Mambo matatu ya kurekebisha ndani ya CHADEMA

Mambo matatu ya kurekebisha ndani ya CHADEMA

.... Kwani Vipi Mkuu, Hawafai?
Kila siku tunawambia Chadema ina wenyewe angalia sasa umetoa mawazo yako unaitwa Fisi halafu wewe unamuita Mkuu..

teh teh tei
 
Napenda kuwashauri CHADEMA watekeleze mambo matatu yafuatayo ili kuondoa propaganda chafu zinazosambazwa na CCM na ambazo zinaweza kuwa na athari mbaya kwa chama chetu.

Wana-CHADEMA,tunapaswa kutambua kuwa watu tunatofautiana katika uelewa wa mambo na katika mapokeo ya taarifa tunazoletewa au kuzisoma.

Kwa maana hiyo basi,mambo haya nashauri yatazamwe upya.
1.Ukomo wa kugombe uongozi urudishwe katika katiba ya chama na ikiwezekano ukomo uwe ni vipindi vitatu vya miaka mitano mitano.

2.Wanachama waruhusiwe kwenda mahakamni na mtu akishindwa kesi aruhusiwe kuendelea na uanachama wake.

3.Mh.Mbowe,kipindi chako cha sasa kikiisha,nakushauri usigombee tena na utoe fursa kwa wengine kugombea na wewe kama kiongozi, ujikite katika kuhakikisha chama kinapata mrithi bora,wa kuamimika na mwenye viwango.

Mchango ndani wako ndani ya chama ni mkubwa na wa kuthaminiwa sana ila ni vizuri sasa ukatoa nafasi kwa wengine ili kukinusuru chama na propaganda hizi.

4.Japo hatuchagu kiongozi kwa kuangalia kabila lake, lakini ikiwezekana katika uchaguzi wa mwenyekiti ajae jambo hili likaangaliwa kwa mapana na marefu yake.

Wenye akili na upeo wa kuona mbali watanielewa, ila wenye kukariri kuwa chama hakihitaji ushauri wa aina hii, watakuja hapa na vijembe na kejeli.

Niwaambie tu,hata kiburi na kujiamini kwa Zitto msingi wake ni uwepo wa hizi propaganda na ndio maana hata anapata public sympathy kutoka kwa baadhi ya watu na watu hao ni wengi tu huku mitaani tunakoishi.Fanya utafiti mdogo uone.

Propaganda zingine ni za msimu tu lakini sio hizi nilizoziongelea hapa.

Yangu ni hayo tu.

Mkuu,aina ya siasa za maji taka muda umepita
 
Last edited by a moderator:
Hakika mtoa mada utajuta kuwafahamu Bavicha!
 
Naomba kuuliza. Ni chama gani cha siasa kimewahi kushtakiana mahakamani kuhusu migogoro ya ndani. Nikijibiwa hili 🙄🙄🙄
NCCR Mageuzi, TLP, CUF. labda ulikuwa bado ujaanza kufuatilia siasa.
 
Kila siku tunawambia Chadema ina wenyewe angalia sasa umetoa mawazo yako unaitwa Fisi halafu wewe unamuita Mkuu..

teh teh tei

Kweli kinawe wenyewe ambao siyo viungaunga wa ccm

Chadema Kwanza
 
Mkuu salary slip,

Naungana nawe ktk hoja zako uko sahihi asilimia mia, ila napingana nawe namna ya uwasilishaji wa hoja zako!! CDM inao utaratibu wake MZURI wa namna ya kuwasilisha maoni na eneo husika, HAPA SIO MAHALI SAHIHI PA KUWASILISHA HOJA ZAKO!!

Salary Slip, nina uhakika uelewa wako ni mkubwa, utatafakari na kunielewa katikati ya mistari. Kwa ufupi hapa unatafta kejeri na vijembe visivyo na msingi!! Otherwise uniambie unayafanyia checkup mawazo yako ili ukayawasilishe!!

Mjadara mwema wakuu.
Ndugu,mimi ni raia wa kawaid tu na sina nafasi yoyote katika chama zaidi ya kuwa mpenzi/mshabiki wa chama hiki na ambae nimechoshwa na udhalimu wa muda mrefu wa CCM.

Ninatamani sana kuona mabadiliko na hicho ndio kinanisukumu kusema yote haya kwa lengo la kujenga na si kuharibu na mahala palipo rahisi kuyasema haya ni kupitia mitandao JF ikiwa ni mojawapo.

Katika yote niliyoyasema,hakuna kipya hapo ni mambo ambayo yanasemwa kila siku isipokuwa tu husemwa na wapinzani wetu.

Matatizo mengine tunajitakia wenyewe tu kwa kutoshauriana vizuri.
 
Inaonesha mmegundua makosa yenu....kali kuliko yote ni chama cha kidemokrasia kukataza kesi kupelekwa mahakamani.nawaza chadema wakipewa dola watafanya kazi vipi na mahakama? Ndipo mambo ya kunyongana na kutupana kwenye makorongo kwa maagizo ya kamati kuu yatakapo anza

Hataaariiii sana hii kitu.
 
Ndugu,mimi ni raia wa kawaid tu na sina nafasi yoyote katika chama zaidi ya kuwa mpenzi/mshabiki wa chama hiki na ambae nimechoshwa na udhalimu wa muda mrefu wa CCM.

Ninatamani sana kuona mabadiliko na hicho ndio kinanisukumu kusema yote haya kwa lengo la kujenga na si kuharibu na mahala palipo rahisi kuyasema haya ni kupitia mitandao JF ikiwa ni mojawapo.

Katika yote niliyoyasema,hakuna kipya hapo ni mambo ambayo yanasemwa kila siku isipokuwa tu husemwa na wapinzani wetu.

Matatizo mengine tunajitakia wenyewe tu kwa kutoshauriana vizuri.
Popote Nchini tanzania kuna wakala au office ya chama hata unge google ungepata mawasiliano ya chama Hata ungetu pm tungekupa utaratibu wakuwasilisha Mawazo yako yangepokelewa na muhusika

Chadema Kwanza
 
Mbowe kuwa makini na tundu lissu anakimaliza chama kaanza na kitilya ' mwigamba ' zitto na sasa kahamia kwa halima mdee isije kuwa lissu katumwa kuwavuruga halafu anawaiya wenzake wasaliti
 
Mbona salary slip kaliweka vizuri jambo hili, hajasema katiba ivunjwe. Amesema iangaliwe ili kuondoa huo unaoonekana ni ukakasi.

Hivi kusema kuwe na ukomo wa uongozi hasa uenyekiti ni dhambi? Kusema mtu aruhusiwe kwenda mahakamani kutafuta haki na hata akishindwa arudishwe kwa kuwa haki itakuwa imetendeka, basi hilo ni dhambi?

Kwamba makabila mengine nayo yapewe nafasi ndani ya chama, ni dhambi?
Hayo uliyoyasema mkuu wangu ndani ya Chadema hayawezekani.
 
Mbowe kuwa makini na tundu lissu anakimaliza chama kaanza na kitilya ' mwigamba ' zitto na sasa kahamia kwa halima mdee isije kuwa lissu katumwa kuwavuruga halafu anawaiya wenzake wasaliti

Kila chama kina mipango yake hatutapokea mawazo yanayoshabiana na ubongo wa fisi

Chadema Kwanza
 
Umejiuliza ni watanzania wangapi wenye uelewa kama wako?

Ni wangapi wenye uwezo wa kuchambua pumba na mchele?

Mtu asie na uwezo wa ku-reason akitajiwa alianza Mtei akafuaya Bob Makani na sasa Mbowe wote wakiwa ni wachaga ni rahisi sana kuamini hizo propaganda.

Tusiotoe mwanya wa watu kutengeneza propaganda.
Hapo kwenye red mkuu ulikuwa unamaanisha nini? Bob naye alikuwa Mchagga? Ila kwa propaganda za ccm inawezekana kusemwa hivyo na watu wakaamini? Hasa hasa hizi propaganda huwa zinaenezwa kwa watu wasiokuwa na elimu (ambao ndo mtaji wa maccm).
 
Hapo kwenye red mkuu ulikuwa unamaanisha nini? Bob naye alikuwa Mchagga? Ila kwa propaganda za ccm inawezekana kusemwa hivyo na watu wakaamini? Hasa hasa hizi propaganda huwa zinaenezwa kwa watu wasiokuwa na elimu (ambao ndo mtaji wa maccm).
Asante sana kamanda
 
Back
Top Bottom