari zinasema kuwa Roberto anaweza kupatikana kwa kiasi cha Pauni 35milioni na jambo hilo linaongeza uwezekano wa kutua katika klabu hiyo yenye maskani yake Old Trafford.

Suala la kuchukua ubingwa katika Ligi Kuu England msimu huu linaonekana kuwa gumu lakini kocha huyo hakati tamaa na anadhani kwamba kama wakishindwa kunyanyua ndoo basi washike nafasi ya pili.

Licha ya kutumia pesa nyingi kuwasajili nyota kama Romelu Lukaku na Nemanja Matic, katika dirisha la usajili lililopita, kocha huyo bado anaona nguvu iliyopo si ya kutisha sana.

Umtiti atakuwa mwiba katika safu ya ukabaji Roberto akionekana kuwa suluhisho katika nafasi ya kiungo.
 
FA imemuuliza meneja wa Manchester United kuelezea kauli zake alizosema kabla ya mechi ya Ligi Kuu Uingereza dhidi ya City uwanjawa Old Trafford
Jose Mourinho ametakiwa na Shirikisho la Soka kuelezea kauli alizosema kwenye vyombo vya habari kabla ya mechi kubwa ya Manchester.
Mreno huyo alishuhudia timu yake Manchester United ikinyukwa 2-1 na mahasimu wao Manchester City kwenye mechi ya Ligi Kuu Uingereza Jumapili ambapo baada ya mechi kulikuwa na tafrani nyingi kuelekea vyumba vya kubadilishia nguo Old Trafford.
FA tayari imeshaziuliza klabu zte kuhusu mtazamo wao katika tukio hilo, ambapo kwa mujibu wa habari Mourinho alimwagiwa maziwa.
Hata hivyo Mourinho amejikuta kwenye wakati mgumu kutokana na kauli zake alizosema kabla ya mechi, alipoishutumu City kwa kutumia ujanja kwenye mchezo, akisema: "Wakipulizwa kidogo na upepe wanaanguka."

Mourinho pia alidai kuwa City wanatumia "mbinu ya faulo" kuvuruga mchezo alipokuwa akizungumzia mechi dhidi ya hasimu wake wa siku nyingi Pep Guardiola.
Tangazo la FA inasomeka: "FA imeomba uchunguzi wa kauli za Jose Mourinho kwenye vyombo vya Ijumaa Disemba 8, kabla ya mechi ya Jumamosi dhidi ya Manchester City.
"Amepewa muda wa kujibu hadi saa kumi na mbili jioni Disemba 18 Jumatatu."

City walitoka kifua mbele, shukrani kwa magoli kutoka kwa David Silva na Nicolas Otamendi walioongeza pengo la pointi kuwa 11 kileleni mwa msimamo wa ligi.
Lakini klabu zote mbili zinaweza kuwa matatani, na huenda FA ikawashughulikia kufuatia tafrani iliyozuka kuelekea vyumba vya kubadilishia nguo ambapo wachezaji walikuwa wakitofautiana.
Inasemekana Mourinho aliingia kwenye chumba cha City cha kubadilishia nguo, akiwa hajafurahishwa na muziki uliopigwa baada ya timu ya Guardiola kuibuka na ushindi.
City na United zimepewa muda hadi Ijumaa jioni kutoa majibu kwa FA kuhusu mtazamo wao kwa tukio hilo.
 

kweli bado mtoto unaiuliza manchester ya 2008? na ya 99/2000 iliyobeba treble?


kisha utakuja kuuliza barcelona ya 2011had 2013 ipo?

au hujui mpira una transition yake na vizazi vyake?


punguza hasira na chuki tatizo mnapigwa sana na hiyo unayoiita united of manchester utapumua siku ukishinda 10-0


huyo pep mwaka jana hakuwepo? alibeba nini?
 
Kiungo wake wa Manchester United Paul Pogba naye amepiga picha na kuipakia kwenye Twitter kuonesha mtindo wake mpya. (Twitter).
 
Tetesi

Manchester United wameulizia kumhusu kiungo wa kati wa Chelsea na Brazil Willian, 29. (Daily Mail)
 
Tetesi
Barcelona wanataka kumnunua beki wa Manchester United kutoka Uholanzi Daley Blind, 27, bila ada yoyote mkataba wake utakapofikia kikomo majira ya joto. (Marca)
 
Tetesi
Manchester United watashindana na Juventus katika kutaka saini ya mchezaji wa Monaco na Brazil Fabinho, 24. (Tuttosport, kupitia Talksport)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…