Mambo ya X

pamoja mkuu!mwanaume huwezi ruhusu ujinga kama huo!yaani hii iko very close to murder case!dk 2 tu unatoa mtu roho!

Kama uanaume ni kukubali kujionyesha kabisa umeshindwa kuhimili pressure iliyokusudiwa... Nadhani unahitaji msaada wa kisaikolojia..
Na huyo X atacheka kwa dharau pia..

Sema,kwa kuwa ujinga kautaka huyo X,hapo wajanja ni kumtonya M/kiti awe aware huyo ni nani,na kwa busara zake anaweza kumhandle huyo X..

Kwa mfano,anaweza akamuembarass kwa kumwambia aongeze hata Mil 5 zaidi kama kweli ameletwa kwenye kikao hicho kwa dhamira ya kuchangia basi aongeze kiasi hicho...
Au,kuandaa mazingira,kumwambia tu kwamba yeye kama ameamua kuwa mjumbe kwenye kamati basi aheshimu kiti cha M/kiti,kwa hiyo kauli ya kusema anamalizia kiwango kilichobaki kina chembe ya unafiki na anaambiwa kwa mila za kabila la bwana harusi mtu wa aina hiyo hupigwa faini ambayo kiongozi wa ukoo hukadiria au anaweza kumwachia jukumu hilo M/kiti...
Hapo mnamtoza twice the amount au thrice kama hajajikojolea huyo jamaa...
 
just take the baksheesh for the job well executed............uchukue usichukue bado huna sauti hapo........
 
Usifanye mchezo na ugonjwa wa moyo,Kumjua tu jamaa aliyekuwa anagonga hiyo kitu before ni noma.Kila ukikutana naye pressure inapanda.HAKIYA NANI MOTO UNGEWAKA NA KIKAO KINGEVUNJIKA!!!!!

pressure ya nini mzee wakati jamaa labda ndiye aliyekufungulia makaratasi ya nailoni!
 
mtoa mada umenikumbusha mbali kwenye mid 80's,kuna dada alikuwa na bwana mme wa mtu,baadae akachumbiwa na kijana mwenzie,msomi lakini ndo hivo tena kipato enzi za mwalimu.Mshefa alidhamini pambano fully lakini kwa dharau nyuma ya kadi aliandika...'printed by...' kisha akaweka jina la kampuni yake.Maisha haya....tumetoka mbali...enzi hizo harusi ukumbi taasisi ya elimu bibi titi au AVI bamaga.
 
huyo x hana akili.

Kabisa Mkuu Chauro. Unaenda kuhudhuria kwenye kikao cha harusi ya X wako ili iweje!? Kama ni mtu mstaarabu huwezi kabisa kuhudhuria kikao cha harusi ya X wako huku ukijua fika kwamba kuwepo kwako kunaweza kabisa kuanzisha varangati la kufa mtu. Mwenye akili za kushikiwa tu ndiye anaweza kuhudhuria.
 
Wewe unatarajia kuoa hivi karibuni!upo ktk kikao chako cha harusi,mmepanga bajeti ni 12m!Bwana harusi umeanza ahadi yako kwamba utatoa 3.5m!wanakamati wawili watatu nao wakatoa ahadi zao!Sasa unajua tena haya mambo ya marafiki kuleta watu pengine wasio rafiki zako ktk kikao wachangie kumbe mmoja wa marafiki zako kamleta X-boyfriend wa mchumba wako mtarajiwa.

Ikafika zamu ya x wa mtarajiwa wako huku nawe ukiwa unajua jamaa alikuwa anakula mzigo wako,jamaa kwa mbwembwe akauliza so far ahadi ya bw harusi na wanakamati wengine ni sh ngapi?ikaonekana jumla ni 5m!jamaa papo hapo akaahidi kutoa pesa yote iliyobakia yaani 7m yaani mara 2 ya pesa uliyoahidi wewe bwana harusi!kama hataki vile jamaa akatoa cheque book ya kampuni yake ambayo mchumba wako alikuwa akifanya kazi enzi ya mahusiano yake na jamaa hapo awali!Jamaa akaanguka saini akakukabidhi cheque ya 7m!

JE UTAIPOKEA?UTAMWAMBIA MCHUMBA WAKO KUWA X WAKE KATOA KIASI HICHO CHA PESA?AU UTAMTOA NDUKI JAMAA?
Baba yangu kabla hajafa aliniambia kuna vitu viwili tuu ambavyo sitakiwi kususa chini ya hili jua navyo ni pesa na chakula,nitaipokea tena na shukrani tele nitampa,hakuna kaburi la mjinga bwana!!!
 
Hii inawahusu wanaoowa kwa michango, ukikubali kuoa kwa mchango, ukubali kuchangia na mkeo.

Mimi sikubaliani na michango ya harusi wala mazishi, sijawahi kutoa, sitotoa, na sitochangisha. Iwe ya harusi au ya maziko. Ni upunguani tu.

Dah.... Nimeipenda sana. Yaani full msimamno
 
shida iko wapi na pokea hiyo check kama hatakua analake jambo atajiju,tenda ndo vizuri atakuwa ametupunguzia gharama za kuchanga!
 
Pokea manake yaliyopita si ndwele! Kuacha kupokea ni kuonyesha kuwa hujiamini, pokea na uende ukamwambie mchumba ako bila woga! Ukisita utamfanya jamaa arudiane na mkeo mtarajiwa..

aah wapi.....wakirudiana ujue wametakana tu na walikuwa wakitamaniana!!yaani mimi sijui nina tatizo,siamini kabisa kwenye kkuibiwa,kwasasbabu yoyote ile!sisi wengine our ego ni kubwa na ndefu kuliko majengo pacha ya b.o.t!kwanza mi kupokea hiyo cheki ngumu sana aisee!
 
Kwani kumwambia ni vibaya? Kwamba unaona kama mkeo mtarajiwa ataona jamaa ana hela zaidi yako then amrudie ama? Usipomwambia manake ni kwamba hujiamini...

kwani nisipomwambia ndo hatajua kama jamaa ana mpunga mrefu kunizidi!!?afu huyo wife to be anaolewa na mimi au na cheque book yangu!!?anapokuja kwangu na mpaka kufikia hatua hiyo anakuwa ananifahamu vizuri,kiwango changu cha maisha,ndoto zangu na mipango yangu yote ya muda mfupi na mrefu,sasa wasiwasi wa kuibiwa unatokea wapi!?akiamua 'kuibiwa' (siamini kama hii ni sahihi)ni uamuzi wake binafsi na anaweza vua ka-Victoria Secret kwa yeyote tu hata house boy wangu!mi sifuatilii mtu hakyanani,kama anafungua miguu kwa yoyote tu,all the best mradi nisimkamate,nikigundua itategemea na hali yangu kwa wakati huo ikoje(kama madhara ya cha- Arusha yamepamba moto au vipi).....lol!!
 
mie napokea tu, namshukuru na kukiwa na umuhimu wa kumuambia wife kuwa ex wake ametoa mchango huo haina shida namuambia...... issue ni TRUST between you two

TRUST..!!???yaani unamwamini huyo 'mkeo/mchumba wako'!??.......sikushauri babu!we ishi tu maisha yako to te fullest,enjoy unapopata muda na epuka kujipa stress kuwaza kumchunga mtu mzima,hususan mwanamke bab.amini uko pekee tu(manake trust yourself) na furahia maisha.wacha kabisa hii mambo ya trust sijui nini!
 
Unaweza kupokea lakini hakuna sababu ya kumwambia huyo mkeo mtarajiwa, kwani inahusu nini ajue umechangiwa na kina nani. ila tia akilini kua mara nyingi ma-x hukumbushana mara moja moja hasa wote wakishaingia kwenye ndoa.

sweetlady?umeolewa?jibu swali la nyongeza nililouliza!au niliweke kwa upande wako ili upate hisia zake!x wa mmeo mtarajiwa kajitolea kumnunulia suti ya harusi mmeo mtarajiwa na honeymoney atawapeleka kwa gharama zake!UTAKUBALI UACHIWE KUMBUKUMBU YA AINA HIYO FOR THE REST OF YOUR LIFE?fikiri kabla ya kujibu
 
Back
Top Bottom