Jose mmali
Member
- Jan 13, 2014
- 17
- 2
binafsi naomba niweke wazi huyu jamaa mimi sio mpiga kura wake!
lakini kwa tetesi zilivyo ndani ya chama chake hakuna wa kumzuia na kibaya zaidi tumebaki wapinzani kuzungumzia huyu jamaa hafai ccm haifai lakini bado sijaona nani atasimama na huyu mtu ikiwa wadanganyika tushazoea kuuza utu wetu kwa fedha! hii ni hatari sana!
jamaa amejipanga na kunatetesi watu wa kaskazini haijalishi wanatoka chama gani ilimradi anatoka huko wengi wako tayari kummunga mkono
sasa sijui wana siasa wanatupeleka wapi wameamua kabisa kwa roho moja kupeleka gari letu mtaloni.
Mi mwenyewe kura yangu hapati. Kwa mtu anayetumia akili yake vizur kwa matumiz anayotumia kununua wapiga kura lazima upate shaka. Lkn watz tulivyo wavivu kufikiri hilo hatulioni eti ni mchapakazi, mchapakazi amekuwa sokoine huyu? Mchapakazi au mchapa mabilioni?