Mtafiti77
JF-Expert Member
- Oct 31, 2011
- 1,938
- 2,353
Mjini bwana binadamu ni wabaya kuliko majini usipofuata principal zilizopo utaangukia pabaya. Moja kati ya mambo unayohitajika uepuke kwenye matembezi yako usiku ni:
1. Epuka kutembea kwa vikundi hasa vya watù wachache 3-5 usiku, mjini bwana mob yenu inaweza kufananishwa na kikosi kazi kilichovamia maeneo fulani alafu wote mkamiminiwa risasi au kusekwa ndani. Mwendo wa solo ni wa kioga ila unaweza kukuokoa.
2. Epuka wakati wa kuongea na simu kuweka simu sikio lililoangalia barabarani, bodaboda wataipitia ndugu yangu wavuruge matumizi ya mshahara wako ujao.
3. Epuka kupita sehemu za madada poa wanaojiuza kwani huko polisi hupita mara kwa mara kubeba watakao watuliza njaa, mitaa kama ya Sinza midnight iepuke. Pia madada poa wa kuzidiwa njaa wanakuitia mwizi wanakupiga tukio, huko nyuma watu wanakuua.
4. Epuka kukimbia kimbia bila sababu utaunganishiwa kelele za mwizi aliyejificha sehemu, wananchi mpaka wajue sio wewe utakuwa umeivaa.
5. Epuka kutembea bila kitambulisho aise, hii itakusaidia ukikamatwa na mamwera, ukipata ajali usiku au tatizo lolote ni rahisi sana kuhudumiwa na ndugu zako kupewa taarifa.
Chunga sana pindi inapofika usiku!! Usiku!
Nipe tahadhari nyingine hapa!!
===
Ikiwa ni usiku mkali kabisa, vua nguo, tembea uchi. Imba wimbo wenye maudhui fulani hivi, mfano, kifo hakina huruma wa Dkt. Remmy Ongala




