Mambo ya kuchunga ukitembea mjini usiku

Mambo ya kuchunga ukitembea mjini usiku

Mjini bwana binadamu ni wabaya kuliko majini usipofuata principal zilizopo utaangukia pabaya. Moja kati ya mambo unayohitajika uepuke kwenye matembezi yako usiku ni:

1. Epuka kutembea kwa vikundi hasa vya watù wachache 3-5 usiku, mjini bwana mob yenu inaweza kufananishwa na kikosi kazi kilichovamia maeneo fulani alafu wote mkamiminiwa risasi au kusekwa ndani. Mwendo wa solo ni wa kioga ila unaweza kukuokoa.

2. Epuka wakati wa kuongea na simu kuweka simu sikio lililoangalia barabarani, bodaboda wataipitia ndugu yangu wavuruge matumizi ya mshahara wako ujao.

3. Epuka kupita sehemu za madada poa wanaojiuza kwani huko polisi hupita mara kwa mara kubeba watakao watuliza njaa, mitaa kama ya Sinza midnight iepuke. Pia madada poa wa kuzidiwa njaa wanakuitia mwizi wanakupiga tukio, huko nyuma watu wanakuua.

4. Epuka kukimbia kimbia bila sababu utaunganishiwa kelele za mwizi aliyejificha sehemu, wananchi mpaka wajue sio wewe utakuwa umeivaa.

5. Epuka kutembea bila kitambulisho aise, hii itakusaidia ukikamatwa na mamwera, ukipata ajali usiku au tatizo lolote ni rahisi sana kuhudumiwa na ndugu zako kupewa taarifa.

Chunga sana pindi inapofika usiku!! Usiku!

Nipe tahadhari nyingine hapa!!


===



Ikiwa ni usiku mkali kabisa, vua nguo, tembea uchi. Imba wimbo wenye maudhui fulani hivi, mfano, kifo hakina huruma wa Dkt. Remmy Ongala
 
Kuna uzi ulianzishwa ukiuliza Kama Kuna mtu amewahi kuipata simu yake iliyoporwa kwa kutumia cyber polisi yaani kitengo maalumu Cha kufuatilia simu polisi.

Baada ya comment Kama 10 hivi akajitokeza mwamba na ushuhuda mzuri wa kuipata simu yake kwa kuandik id ya huyo yoashi aliyepo humu jf kwamba ndie mtaalamu wa Mambo hayo.

Ghafra Yoashi akaja na mbwembwe zote kwa kujinadi, hiyo Ni kazi ndogo San kwake licha ya baadhi ya wadua wakisema Kuna baadhi ya simu zikibadilishwa imei huwezi kuzipata.

Jamaa akaonesha umwamba wa kibabe pale na akaalika wenye matatizo ya kutafutiwa simu tumuone PM.

Aisee, alitulamba pesa wakubwa kwa wadogo then akapotea hewan mpaka Leo.!!!

Kwanza sipendagi kkumbuka ka hela kangu dah..!
Bora ningenunulia kiatu na suluali kadeti Safi!!
jf kuna watu matepeli,basi tu
 
Kuna sehemu inabidi uvue shati ubaki kifua wazi tena shati unachomeka mfuko kwa nyuma ndiyo unavuka kama ni reli au darajani, hii huwafanya wezi waliojificha wataendelea kujificha na kuendelea kukutazama bila kuelewa kinachoendelea na kusahau lengo lao la kukuibia.
 
Ukitembea usk hakikisha unavaa mzula na koti refu, Hakuna atakaye kusogelea kila mtu anakukimbia,afu unatembea Taratibu

Hakikisha hukosi bisibisi Au ka kisu.

Natembeaga ata saa nane wauni wakiniona ata wakiwa kikundi wanakimbia Kwa speed, laiti wangejua afu nakuwaga mdg mdg
 
Ukiona mtu anaiba kwa kutumia akili ujue msomi inawezekana ana form six, Masters au digrii.

Ukiona unakabwa roba ujue vibaka wa darasa la saba.

Mimi ni Bora nikutane na msomi aniibie kwa ujinga wangu japo inauma, ila sio hawa vibaka wanaweza kuua hawanaga hasara.

Mwingine yupo humu anaitwa yoashi alitupiga humu JF siji sahau.!! Alikuja na ishu ya ku track simu zilizo ibiwa.
Dah acha tu.!

Usiwaamini watu humu mtandaoni pole sana
 
Kuna siku ilinikuta hiyo, namwaga mkojo sehemu nikamwona jamaa ananifukuzia nilitoka nduki huku dudu inaning'inia umbali wa Km 1 hv nilikuja kui-park vzr baadae sana baada ya kuwa sehenu salama.... Arusha hiyo mzee!!
 
Kuna sehemu inabidi uvue shati ubaki kifua wazi tena shati unachomeka mfuko kwa nyuma ndiyo unavuka kama ni reli au darajani, hii huwafanya wezi waliojificha wataendelea kujificha na kuendelea kukutazama bila kuelewa kinachoendelea na kusahau lengo lao la kukuibia.
Ila kweli aiseee
 
Kuna sehemu inabidi uvue shati ubaki kifua wazi tena shati unachomeka mfuko kwa nyuma ndiyo unavuka kama ni reli au darajani, hii huwafanya wezi waliojificha wataendelea kujificha na kuendelea kukutazama bila kuelewa kinachoendelea na kusahau lengo lao la kukuibia.
hizi staili za masela mavi a.k.a masela nnya upenda kuvua shati lake analikunja na kuliweka kwenye mfuko wa suruali wa nyuma

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Kuna siku ilinikuta hiyo, namwaga mkojo sehemu nikamwona jamaa ananifukuzia nilitoka nduki huku dudu inaning'inia umbali wa Km 1 hv nilikuja kui-park vzr baadae sana baada ya kuwa sehenu salama.... Arusha hiyo mzee!!
kijana umenichekesha sana au ulikojoa ile sehemu inaitwa,, MARUFUKU KUKOJOA HAPA

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom