jMali
JF-Expert Member
- Nov 9, 2010
- 8,412
- 5,013
- Thread starter
- #41
Mkuu jmali ukweli lazima tuuseme hata kama haupendi kuusikia you are not a Tanzanian and you will never being a Tanzanian,nimefurahi uliponiita mtutsi na baadae ukasema wahutu walioko congo ni ndugu zangu ni kweli wote ni ndugu zangu kwasababu naamini binadamu wote ni sawa ndio maana damu ya mhutu hospital anaongezewa mtutsi and vise versa.Nakubaliana nawewe kwamba katika vita ile 1994 walikufa wahutu,watwa na watutsi,ingawa watutsi waliuawa kwa idadi kubwa lakini walipochukua madaraka waliamua kusamehe na kuunda serikali ya wanyarwanda wote.toka mwanzo pointi yangu ni kwamba fdrl wanapaswa kusamehe ili waweze kusamehewa warudi kwao na kuendeleza mshikamano nchini mwao,leo hii rwanda hauwezi kusikia mtu anasema huyu ni mtutsi ama mhutu wanatambuana kwa utaifa wao wanyarwanda tu.
Nilishasema kuwa mkitaka niwe mhutu au mmasai sina shida as long as mnajadili kwa hoja. Tatizo lenu hoja hamna mnabaki kuita watu wahutu as if uhutu ni tusi fulani hivi huko kwenu, hicho ndicho tunashoshangaa watanzania.
Pili, si kweli kuwa watutsi walikufa wengi 1994, waliokufa wengi ni wahutu. Watutsi walikufa kwa genocide wakati wahutu waliuawa na majeshi ya RPA. Waliochukua madaraka sio watutsi wa rwanda bali watutsi wa uganda na diaspora ambao walikuja baada ya kagame kuchukua nchi. Hawa hawajamsamehe yoyote kwa sababu majority yao walikuwa wamelowea nchi za watu for generations, hawana hata kijiji wanachokijua, let alone ndugu yoyote aliyeuwawa. Watutsi na wahutu "original" kina kizito mihigo and company ndio waliosamehe wahutu walioua ndugu zao, tatizo ni kuwa wahutu hawajasamehe kwa sababu RPA inalazimisha kuwa ndugu zao waliouawa bila hatia walikuwa ni interahamwe/wauaji wa kimbari. Utulivu sio kiashiria cha amani, watu wanaweza kuwa wametulia kumbe wana yao moyoni. Watutsi wamepata haki kwa sababu wauaji wao wameshitakiwa, wahutu hawajapata haki kwa sababu ndio kwanza wauaji wao wanaendesha serikali. Hivi unadhani mhutu aliye-survive kibeho massacre anajisikiaje akimuona kagame?
Tatizo lingine ni hili la FDLR. Hata mushikiwabo na wenzake wanakubali kuwa majority ya hawa FDLR sio interahamwe, wala sio wauaji ndio maana hata wengine wanarudi na kuishi rwanda baada ya kuachana na FDLR. Sasa wewe unayekaa bongo unasemaje FDLR wasamehewe? For what? for being born hutu? for being born refugees? for what exactly? for what crime? Wauaji wote wa kimbari wanajulikana wameshashitakiwa ICTR na gacaca courts, some of them ambao hawajapatikana bado wanatafutwa, lakini orodha ipo. Hakuna FDLR member hata mmoja aliyeshitakiwa ICTR wala gacaca courts, wasamehewe kwa kosa gani? Acha ukabila. Unajua chuki inamtafuna mtu aliye nayo kuliko hata huyo anayechukiwa. Ushauri wa bure huu.