Talkandtalk
JF-Expert Member
- Jan 28, 2014
- 291
- 184
Just for your information!RPF ilipigania WanyaRwanda warudi kwao kwani serikali iliyokuwepo ilikuwa haitaki warudi;na alikuwa anatoa the same reason kama unazotoa hapa, eti hakukuwa na resources?really? who is entitled to the nation resources? WanyaRwanda wote wana haki sawa kwenye resources za nchi, hivyo sio haki kubakisha some of them out as refugees, on the otherside sasa hivi hawa wanabembelezwa warudi tu share the little we have, na tusaidiane kuendeleza nchi yetu.1. Mambo ya DRC ni mambo mtambuka hivyo kulingana na unajadili nini lazima definition zibadilike kulingana na kinachojadiliwa, haimaanishi kuwa M23 kuwa sehemu ya FARDC hawana askari wa RDF ndani yao. Na haimaanishi kuwa Laurent Nkunda kuwa askari wa FARDC hakuwa askari wa RPA. hakuna nilichochanganya hapo.
2. Hapo kwenye hoja yako ya mtoto wa miaka 20, naomba nikujibu kwa mfano mzuri sana:
Paul kagame aliingia uganda akiwa amebebwa mgongoni akiwa na miaka 3, karudi Rwanda ameshika mtutu akiwa na miaka 37. Kwa nini muda wote huo wazazi wake hawakurudi Rwanda bila masharti? Kwani wazazi wa kagame walifukuzwa au waliondoka wenyewe baada ya mapinduzi? Mbona majority ya watutsi have always been in Rwanda, what made them stay in Uganda for all that time? vile vikundi vya tutsi insurgency vilikuwa vinawatumia kina kagame as human shields au? vinawazuia wasirudi kwao for all that time? Mi nadhani hawakurudi kwa sababu whatever it was walichokimbia bado kilikuwapo ndio maana waka-settle uganda.
Na please don't give me that poor excuse kuwa habyarimana alikuwa hataki, habyarimana hakuwa na shida na watutsi kurudi alikuwa na shida na resources za kuwaweka hao watakaorudi. Hata huyu kagame anavyosema FDLR warudi bila masharti, sio kwamba watarudi kule walikokuwa zamani. Nyumba zao, mashamba yao tayari yameshagawiwa siku nyingi tu, hivyo kurudi kwao sio kama vile kuingia toilet, ni lazima RPF wameweka utaratibu, possibly makambi au sio?
3. waliozaliwa DRC ni wakimbizi wa kihutu ambao wazazi wao walikuwa wakiuawa na kagame na majeshi yake kwa visingizio mbalimbali. Watarudi vipi Rwanda kwa kagame yule yule aliyewafanya wao wawe wakimbizi? Kwani wazazi wao walivyokimbilia DRC walikwenda picnik? walikuwa wanakimbia mauaji ya RPF! Mauaji ambayo yako documented hata kwenye ripoti za UN, angalia hata documentary ya BBC (hata kama hutaki) imeonyesha footage ya kambi ya wakimbizi ilivyokuwa imesambaratishwa na RPF nchini DRC, mass graves, etc, hata mdada anayeongea kwenye ile documentary alikuwa mtoto aliyesalimika kwenye mauaji yale. Hivi yule dada unataka arudi Rwanda bila masharti kweli? Impossible!
4. FDLR haina nguvu za kijeshi we all agree on that. Lakini wana nguvu ya kisiasa. Unaweza kuita siasa zao propaganda na mmeziita hivyo kwa muda mrefu lakini hatimaye ukweli umeanza kujulikana sasa kuwa nani anafanya siasa na nani anafanya propaganda. Hebu tusaidie watu wa JF japo propaganda moja tu "negative" inayoenezwa na FDLR, JUST ONE!, popote pale ambapo FDLR ime-advocate mauaji ya watutsi or something like that, please just one...watanzania tumechoka kuambiwa tunatetea interahamwe bila ushahidi wa hao interahamwe kuwa interahamwe. Nyie mnaodai kuwa hamtaki ukabila ndio wa kwanza kuleta ukabila, unaposema "ni askari wa habyarimana, we fought and defeated them", unajipambanua kuwa wewe ni RPA, a tutsi-rebel group, that included Laurent Nkunda, bosco ntaganda, sultani makenga na magaidi wengine wa kitutsi waliojaa damu za wana-afrika mashariki, huoni haya? wakati huo wewe ulikuwa wapi kama sio Tanzania? kwa tanzania kuitisha mazungumzo kati ya "nyinyi" RPA na serikali ya Habyarimana mbona hakumdai Tanzania inaingilia mambo yenu kama mnavyodai sasa?
hapo kwenye red naona umekuwa touched sana, hahhhhhhhhh!kumbuka it was you, uliyetoa ufafanuzi kuwa FDRL ni mabaki ya askali wa Habyarimana, si ndio?
Sasa ni sili kuwa majeshi ya Habyarimana yalipigwa?...najua inakuuma sana lakini that what happened.
Sasa tumepigana, wakashindwa, wakajaribu kujiorganize tukawapiga tena, then leo ndio wanakuja eti wanataka kuweka masharti ya jinsi ya kurudi?? That`s funny...
Being RPA is not an insult to me, manake jeshi hilo lina credibility kubwa sana barani Africa not only in Rwanda;this can be proved by Darfur residents and Central Africans.