baada ya kufungwa na Chelsea kwenye mechi ya FA nakumbuka nilitoa mawazo yangu kuhusiana na mwenendo wa timu yetu na miongoni mwa mambo niliyoyazungumzia ni kwamba hatuwezi kuifunga Chelsea mechi ya ligi kuu kama tutashindwa kumdhibiti eden hazard na pia nilisema ya kwamba hatuwezi kushika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi kuu kwa hivyo ni bora tupiganie kombe la Europa ambalo tumebakisha mechi 5 tu ili tuwe mabingwa na kujihakikishia nafasi ya kushiriki UEFA kuliko kupoteza nguvu nyingi kwenye ligi kuu ambapo tulikuwa tumebakisha mechi takribani 14.
kiukweli hili suala la kutokuwa na uwezo wa kupata nafasi ya nne lilikuwa ni gumu sana kwa baadhi ya washabiki wa humu ndani kulikubali nahii ilitokana na kuwa mashabiki wengi wao waliamini mechi bado ni nyingi na timu inaweza kufanya vizuri na timu pinzani kama Liverpool zinaweza kupata matokeo mabaya na ikawa ni faida kwetu.
naamini jose mourinho thread hii hajawahi kupita nawala haifahamu ila nashukuru mawazo yangu aliyafanyia kazi kwa sababu alitafuta dawa ya kukabiliana na hazard na pia alizidisha nguvu kwenye mapambano ya kuwania kombe la Europa na kilichotokezea kila mshabiki wa Manchester united kimemfurahisha.
wapo mashabiki wanaomkosoa mourinho kutokana na mbinu zake ila mimi naamini ndani ya mwaka mmoja wa utawala wake amerudisha ubora wa timu kwa 60% na naamini 40% zilizobakia atazikamilisha msimu huu.mimi binafsi nilipokuwa naangalia mechi za Manchester united hususan kwenye round ya pili nilifika wakati nilikuwa sina presha yoyote kwa sababu nilikuwa nayafahamu matokeo tutakayoyapata inawezekana tutapata ushindi au tutatoka draw ya goli moja. nilikuwa naamini hakuna timu yoyote yenye uwezo wa kutufunga goli Zaidi ya moja kwenye mechi na kumbukumbu zangu zinaniambia ukitoa mechi ya arsenal na tottenham ambazo kwangu mimi nazichukulia kama ni mechi za kirafiki sifikirii kama kuna mechi nyengine ambayo tuliruhusu bao Zaidi ya moja kwenye round ya pili na kiukweli haya ni mafanikio makubwa sana.
tatizo kubwa ambalo lipo ndani ya timu yetu ni umaliziaji wa mechi na hili ndio lililosababibisha tufanye vibaya kwenye ligi kuu,laiti kama tungelikuwa makini kwenye ufungaji basi mechi zote tulizotoka suluhu ndani ya old Trafford tulikuwa na uwezo wa kushinda wastani wa mabao (3-1).tunahitaji mshambuliaji ambaye ana uwezo wa kufunga magoli 25 kwa msimu,
wapo baadhi ya mashabiki wanamuona belotti anatufaa kwenye timu yetu, mimi sijawahi kumuona akicheza kwa sababu sijawahi kuangalia mechi ya torino ila napatwa na mashaka na wachezaji wa ligi ya Italy wanapokuja uingereza wanapata wakati mgumu sana kwa mfano Crespo, veron, Shevchenko, jovetic, savic, ballotelli wote viwango vyao havikuwa vizuri kama mashabiki walivyotegemea.
mimi naamini wachezaji hawa tulionao basi tuna uwezo wa kucheza robo final msimu ujao kwenye uefa na si kwasababu ni wachezaji wazuri sana ila sababu kubwa tuna mwalim bora ambaye anafahamu jinsi ya kuzitumia mechi mbili za mashindano ya uefa, Mourinho ndiye mwalimu pekee ambaye ana uwezo wa kuondoa huu utawala wa timu 3 uliopo kwenye uefa ambapo nawazungumzia real Madrid,Barcelona na Bayern munich. tunahitaji kufanya usajili kwa kuziangalia timu hizi ambazo ndio bora kwa kipindi cha miaka 6 mfululizo na si kuwaangalia timu kama Arsenal, Liverpool,Chelsea, Manchester city na tottenham wamefanya usajili gani, mimi hawa nawachukulia kama ni majirani zetu na si wapinzani wetu kwa sababu ni wachezaji wachache sana wanaozichezea timu hizi ambao wanaweza kupata namba kwenye vikosi vya real Madrid, Barcelona na Bayern munich.
ukiondoa tatizo la ushambuliaji pia tuna tatizo la upande mzima wa kushoto kuanzia beki tatu na winga, wapinzani wetu wako vizuri kwenye upande huu, real Madrid wana carvajal, bale, asensio ,isco.hivyo tunahitaji mlinzi bora wa kushoto kama rose wa tottenham na winga kama perisic wa inter milan na naamini kama atajikaza mourinho wote anaweza kuwasajili.
pia tunahitaji viungo wa kati ambaye atakuwa na uwezo wa kukabiliana na wachezaji kama modric,isco,vidal,rakitic,bosquet na wengineo na nafikiri bakayoko anatufaa kutokana na umbile lake na hata matuidi japokuwa ana miaka 30, kama tutaongeza viungo itakuwa ni faida kubwa sana kwetu kwa sababu tutapata kumtumia pogba na Herrera kwenye namba zao za asili.
Tafadhali jose mourinho turudishie heshima yetu na pia tuondolee huu utawala ninaouchukia wa timu za Hispania kwenye ligi ya mabingwa na yote hayo yanawezekana kwako wewe kwa sababu wewe ni:
bingwa wa tactics na uwezo huu umeuonesha kote ulipofundisha kuanzia porto, intermilan, Chelsea, na hata real madrid