Itakuwa sio haki Kama Pazi hakuja kusema Hongera hapa Hongereni Mmetufundisha mpira kwa mengi Leo kuna game mtu unaomba ziongezeke dk 5 au 6 Mrudi ila hii mtu unaomba uishe tu aibu tupu Man United mmetuweza kila pembe mpaka kwa Refa inaonyesha vipi tumekuwa wabovu ila cha zaidi nimejifunza kitu Manchester United ni Manager Leo nimeona kwanini David Moyes kufukuzwa Moyes angebaki Manchester United wasingepata Di Maria,blind,Falcao,Rojo japo hao hawakuwepo na wangekuwepo basi 5 mtu Kama Brendan Rogers na. David Moyes timu zao ni zile zile kina Swansea na Everton kila usijifanya roho ngumu Manager Kama hao Kubaki nao ndio timu inakuwa Kama Swansea au Everton au mbovu zaidi kwanza wachezaji wa nje wakitizama mtu Kama David Moyes au Brendan Rogers hawaji haijalishi Man U kubwa vipi au Liverpoolfc Kubwa vipi tuliona David Moyes alivyokuwepo Man U alikosa wachezaji na tunaona Brendan Rogers pesa zote zile kapata wachezaji si wa kipaji cha Top 4 wala top 10 utumbo mtupu...... Sasa nimeona bora hata Kenny Daglish alikuwa anajuwa ku win Cup Liverpoolfc watafute Manager wa Nje sasa hivi kwajili ya January la sivyo kushuka daraja ndio nafasi kubwa kuliko hata Kuwa top 10 hii LFC tunaongelea Top 10 ni aibu.... hongera Man United Hongera Van Gaal na timu yake hongereni Nzi Belo na. DonDonald na Wenzenu asanteni kwa kumuweka Brendan Rogers nje ya Mlango wa Anfield na Arsenal mashabiki Kama mnasema hapa msiombe kumfukuza Arsene Wenger mtajutia hasa mkichukuwa Manager wa EPL ambao wamefanya tu vizuri msimu miwili mtajutia.