Smartbeing
JF-Expert Member
- Apr 7, 2014
- 323
- 426
Umofia kwenu,
Leo nipende kuleta kero ya baadhi ya mamonita madarasani. Hii inahusisha mamonita wa shule za kata hadi zile za private ambao kwa kweli wanatumia nafasi na madaraka yao vibaya. Tunafahamu kuwa ninyi ni viongozi wetu wa madarasa lakini tunaona kuwa kuna mambo mnahitaji kujua.
Mosi, mmekuwa mamonita sio kwa sababu mna akili kuliko wote darasani au mnajua sana kuongoza, hapana wengine ni kwa sababu tu mmeteuliwa na mwalimu wa darasa kutuongoza na wengine ni watoto wa walimu tu na pengine angeweza kuchaguliwa mwingine kama tungepiga kura vizuri sema tu mara nyingine tunakuwa hatuna option ya kuchagua.
Pili tabia yenu ya kutuziba midomo hatupendi. Mara nyingine somo darasani linakuwa zuri tunapenda kujibu maswali au kumuuliza mwalimu lakini hampendi tufanye hivyo mnapenda muulize wenyewe na mtuulizie hata yale ambayo mnadhani ndo maswali yetu kumbe sio.
Tatu kutulazimisha tuwafanyie majukumu yenu mfano kuwaandikia notisi ambazo ni jukumu lenu, kuwahi namba kwa ajili yenu halafu hamna shukrani.
Finally niwaombe viongozi wa madarasa muache kunyanyasa wenzenu, na tukiwaeleza ukweli muache kutuandika kwenye listi ya wapiga kelele. Have a good day
NB: Sio viongozi wote wa madarasa ni wabaya wengine, huwa wanakubali hata kuchapwa kwa kosa letu ili mradi wasitutaje tukizingua darasani.
Leo nipende kuleta kero ya baadhi ya mamonita madarasani. Hii inahusisha mamonita wa shule za kata hadi zile za private ambao kwa kweli wanatumia nafasi na madaraka yao vibaya. Tunafahamu kuwa ninyi ni viongozi wetu wa madarasa lakini tunaona kuwa kuna mambo mnahitaji kujua.
Mosi, mmekuwa mamonita sio kwa sababu mna akili kuliko wote darasani au mnajua sana kuongoza, hapana wengine ni kwa sababu tu mmeteuliwa na mwalimu wa darasa kutuongoza na wengine ni watoto wa walimu tu na pengine angeweza kuchaguliwa mwingine kama tungepiga kura vizuri sema tu mara nyingine tunakuwa hatuna option ya kuchagua.
Pili tabia yenu ya kutuziba midomo hatupendi. Mara nyingine somo darasani linakuwa zuri tunapenda kujibu maswali au kumuuliza mwalimu lakini hampendi tufanye hivyo mnapenda muulize wenyewe na mtuulizie hata yale ambayo mnadhani ndo maswali yetu kumbe sio.
Tatu kutulazimisha tuwafanyie majukumu yenu mfano kuwaandikia notisi ambazo ni jukumu lenu, kuwahi namba kwa ajili yenu halafu hamna shukrani.
Finally niwaombe viongozi wa madarasa muache kunyanyasa wenzenu, na tukiwaeleza ukweli muache kutuandika kwenye listi ya wapiga kelele. Have a good day
NB: Sio viongozi wote wa madarasa ni wabaya wengine, huwa wanakubali hata kuchapwa kwa kosa letu ili mradi wasitutaje tukizingua darasani.