Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Saa nyingine inaudhi sana mkuu, Kwa mfano yule Falcao ametanguliziwa fresh halafu anapiga nje... yaani anakosa sana zaidi ya kufunga sana ana kiwango kama cha Welbeck tu Toka atue Manchester United... Man U hata akicheza na timu ipo namna gani, game yake inakuwa ngumu...

Kikosi ukiangalia kwa macho ni kikali, lakini kiwango chao cha uchezaji hawana tofauti na zile timu cha chini yake... Van Persie ni striker mkali lakini kwenye top ile ya wafungaji hayumo... Wanamwangalia mtu anapiga danadana halafu anatupia, jana waliniudhi kama wale wa Ghana walivyokosa penati pamoja na kipa wao ambae hakupangua hata penati moja...

kwa kikosi hicho cha Man U ilitakiwa wawe wanasumbuana na chelsea pale juu... lakini eti wanagombea nafasi ya 3 na 4...
 
Manu sio wabovu sana tatizo ni team selection na tactics mbovu za kocha

Selection ipi mkuu unayotaka? Uko na RVP, Falcao, Di Maria, Januzaj na Rooney? mkuu mi nakubaliana na mdau mmoja hapo juu kwamba kwa kikosi cha ManU jinsi kilivyo ilikua inapaswa awe anatifuana na Chelsea lkn sasa ndo kwanza anagombania no3 na Soton! hii inashangaza kwa kweli km ilivoshangaza jana mmeweka full mkoko lkn mnashindwa kupata goli! Mnapata goli kwa taabu kweli..........nini shida iliopo kwa ManU? Hebu nisaidieni jamani maana haiwezekani na kamwe haitowezekana unakua na watu wazuri alafu unafanya vibaya!
 
Sawa wataalamu...

Siyo kazi ndogo kuvaa viatu vya SAF kama tunavyofikiri humu...

Hadi sasa leo la kurudi UCL mwakani bado lipo...uwezekano wa kumaliza top 4 bado upo...na hii ndiyo realistic target ya timu....hayo mambo ya kusema LvG alichukua makombe msimu wa kwanza katika timu alizopita, siyo ya kuyafikiria katika EPL...

Pamoja na mapungufu yake ya kibinaadamu, bado namwaminia LvG...tukianza fukuzafukuza ya makocha, timu haitokuwa stable kwa misimu 10 ijayo...

Tulizoeshwa raha sana na SAF, sasa tuonje shubiri kidogo ili tupate utamu misimu miwili ijayo..

Yangu ni haya tu..
 


Mkuu nakubaliana na wewe kabisa ktk maelezo yako lkn nashindwa kuelewa kwanini Nzi hayaoni haya? Bora ya RRONDO kaona lawama zote atupiwe Van Gaal na mimi naona Van Gaal au bench la ufundi linashida. Kabla ya mchezo wa jana niliona nafasi kwa ManU kua ktk nafasi ya pili kumekaribia maan km wangeshinda jana basi pengo la points kati ya Man City na ManU lingekua ni 3, alafu Tarehe 1 mwezi ujao City anakwenda kwao Liverpool huo mchezo nahisi city atapoteza na hapo ManU na City wangekua sawa kwa points na ukumbuka kua huyu City bado hajaja hapo OT. kitu amabacho akija hapo lazima City afungwe maana mchezo wao wa kwanza ManU akiwa ktk kiwango kibovu, City alimshinda ManU kwa makosa ya beki Chris kitu ambacho km ManU wangekua wote kamili uwanjani City alikua anapoteza ule mchezo....kwa hiyo nilivoona hivo nikaona ManU wana nafasi kubwa ya kua nafasi ya pili....lkn baada ya hapo naona vijana wa Big Sam wanamuabisha tena Van Gaal....ni shida mkuu. hizi timu zinatakiwa kujifunza kwa chelsea km zinataka kufikia hatua nzuri.




Kuhusu Ghana mkuu, mimi nawalaumu wachezaji kwanza then kipa. Haiwezekani Ivory Coast wamepoteza mikwaju miwili ya penati mfululizo alafu na badala ya wao kutumia hio nafasi kuua mchezo na wao wanafanya makosa hayo hayo. Alafu ktk dakika zote 120 Ghana wamemiliki mpira na kufanya mashambulizi mengik ktk lango la wenzao lkn tatizo la umaliziaji kwa Ghana limekua SUGU miaka yote. Maana kwenye viungo wako vzr sn mabeki alkadhalika wako poa sn kipa ndio hivo tena ako poa....shida inakuja ktk finishing tu. Wako poor sn ktk hilo swala. Wanapaswa kubadilika na kuangalia sn ktk swala la umaliziaji.
 
Last edited by a moderator:



Mkuu, binafsi namkubali sn huyu Mzee Van Gaal na pia sina maan kwamba afukuzwe lkn ananipa tabu sn kujiuliza kuna shida gani iliopo ktk timu yake wakati ana wachezaji wazuri na wenye uwezo mkubwa na ujuzi na uzoefu? Maana kwa kikosi alichopanga jana watoto wa Sam hawakupaswa kumsumbua kiasi hicho.



Km asipobadilika huyu Van Gaal na timu yote kubadilika, basi ata hiyo nafasi ya top four hamtoipata. maana Liverpool na Arsenal wanakuja na wao tena wameonekana kuimarika sn na Spurs pia na yeye anakuja wakati huo huo Soton anakomaa hataki kutoka hapo juu na kocha wao ameapa kugombania nafasi hiyo ya top 4 mpk mwisho wa ligi na kweli wanaonyesha uwezo wa kugombania hiyo nafasi......
 

Wachezaji wanachezeshwa out of position (Di Maria,Rooney) then Ander Herrera huyu ndio best creative midfielder tuliye naye huyu ndio anapaswa kucheza kiungo Rooney acheze no 10 au striker RVP/Falcao mmoja aanze benchi.Tulivyoanza ligi Di Maria alicheza winger,Rooney no 10 na Herera alicheza kiungo wote Di Maria,Rooney,Herrera walishine tulikuwa tunafunga magoli na kutengeneza nafasi nyingi tatizo lilikuwa defence now defence iko stable Rooney anachezeshwa kiungo,Di Maria forward,Herrera benchi kabisa
 



Mkuu Rooney kucheza nafasi ya kiungo ni jambo zuri sn km anamudu kufanya hivo na ni kweli Rooney ata wakati wa babu Alex alikua anacheza km Striker lkn alikua anashuka chini na kuchukua mipira na kuipeleka mbele na wakati mwingine huwachezesha wenzake na ndivo huyu Van Gaal anatumia uwezo wa Rooney kumpanga ktk hiyo nafsi kwasbabu anamudu vzr.

Kwa game ya jana Di Maria alicheza nafasi ya kiungo ingawa alipangwa katikati lkn hakucheza km forward kwasababu mbele yake kulikua na Falcao na RVP. Sioni km kwa kupanga hivo ni makosa kwasababu hii inasaidia sn timu ikiwa na wachezaji wa aina hii wakiwa wanashambuliua wanakua na ujuzi na uwezo mkubwa kwasababu ni nafasi ambazo ndio wanauzoefu zaidi.

Antonio Valencia ktk taifa lake alikua anacheza Striker wa katikati, alipokuja ManU Mzee Alex alimpanga kucheza winger wa pembeni na alifanya vzr tu na siku hizi Van Gaal anampanga huyo Valencia beki wa pembeni kulia na anafanya vzr anakaba na anapanda mbele anaingiza klosi nzuri na amewaweka bench kina Rafael. Mbona hili haulizungumzii? Kuna shida ingine mkuu na wachezaji hawajitumi huo ndio ukweli.
 

Acha unafiki...sasa downfall ya United wewe inakuuma nini? Si unapaswa ufurahie kukosa wapinzani ili uchukue ubingwa ama?!?

LvG ni binaadamu; hata SAF alichemsha mara nyingi kupanga timu...

Pamoja na kiburi chake, LvG ni mtu sahihi kuiweka timu sawa...hayo mengine ni mapito tu...

hizi timu zinatakiwa kujifunza kwa chelsea km zinataka kufikia hatua nzuri.

Ati nini?!? Doh! United ijifunze kwa rentboys? Acha masihara chifu...

Kuongoza ligi mnaanza kujiona mpo on top of English football?!

Yaani nyiye bado sana, labda miaka 200 ijayo...United itarudi mahala pake pa siku zote...

Rentboys zaidi ya kuongoza ligi, haina chochote cha kuishinda United! Sasa unataka United ijifunze nini kwa rentboys?!? Kuongoza ligi?!? Been there, done that..
 
Last edited by a moderator:

Kucheza kiungo Rooney kuna hasara kubwa kuliko faida,mpange kiungo kama huna option but tuna Herrera ambaye mwanzo alicheza vizuri,Rooney alicheza vizuri akicheza no 10 na alikuwa anafunga magoli.Falcao/RVP wanakosa magoli ambayo Rooney angeyafunga.Ukicheza na Stoke/West Ham ni timu zinazocheza mpira wa nguvu sana but kocha anampanga Januzaj while Mata na Fellaini wanakaa benchi.Game ya jana kocha alichemsha sana,kama tungefungwa mashabiki wangemzomea
 

Haya ndio matatizo ya mashabiki wa humu Jf. Pale mtu anapotoa mawazo yake kwa uhuru km mpenzi wa mpira mnaanza kumuita mnafiki mara sijui nini....ndio maana mnajifungia ktk thread zenu kwasababu sio wapenzi wa mpira.

Baadhi ya Wachambuzi wa soccer baada ya matokeo ya Man City na ManU na Arsenal na Liverpool wengi wamesema ili hizi timu zifikie hatua nzuri na nafasi nzuri msimu huu lazima wajifunze kutoka kwa Chelsea. Maana huwezi mchezo huu ukapata matokeo mazuri alafu mchezo ujao ukaboronga mbaya.
 



Poa mkuu nimekupata vzr mkuu Belo. Ngoja tuone Van Gaal atakavofanya mabadiliko ktk michezo ijayo. Ila kwa jana mkuu Van Gaal na wachezaji wake wametuabisha sn.
 
Last edited by a moderator:

Mkuu usilaumu mashaki, ukweli ni kwamba LVG anatuchosha kwa kubadili mfumo wa timu kila siku. Angalia game ambazo Rooney anecheza centre forward na De Maria amekimbiza winger huku fundi Carick kiungo.
Shida ya LVG ni kubadili mifumo na kuwapa mjukumu yasiyo yao wachezaji muhimu. Binafsi huyu babu ameshaanza kunichosha.
Nzi hapendi mabadiliko hata kipindi cha D. Moyes alifikia kutuita wengine humu si Man U fans.
LVG amekosa kujiamini ndiyo maana mechi na QPR ilibidi mashabiki waje juu 4 4 2 alipobadili mfumo ndiyo goli likapatikana.
 

Kuwa mpenzi wa soka na kutoa mawazo huru hakuna mahusiano yoyote....

Kwa sababu kiukweli United haina cha kujifunza kutoka kwa rentboys...rentboys washukuru timu nyingi haziko vizuri msimu huu..ila mpira wao wa kawaida sana...mpira wao umezidiwa hata na uliokuwa ukipigwa na Liverpool msimu jana...

Na hakuna mahala popote panaposema ni lazima mtu kuchangia kwenye majukwaa yote..nitachangia jambo ambalo nalitaka mimi...sina haja ya kuchangia mahala ili nionekane ni mpenzi wa mpira ebo!

Hao wachambuzi wa soka ni binaadamu kama sisi, hawana authority ya kuwa quote kama wao ni miungu watu...waliyoyasema ni mawazo yao kama yangu na yako...

Ndiyo maana nilisema haya na mawazo yangu...sasa kama hukubaliani nayo ni sawa kabisa...lakini siyo kuniambia sijui wachambuzi wa soka!!! Wachambuzi wenyewe kina Merson, Jamie na Chogo?!?
 

ndiyo ndiyo tuko pamoja mkuu, kama LVG hata badilika atakutana na mabandiko kama DM.
 



Nilipita kuwasalimu tu humu ndani lkn naona mnajaa upepo kweli. Mtasubiri sn safari hii zama zenu kwishiney.....shaja na mongo gwa le Simiyu. Babu Alex wamchezo
 
Nilipita kuwasalimu tu humu ndani lkn naona mnajaa upepo kweli. Mtasubiri sn safari hii zama zenu kwishiney.....shaja na mongo gwa le Simiyu. Babu Alex wamchezo

Sawa..zama kwishney..lakini itawachukua miaka 200 kuzisogelea zama hizo...kwani sasa timu zote zinaishi katika kivuli cha United...United ilisha-set benchmarks, kazi kwenu...
 
Nilipita kuwasalimu tu humu ndani lkn naona mnajaa upepo kweli. Mtasubiri sn safari hii zama zenu kwishiney.....shaja na mongo gwa le Simiyu. Babu Alex wamchezo

Afadhali sisi tulikuwa na zama sasa zimeisha nyinyi hamjawahi kuwa na zama wala enzi....no history,no class...plastic fans damn rentboys!
 
Afadhali sisi tulikuwa na zama sasa zimeisha nyinyi hamjawahi kuwa na zama wala enzi....no history,no class...plastic fans damn rentboys!



Na wewe unaandika hivi sio? Poa utakuja kwetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…