Mama yangu ni Bonge la mpambanaji

Mama yangu ni Bonge la mpambanaji

Acha tu niseme bi mkubwa wangu ni bonge la fighter. Licha ya kazi anayofanya kua na maslahi madogo lakini mambo anayoyafanya ni makubwa. Mama yangu ni mwalimu wa shule ya msingi ila mungu kamjalia akili ya MAISHA..

Maisha ya walimu wa S/M wengi mnayajua ni mwendo wa madeni tu mwanzo mwisho Deni linaisha uku linakuja uku. Mpka muda mwingine unataman kuacha kazi. Kuna kipind mama alishawai kunitamkia ivo nikiwa form 2. Nikamwambia pambana. Lakini kwa msoto wote uo bado bi mkubwa. Kasimama.. Anawasaidia sana ndugu zake, anatusomesha sisi wanae mpka ndugu zake, anawahudumia wazazi wake kadri awezavyo.

Kwenye family tupo wa 3.. Mimi kama first born na wenzangu wa 2 (wote wa kike).. Kingine ninachoshukulu kwa bi mkubwa ametupanga vizuli, Imagine mimi kama mtoto wa kwanza nipo chuo kikuu kimoja cha AFYA hapa nchini nimebakiza semester moja nimalize tunaisubil COVID-19. ila anaenifatia yupo form 3.. Na anaefata Ndio ameanza darasa la kwanza mwaka huu ( 2020). Naisi hii imempa muda mzuri

Kama first born najitahid ku play part yangu vizuri sana ikiwemo kujenga uaminifu. Mkubwa sana kuna kipindi nikiwa likizo alinipa pesa nisimamie ujenzi wa nyumba.. Basi mjengo unaanza mpka unakamilika sijaichukua hata. TSh.100. Expenditure zote nilizofanya nilikua nazinote kwenye notebook. Baada ya ujenzi kuisha nikamkabidhi zile kalatasi nikamwambia matumizi Ndio kama hayo na pesa full ulizonikabidhi zilikua hizi na zilizobaki hizi.. Daah kiukwel hakuamini naisi alidhani pesa yote ingeisha.. Akamega kias. flan cha pesa akanipa.. Guys hakuna jambo zuli kwenye kazi za watu kama UAMINIFU.. Ukiwekwa sehemu acha Tamaa.. Toka siku hiyo hakuna password yake nisiyoijua kuanzia BANK mpka miamala ya kwnye simu.. Kila jambo la maendeleo analotaka kufanya lazima anishilikishe.

Honestly bi mkubwa ni mtu wa kubana sana SAVING zinamtoa sana na miradi yake mengine.. Kuna siku aliniambia mwanangu ukianza kujitegemea jalibu kuweka walau 10% ya Pato lako kwa mwezi.... Kulingana na kipato chako.. Akanimbia usiwe mtu wa kumaliza elfu 20 Au 15 kwa siku kwnye kula tu.. Hahaha mwenyewe ana msemo wake anasemaga "TUMBO HALINA SHUKRAN" ila siku moja moja sio mbaya Una enjoy vitu vizul.. Daaaah Mungu niwekee mama yangu Nami nije kumlea... Inshaallah

Mungu awape nguvu wakina mama + wakinadada wapambanaji wote na kuendeleza hizi race.. Uwe umeajiliwa, umejiajili, Au umeajiliwa + kujiajili) mwenyezimungu awazidishie..

Kama hii thread imekuja sehemu sio mniwie radhi wakuu maana hili Ndio jukwaa langu pendwa Humu JF . na linalotembelewa na watu wengi.. Finally tujikinge na COVID-19..

Nawasilisha
From Caglar SOYUNCU
I miss my Mother...R.I
P Queen.
She was a fighter too!

Sent from my SM-A507FN using JamiiForums mobile app
 
Mama yangu sio fighter lakini ni responsible na wa uhakika. Anafaa kuwa subordinate wa mtu na anaperform vizuri kabisa kazini wakati ana elimu si kubwa sana ya kutisha.
Nishaona hana uwezo mzuri wa kusimamia shughuli zake, labda kwakuwa experience hana.

Anatulea peke yake, mzee yuko bize na maisha yake na hataki 'mazoea' kabisa.
Hatuna pesa wala mali za aina yoyote. Tumebarikiwa amani na afya.
Bahati nzuri sisi hatusumbui wala hatuna historia ya utukutu, sio wakorofi wala wasumbufu. Mama haugui kabisa, mara ya mwisho kuumwa serious hatujui ni ugonjwa gani. Alipofukuzwa tu kazi kwa utoro ugonjwa ukaisha.

Naweza jitegemea kwa mambo mengine lakini si kwa ada. Niko chuo, dogo yuko form four.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Poa poa kaza.. Kaza uko ulipo
Mama yangu sio fighter lakini ni responsible na wa uhakika. Anafaa kuwa subordinate wa mtu na anaperform vizuri kabisa kazini wakati ana elimu si kubwa sana ya kutisha.
Nishaona hana uwezo mzuri wa kusimamia shughuli zake, labda kwakuwa experience hana.

Anatulea peke yake, mzee yuko bize na maisha yake na hataki 'mazoea' kabisa.
Hatuna pesa wala mali za aina yoyote. Tumebarikiwa amani na afya.
Bahati nzuri sisi hatusumbui wala hatuna historia ya utukutu, sio wakorofi wala wasumbufu. Mama haugui kabisa, mara ya mwisho kuumwa serious hatujui ni ugonjwa gani. Alipofukuzwa tu kazi kwa utoro ugonjwa ukaisha.

Naweza jitegemea kwa mambo mengine lakini si kwa ada. Niko chuo, dogo yuko form four.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunashare story mkuu

More life to all mothers

#Stayhome safe COVID-19 is everywhere
 
Back
Top Bottom