Mambo ya Kuzingatia ili Wananchi watoe taarifa kwa Uhuru

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,377
8,120
Wajibu wa kutoa taarifa juu ya uhalifu ni wa kila mmoja wetu ambaye anajua au amesikia kuhusiana na tukio lolote la kijinai.

Tumeona katika makala iliyopita juu ya changamoto zinazowafanya watu au wananchi kutokuwa wepesi kutoa taarifa za uhalifu katika maeneo yao. Leo tunaangalia juu ya mambo ya msingi yanayoweza kufanywa ili watu kuwa na utayari wa kutoa taarifa za uhalifu mapema kwa vyombo husika.

1. Mfumo wa utoaji taarifa
Kama tulivyoona kwa mujibu wa sheria mtoa taarifa anapaswa kuwasilisha taarifa za uhalifu kwa kituo kilicho karibu yake. Hatahivyo uzoefu unaonesha mazingira ya uwasilishwaji wa taarifa hizi si rafiki sana kwa watoa taarifa. Kutokana na maendeleo ya kisayansi na teknolojia, mamlaka zinapaswa kuanza kutumia mbinu nyingine za ukusanyaji wa taarifa za kihalifu ambazo watoa taarifa wataona wapo salama zaidi. Mfano taarifa zinaweza kutolewa kwa njia ya simu, au ujumbe mfupi au barua pepe au barua pasipo kudhihirisha utambulisho wa mtoa taarifa. Ni kazi ya mamlaka kuchunguza endapo taarifa hizo zinaweza kuwa za ukweli na kuzuia uhalifu kujitokeza mahali.

2. Usiri wa mtoa taarifa
Hofu kubwa kwa watoa taarifa ni hali ya usiri wa taarifa wanazotoa. Ni muhimu sana kwa mamlaka zinazopokea taarifa za uhalifu au matukio kujua namna ya kutunza siri za watoa taarifa zao. Ni lazima watu wanaohusika na uchunguzi wa taarifa hizo wawe waaminifu kuhakikisha kuwa mtoa taarifa analindwa kutokana na taarifa alizotoa endapo zitasaidia kuzuia uhalifu au kuwakamata wahalifu.

3. Ushirikiano na watoa taarifa
Watoa taarifa wamekuwa na malalamiko juu ya wao kusumbuliwa na mamlaka kwa taarifa wanazotoa. Ni muhimu watoa taarifa kupewa ushirikiano kama wasaidizi wa kuzuia uhalifu na si kama wahalifu wenyewe. Zipo harakati na juhudi zinazofanywa na mamlaka kuweka ukaribu zaidi na jamii ili kusaidia jamii kuona wajibu wa kuzuia uhalifu kwani waathiriwa wakuu ni jamii husika.

4. Ulinzi wa kisheria kwa watoa taarifa
Kwa muda mrefu kumekuwa na jitihada za uundwaji wa sheria maalum ya ulinzi juu ya watoa taarifa. Jitihada hizi zimefanikiwa na Bungu limetunga sheria hii maalum kwa ajili ya ulinzi wa kisheria kwa watoa taarifa mbalimbali zinazoweza kuzuia uhalifu au kubaini wahalifu.

Hitimisho
Kama tulivyoona ya kwamba suala la utoaji wa taarifa za uhalifu ni jukumu la kila mmoja wetu mwenye kujua taarifa husika. Ni muhimu sana kwa wananchi kuwa na imani na vyombo vya uchunguzi ili taarifa zinazotolewe zilete tija na kuzuia uhalifu katika jamii. Pia vyombo vinavyohusika na uchunguzi vinapaswa kuchukua taarifa za uhalifu kwa umakini na usiri huku wakizifanyia kazi kwa weledi wote.

Kwa ushauri zaidi usisite kuwasiliana nasi kama inavyoelekezwa hapo chini katika makala hii.

Kumbuka ‘kutokujua sheria si utetezi iwapo utatenda kosa lolote tafuta maarifa sahihi ya kisheria yakusaidie kufanya maamuzi sahihi kila siku.
 
Hapa jirani wapo wauza piwa, siku moja walikamatwa, yaani kabla ya kufikishwa kituoni washaambiwa wakiowataja.
 
Back
Top Bottom