Mambo 4 ya kufanya mwanamke akupende

Mambo 4 ya kufanya mwanamke akupende

Kuna wanawake wanaume zao wa ndoa wanahela nyingi lakini hawana amani, mwanaume mwingine Malaya mbwa (money source of Evil)!
Mungu azidi kutunusuru na mabaya!
Bora kuwa na kiasi !
Kipindi flani hivi wakati bado nasoma nilikuwaga naishi karibu na kota za polisi kwenye geto la mchizi wangu ambae nilikuwa namuita bro! Huyo bro alikuwa ni dereva tax tena day worker tu.

Alitokea kuzoeana sana na mother mmoja hivi ambae alikuwa ameolewa na inspector wa polisi, kutokana na mazoea yao yaliyokuwa yanatia shaka nilimuuliza bro kama wana uhusiano wowote, ila yeye alinificha akakataa kuniambia ukweli akiofia kwamba mimi ni dogo sina siri nitaenda kumtangaza kwa watu.

Nikashangaa siku moja akapotea ghafla na ikapita wiki nzima aonekani geto bila taarifa yoyote, ikabidi niende kijiweni kwake kumuulizia kwa madereva tax wenzie. Kumbe bana yule bro alikuwa anatafutwa na polisi tena kwa kesi ya uvamizi wa kutumia siraha, kwa baadae nikaja kupata stori kamili kumbe bro alikuwa ana tembea na yule mke wa inspector na inspector aliamua kumsakizia kesi ya ujambazi baada ya kubaini anatembea na mke wake.

Nikikumbuka tulivyokuwa tunaishi huyo bro wangu alikuwa ni mpuuzi tu fulani hana hela lakini alikuwa ana mvua chupi mke wa inspector. Sasa nikionaga comments za watu humu eti mwanamke anatulizwa na pesa huwa naishia kucheka tu na kusikitika.
 
Kuna wanawake wanaume zao wa ndoa wanahela nyingi lakini hawana amani, mwanaume mwingine Malaya mbwa (money source of Evil)!
Mungu azidi kutunusuru na mabaya!
Bora kuwa na kiasi !
Pesa ni nyongeza tu ya mapenzi kwakweli kuna watu wana kila kitu lakini hakuna amani wala upendo kimebakia ni uvumilivu tu, mnaweza kuwa mnapendana ngoja kipato kiongezeke ndiyo wanawake warembo wanaonekana
 
Mwanaume ajue kujiongeza ajue kujitoa, akuheshim, akupende, akuthamini, akujali, akupe muda wake (itaingia hukohuko kwenye kujali)ajue kuvumilia awe na upeo mkubwa wa kufikiri nadhani huyu kwangu ana kila sababu ya kumpenda
Ninavyo vyote, shida yangu nimoja, nataka kua mfalme suleiman.
 
Mwanaume ajue kujiongeza ajue kujitoa, akuheshim, akupende, akuthamini, akujali, akupe muda wake (itaingia hukohuko kwenye kujali)ajue kuvumilia awe na upeo mkubwa wa kufikiri nadhani huyu kwangu ana kila sababu ya kumpenda
Ahsante madam!
 
Mwanaume ajue kujiongeza ajue kujitoa, akuheshim, akupende, akuthamini, akujali, akupe muda wake (itaingia hukohuko kwenye kujali)ajue kuvumilia awe na upeo mkubwa wa kufikiri nadhani huyu kwangu ana kila sababu ya kumpenda
Dada yaan vyote ivi mnataka nyinyi tu kwel??
Ina maan mwanaume hastahil ivi vitu?

Ndo maan furaha yangu haitegemei mtu
 
3&4 nimezishika patamu. Ila 1&2 zimenishika pabaya
 
Habari Wana wa JF.Natumai muko sawa,

Leo nashukuru Mungu kuchukua fursa hii kwa mara nyengine tena kuwaelezea kile ninachokifahamu katika maisha.Nimekuja na mambo manne ukiwa nayo mwanamke atakupenda na utamfanya mkeo awe na furaha.

1.KUWA NA HESHIMA.
Heshima inasababisha mwanamke kukupenda kwasababu utapokuwa na heshima una-epukana na dhararu na wanawake karibuni wote hawapendi kudharauliwa.Heshima ni miongoni mwa kumsikiliza mtu,kutoongea nae kwa maneno machafu,kutompiga pasi na sababu,kutofanya vitu ambavyo yeye havipendi,kuonesha unajali kwake n.k.

2.KUDHIHIRISHA UPENDO
Unapoishi onesha kwamba una upendo na kila mtu,kwasababu mwanamke anahitaji amani na maelewano.Unapokuwa na sura pamoja na moyo wa upendo kila mtu anavutika nawe na anakupenda sio mwanamke tu peke yake, na wala watu hawatokuchoka.

3.KUWA MWEREVU
Hutakiwi kuwa mjinga mbele ya jamii.Unatakiwa kuishi ki-professional.Kwa sababu mwanamke anajivunia sana anapokuwa na mwanamume mwenye busara,anahisi ni wato-fauti.Jaribu kuwa mkimya usiwe unaongea ovyo,kuwa mtaratibu na usiwe unakimbilia kutoa hukumu kabla ya kufikiri.
Fikiria kwanza,Ongea maneno madhubuti. Mimi binafsi, kwenye miaka kama 5 iliyopita kuna mtu alikuwa anapenda sana kuniambia maneno haya "I like the way you are".

4.KUWA NA UVUMILIVU
Wanawake ni watu wenye vituko sana.Na muda mwengine huwa ni kama tabia kwao wanapokuwa wanaumwa ama wana stress zao tu ki-kawaida.Sasa unatakiwa ufahamu kwamba wewe ni mwanamume unatakiwa kuvumilia na hivyo vituko na maudhi yote hayo.Unatakiwa kuwa mkimya na uweze kudhibiti hasira zako.Mwachie mtu mpaka ajitambue mwenyewe kama ana makosa.

Kujifunza tabia hizi utakuwa umeuteka moyo wa mwanamke


TUMUELEKEENI MUNGU, WANAWAKE WENGI TULIIOA NI WACHAWI, NYIE HANGAIKENI KUWAFURAHISHA TU BADALA YA KURUDIA MAKUSUDI YA MUNGU KWENYE MAISHA YENU.
 
Smart people are not looking for the money but they look on how they'll manage their time, because it is only time create money.
If you are looking for money, you will be end up nothing.
 
Mwanaume ajue kujiongeza ajue kujitoa, akuheshim, akupende, akuthamini, akujali, akupe muda wake (itaingia hukohuko kwenye kujali)ajue kuvumilia awe na upeo mkubwa wa kufikiri nadhani huyu kwangu ana kila sababu ya kumpenda
Ninavyo vyote hivyo bibie nipende bas
 
kama huna pesa hayo yoye ni kama feni ya solar,,,,,,mvua ikinyesha wiki nzima, haiwaki.....tafuta money brother wacha story
 
Back
Top Bottom