Mama yangu adui yangu

Mama yangu adui yangu

Mama Yangu Adui Yangu - 47-


ILIPOISHIA:
“Nina imani hivi karibuni mmeona mabadiliko ya hali ya mama yenu?”
“Ni kweli,” tulijibu kwa pamoja.
“Nina imani hali hii imewashtua sana na kukosa jibu, ni kweli?”
“Kweli,” dada alijibu.
“Nina imani mi si msemaji ila mzungumzaji mkubwa ni mama yenu ataelezea kinachomtesa moyoni mwake.”
“Hakuna tatizo,” dada mkubwa alijibu.
“Kabla sijamkaribisha mama yenu naomba kuwauliza.”
“Uliza tu,” tulimkubalia.
“Je, mnampenda mama yenu?”
“Zaidi ya sana.”
“Kama amewakosea mpo tayari kumsamehe?”
“Leo mpaka kesho kiama,” tulijibu wote kwa vile tulikuwa tukimpenda mama yetu.
SASA ENDELEA...


“Haya mama Zamda hebu toa dukuduku lako wanao wamesema wamekusamehe leo na kesho kiama.”
Wote tulihamishia macho yetu kwa mama aliyekuwa ameweka mkono shavuni. Mama alitoa mkono shavuni na kufuta machozi kwa mtandio kisha alikohoa kidogo na kupenga makamasi na kujifuta kwa kitambaa kidogo cha mkononi kisha alisema kwa sauti ya kujilazimisha:
“Nikuwa na mtihani mzito baada ya kugundua nilichokifanya si sahihi hasa kwa mzazi kama mimi. Lakini nimekuwa na wakati mgumu kuyasema haya kwenu.
“Kwangu ni sawa na kutembea bila ya nguo mbele ya kadamnasi, lakini sina jinsi lazima niseme. Namuomba Mungu anipe nguvu ya kuweza kuyasema haya.
“Nina imani huenda wanangu mnasema mtanisamehe mama yenu kwa vile hamjui kipi kibaya nimewafanyia ambacho kinaweza kuwafanya mkanichukia na kutaka hata tusizikane kitu ambacho nina imani kitaniweka katika wakati mgumu sana hata kusababisha nife kwa kihoro.”
“Mama kwa lolote baya hata kama ulitaka kutuua mimi nakutoa wasiwasi, kwa upande wangu nilichosema sitabadili kauli yangu. Kama nitafanya hivyo basi Mungu anifufue nguruwe siku ya kiama.”
Nilijikuta nikisema kwa uchungu mpaka machozi yakanitoka huku moyo ukiniuma. Niliamini mama yetu alikuwa na mzigo mkubwa moyoni mwake kuyaanika mabaya yake kwa kinywa chake.
Niliamini kuyasema yale ilikuwa njia ya kumpa nafuu mama kwa kile alichotaka kukitoa mbele yetu. Dada zangu nao waliungana nami kumhakikishia mama hakuna atakaye badili kauli ya kumsamehe.
Baada ya kauli yangu mama alishusha pumzi ndefu na kusema:
“Kwanza napenda kumshukuru Mungu kunipa watoto wenye mapenzi makubwa kwangu japokuwa mama yenu nilikosa mapenzi ya dhati kwenu japo niliamini nawapenda sana lakini mapenzi yangu kwenu yaligeuka sumu.”
“Pia namshukuru mama Amina Mungu amzidishie, kwa umri namzidi sana lakini amekuwa mwanamke shupavu mwenye moyo wa kipekee kuipigania familia yangu, Mungu atakulipa.”
“Amina,” aliitikia mama Amina.
Mama alianza kumwaga siri zake kwa kujilazimisha kama mtu aliyekuwa akinyweshwa shubiri. Kuanzia siri nzito ambayo hatukuijua ya kifo cha baba kuwa yeye ndiye alichangia.
“Wanangu kifo cha baba yenu naweza kusema mimi ndiye chanzo. Kilitokana na mateso mazito yaliyofanya mimi mama yenu niingie kwenye mchezo mbaya.
“Baba yenu aliondoka nyumbani nikiwa na ujauzito wa miezi miwili wa Mwaija na kuhamia kwa mwanamke wa nje.
“Mwanzo sikushtuka kwa vile mahitaji yote ya muhimu nilikuwa nayo nilijua atarudi. Lakini adha ya mateso ilianza baada ya kuishiwa kila kitu ndani. Kwa kweli niliteseka kufikia hatua ya kushinda na njaa mimi na ninyi wanangu, kibaya nilikuwa mjamzito.
“Yeye baba yenu alikuwa ameshikwa na mwanamke wa nje ambaye alimfanyia madawa na kumfanya aisahau familia yake.
“Kila kukicha hali ilizidi kuwa mbaya nikawa napita kwa majirani kuwaombea chakula. Kuomba kila siku nilishindwa na kuamua siku nyingine kuwakorogea uji bila sukari.
“Maisha yangu yalikuwa magumu sana kwani kuna wakati nililazimika kushinda na njaa, nikawa mtu wa kuwaza tu. Nilikuwa nakonda kila siku na kushinda nalia kutokana na mateso mliyokuwa mkiyapata wanangu.
“Kuna siku mlishindwa kunyanyuka kitandani kutokana na njaa, Nilijikuta naingia nyumba ya jirani na kuiba unga. Nilishindwa na kuwa aibu mtaani.
“Nilijikuta nikipata mawazo mengi kufikia kuwaza kunywa sumu, lakini moyo ulinisuta kufanya hivyo kwa vile ningetoa uhai wa kiumbe kisicho na hatia pia kuwaacha wanangu kwenye mateso mazito.
“Siku moja nilipata wazo baada ya kumuona mwanamke mmoja akiuza mboga za majani huku akiwa na tumbo kubwa. Sikusita kumuuliza na kunieleza ana watoto wanne, mumewe alimkimbia na kuamua kufanya biashara ile ambayo ilimsaidia kupunguza ukali wa maisha.
“Wazo lile nililiafiki na kumuomba msaada wa mimi kupata zile mboga. Alinielekeza jinsi ya kuzipata nami nikaingia kwenye biashara hiyo.
“Mwanzo niliona aibu, lakini aibu ilinitoka baada ya kumaliza mapema na kununua mahitaji muhimu ya siku ile japo hayakulingana na aliyokuwa akinipa baba yenu.
“Siku za kujifungua nazo zilikaribia nikawa nachoka sana. Ilibidi nipumzike na biashara ile kutokana kuelemewa na tumbo.
Ugumu wa maisha ulianza kujirudia, lakini nilipata bahati kuna dada mmoja alihamia jirani ambaye kwa kweli tulikuwa tumezoeana. “Nilipomueleza matatizo yangu hakutaka kuniacha alinisaidia mahitaji madogomadogo. Namshukuru Mungu nilijifungua salama mtoto mwenye afya njema.
“Kwa vile tulikuwa na vitu ndani, alinishauri niuze baadhi ili nipate fedha ya kujikimu na maisha.
“Nilifanya vile kwa kuuza kabati kubwa la nguo, tivii na deki kwa bei ya kutupa. Baada ya kufanikiwa zoezi lile alinishauri nihangaike kwa vile baba yenu aliikimbia familia yake, lazima kutakuwa na mkono wa mtu. Bila hivyo nitaiua familia yangu.
“Siwezi kumlaumu kwa kunipa wazo la kumuhangaikia baba yenu. Baada ya kuyafanyia kazi mawazo yake ambayo baadaye yalikuwa majuto ya milele.
“ Alinipeleka kwa mtaalamu mmoja ambaye alinieleza kila kitu juu ya baba yenu kushikwa kishirikina na mwanamke wa nje.
“Aliniahidi kunisaidia basi alinipatia tiba ya kusafisha mwili wangu na dawa nyingine.
Niliamini uchawi upo na dawa zipo kwani baada ya kutumia zile dawa kwa wiki moja baba yenu alirudi na kuonekana kama mtu ambaye hakuelewa alikuwa wapi.
“Kwa vile nilikuwa nimepewa dawa ya kumtuliza, nilimwekea kwenye chakula na kwenye maji na kuchukua nguo alizorudi nazo na kuzipeleka kwa mtaalamu ambapo alizifanyia dawa.
“Baada hapo baba yenu alitulia nyumbani na hali ya maisha ilirudi kama zamani kwa kurudisha vitu vyote nilivyoviuza. Pia alinionesha na nyumba aliyokuwa akiijenga ambayo baadaye aliiandika jina la Mwaija kama zawadi ya kuzaliwa kwake bila ya wewe kuwepo.
“Niliendelea kutumia dawa nilizopewa. Kila nilipokwenda kwa mtaalamu alinieleza vita iliyokuwa nje ni kubwa kwa yule mwanamke aliyetaka kumchukua tena baba yenu.
Lakini mganga alinihakikishia hawezi kufanya kitu. Nilimshukuru shoga yangu kuweza kuiokoa familia.
“Wakati nikiamini mambo yametulia kumbe yule mwanamke alikuwa halali kwa ajili ya baba yenu, alizunguka pande zote za dunia. Mwaija alipofikisha miaka miwili mambo yalibadilika.
“Ya mwanzo ilikuwa cha mtoto, kwanza tulianza kukosana ndani, jambo si jambo linakuwa ugomvi mkubwa. Nilirudi haraka kwa mtaalamu na kunipatia dawa. Lakini ndiyo kwanza zikamfukuza ndani baba yenu.
“Baba yenu alitoweka sikujua yule mwanamke kamficha wapi. Nilihangaika kutumia dawa za yule mtaalamu bila mafanikio. Taratibu maisha yakaanza kuwa magumu tena.
“Niliapa kuuza hata nguo ya ndani ili kumshikisha adabu yule mwanamke. Nilikwenda kwa kila mganga niliyeelezwa, niliuza vito vyangu vyote ili kuhakikisha namrudisha baba yenu, lakini sikufanikiwa na kujikuta nimeuza nguo zangu zote za maana ili kuhakikisha naendelea kumuhangaikia baba yenu.

Itaendelea Jumapili ijayo....
 
ILIPOISHIA:
“Wakati nikiamini mambo yametulia kumbe yule mwanamke alikuwa halali kwa ajili ya baba yenu, alizunguka pande zote za dunia. Mwaija alipofikisha miaka miaka miwili mambo yalibadilika.
“Ya mwanzo ilikuwa cha mtoto, kwanza tulianza kukosana ndani, jambo si jambo linakuwa ugomvi mkubwa. Nilirudi haraka kwa mtaalamu na kunipatia dawa. Lakini ndiyo kwanza zikamfukuza ndani baba yenu.
“Baba yenu alitoweka sikujua yule mwanamke kamficha wapi. Nilihangaika kutumia dawa za yule mtaalamu bila mafanikio. Taratibu maisha yakaanza kuwa magumu tena.
“Niliapa kuuza hata nguo ya ndani ili kumshikisha adabu yule mwanamke. Nilihangaika kwa kila mganga niliyeelezwa, niliuza vito vyangu vyote ili kuhakikisha namrudisha baba yenu, lakini nilidunda na kujikuta nimeuza nguo zangu zote za maana ili kuhakikisha naendelea kumhangaikia baba yenu.
SASA ENDELEA...

“Hamuwezi kuamini wanangu kipindi cha kuhangaika kwangu sikujua malezi yenu. Nilikonda nilikuwa sijijali, kuoga na kubadili nguo hakikuwa kitu muhimu kwangu kwa wakati ule kwa ajili ya kumhangaikia baba yenu.
“Mpaka nakufa yule mwanamke siwezi kumsahau.
Kuna mtu alinieleza kuna sehemu nikienda baba yenu atarudi na asingetoka tena. Kwa vile kulikuwa mbali, niliwachukua na kuwapeleka kijijini kwa mama na mimi kuondoka kwenda kuhangaika.
“Nilikwenda mpaka Ufipa ambako nilikaa zaidi ya miezi mitatu na kubahatika kumpata mganga ambaye alinihakikishia baba yenu atarudi na hataondoka tena kwenda kwa yule mwanamke na kama angerudi basi ningekwenda kuchoma mikoba yake.
“Pia alinihakikishia kama yule mwanamke atatia tena mkono basi atabakia jina.
“Baada ya kupata tiba nilirudi nyumbani na dawa kibao, za kuoga, kunywa, kuchoma na kuchanganya kwenye chakula. Niliandikiwa dawa zote na matumizi yake.
“Baada ya kupewa dawa nilirudi nyumbani nikiwa hoi. Nilikonda mama yenu na kusawajika kwa ajili ya kuhangaika kumrudisha mume wangu nyumbani.
“Nilifika nyumbani majira ya saa moja usiku, siku ileile sikutaka kulala. Nilichukua dawa zangu, nilianza kwa kuoga dawa na nyingine kumwagia kila kona ya nyumba kuondoa uchawi. Kisha nilianza kufanya kama nilivyoelekezwa jinsi ya kumvuta baba yenu.
“Kwa vile nilikuwa nimefika jioni sana, usiku ulipofika nilichoma dawa huku nikimwita baba yenu kwa jina arudi nyumbani. Nilifanya vile bila kupumzika kama nilivyoelezwa mpaka nitakaposikia hodi.
“Narudia tena kusema uchawi upo na dawa zipo. Nikiwa katikati ya zoezi ambalo lilikuwa linachukua zaidi ya saa moja na nusu. Nilisikia mlango ukigongwa, niliacha kunuiza na kwenda kufungua mlango.
“ Sikujua nani anayegonga, nilipofungua mlango kidogo nianguke kwa mshtuko baada ya kumuona baba yenu mbele yangu.”
Kauli ya mama ilifanya mwili wangu usisimke, nilimuangalia mama aliyekuwa akizungumza taratibu huku akifuta machozi, moyo uliendelea kunifukuta.
“Nilimuona baba yenu kama msukule aliyerudishwa baada ya kuchukuliwa kichawi. Alikuwa kama mtu asiyejifahamu. Kama mmeshawahi kuona mtu akirudishwa baada ya kuchukuliwa kichawi ndivyo baba yenu alivyokuwa.
“Ile hali nilielezwa na mganga itajitokeza lakini alinieleza nimshtue kwa kumpiga na maji ya dawa usoni kisha nimuoshe kwa dawa aliyonipa na nyingine nimpe anywe, siku ya pili angeamka akiwa mzima kabisa.
“Baada ya baba yenu kuingia ndani moyo uliniuma sana kutokana na hali aliyokuwa nayo. Kumbe alikuwa yupo na yule mwanamke na aligeuzwa msukule kwa kufanyishwa mambo bila kujua.
“Nilifanya kama nilivyoelekezwa, nikampiga usoni na maji ya dawa ili kumzindua kwenye kifungo cha kichawi. Baada ya kuchanganya dawa kwenye maji nilimpiga nayo usoni na kumfanya ashtuke kama anatoka usingizini.
“Cha kwanza kilikuwa kuwauliza wanawe, nilimueleza mmekwenda kumtembelea bibi yenu kijijini. Alijinyoosha kama mtu aliyekuwa amechoka sana na kupiga miayo.
Nilimpelekea maji bafuni yaliyochanganywa na dawa. Baada ya kuoga nilimpa dawa ya kunywa na kumuacha alale.
“ Mmh! Yaani baba yenu alipolala ha..ha..ku..amka tena.”
Mama alianza kulia kwa kwikwi, kitu kilichofanya wote tulie kilio cha kimya kwa kutokwa machozi huku nikizidi kumuonea huruma mama yetu.
Ilibidi mama Amina aanze kazi ya kumbembeleza mama aliyekuwa akilia kilio cha kwikwi. Nilipowaangalia dada zangu kila mmoja alikuwa akilia.
Kwa kweli ilikuwa simulizi yenye kuumiza na kuupasua moyo bila ganzi. Baada ya mama kunyamaza aliendelea kuzungumza kwa sauti ya kilio na kuzidi kuniumiza.
“Kwa kweli sikuelewa sababu ya kifo cha baba yenu, nilijiuliza labda dawa niliyompa kunywa ndiyo iliyochangia kifo cha baba yenu na kama ni ile nilikosea sehemu nini? Niliumia mara mbili baada ya kuhaingaika kote kumbe natafuta kumuua mume wangu.”
Kufikia hapo tena mama akaanza kulia tena.
Nilishindwa kujizuia nilijikuta nikisema kwa sauti bila kujielewa:
“Mama hujamuua baba, ulifanya kwa ajili yetu lakini bahati mbaya ikatokea iliyotokea.”
“Hapana wanangu bila mimi msingekuwa yatima.”

Itaendelea katika Risasi Jumatano...
 
sajosojo

si ufungue uzi wako, acha kutuaribia utamu anaotuletea MziziMkavu

au unadhani hatujui kuwa tunaweza soma kwingine?????????????????

acha kupost hii, story muwege na heshima wakati mwingine unaboa sana. wewe unadhani uondo asingeuanzisha humu tungejua story hii, nenda katafute ingine ya kuja kuweka.
 
[h=1]Mama Yangu Adui Yangu - 48-[/h]ILIPOISHIA:
"Wakati nikiamini mambo yametulia kumbe yule mwanamke alikuwa halali kwa ajili ya baba yenu, alizunguka pande zote za dunia. Mwaija alipofikisha miaka miaka miwili mambo yalibadilika.
"Ya mwanzo ilikuwa cha mtoto, kwanza tulianza kukosana ndani, jambo si jambo linakuwa ugomvi mkubwa. Nilirudi haraka kwa mtaalamu na kunipatia dawa. Lakini ndiyo kwanza zikamfukuza ndani baba yenu.
"Baba yenu alitoweka sikujua yule mwanamke kamficha wapi. Nilihangaika kutumia dawa za yule mtaalamu bila mafanikio. Taratibu maisha yakaanza kuwa magumu tena.
"Niliapa kuuza hata nguo ya ndani ili kumshikisha adabu yule mwanamke. Nilihangaika kwa kila mganga niliyeelezwa, niliuza vito vyangu vyote ili kuhakikisha namrudisha baba yenu, lakini nilidunda na kujikuta nimeuza nguo zangu zote za maana ili kuhakikisha naendelea kumhangaikia baba yenu.
SASA ENDELEA...

"Hamuwezi kuamini wanangu kipindi cha kuhangaika kwangu sikujua malezi yenu. Nilikonda nilikuwa sijijali, kuoga na kubadili nguo hakikuwa kitu muhimu kwangu kwa wakati ule kwa ajili ya kumhangaikia baba yenu.
"Mpaka nakufa yule mwanamke siwezi kumsahau.
Kuna mtu alinieleza kuna sehemu nikienda baba yenu atarudi na asingetoka tena. Kwa vile kulikuwa mbali, niliwachukua na kuwapeleka kijijini kwa mama na mimi kuondoka kwenda kuhangaika.
"Nilikwenda mpaka Ufipa ambako nilikaa zaidi ya miezi mitatu na kubahatika kumpata mganga ambaye alinihakikishia baba yenu atarudi na hataondoka tena kwenda kwa yule mwanamke na kama angerudi basi ningekwenda kuchoma mikoba yake.
"Pia alinihakikishia kama yule mwanamke atatia tena mkono basi atabakia jina.
"Baada ya kupata tiba nilirudi nyumbani na dawa kibao, za kuoga, kunywa, kuchoma na kuchanganya kwenye chakula. Niliandikiwa dawa zote na matumizi yake.
"Baada ya kupewa dawa nilirudi nyumbani nikiwa hoi. Nilikonda mama yenu na kusawajika kwa ajili ya kuhangaika kumrudisha mume wangu nyumbani.
"Nilifika nyumbani majira ya saa moja usiku, siku ileile sikutaka kulala. Nilichukua dawa zangu, nilianza kwa kuoga dawa na nyingine kumwagia kila kona ya nyumba kuondoa uchawi. Kisha nilianza kufanya kama nilivyoelekezwa jinsi ya kumvuta baba yenu.
"Kwa vile nilikuwa nimefika jioni sana, usiku ulipofika nilichoma dawa huku nikimwita baba yenu kwa jina arudi nyumbani. Nilifanya vile bila kupumzika kama nilivyoelezwa mpaka nitakaposikia hodi.
"Narudia tena kusema uchawi upo na dawa zipo. Nikiwa katikati ya zoezi ambalo lilikuwa linachukua zaidi ya saa moja na nusu. Nilisikia mlango ukigongwa, niliacha kunuiza na kwenda kufungua mlango.
" Sikujua nani anayegonga, nilipofungua mlango kidogo nianguke kwa mshtuko baada ya kumuona baba yenu mbele yangu."
Kauli ya mama ilifanya mwili wangu usisimke, nilimuangalia mama aliyekuwa akizungumza taratibu huku akifuta machozi, moyo uliendelea kunifukuta.
"Nilimuona baba yenu kama msukule aliyerudishwa baada ya kuchukuliwa kichawi. Alikuwa kama mtu asiyejifahamu. Kama mmeshawahi kuona mtu akirudishwa baada ya kuchukuliwa kichawi ndivyo baba yenu alivyokuwa.
"Ile hali nilielezwa na mganga itajitokeza lakini alinieleza nimshtue kwa kumpiga na maji ya dawa usoni kisha nimuoshe kwa dawa aliyonipa na nyingine nimpe anywe, siku ya pili angeamka akiwa mzima kabisa.
"Baada ya baba yenu kuingia ndani moyo uliniuma sana kutokana na hali aliyokuwa nayo. Kumbe alikuwa yupo na yule mwanamke na aligeuzwa msukule kwa kufanyishwa mambo bila kujua.
"Nilifanya kama nilivyoelekezwa, nikampiga usoni na maji ya dawa ili kumzindua kwenye kifungo cha kichawi. Baada ya kuchanganya dawa kwenye maji nilimpiga nayo usoni na kumfanya ashtuke kama anatoka usingizini.
"Cha kwanza kilikuwa kuwauliza wanawe, nilimueleza mmekwenda kumtembelea bibi yenu kijijini. Alijinyoosha kama mtu aliyekuwa amechoka sana na kupiga miayo.
Nilimpelekea maji bafuni yaliyochanganywa na dawa. Baada ya kuoga nilimpa dawa ya kunywa na kumuacha alale.
" Mmh! Yaani baba yenu alipolala ha..ha..ku..amka tena."
Mama alianza kulia kwa kwikwi, kitu kilichofanya wote tulie kilio cha kimya kwa kutokwa machozi huku nikizidi kumuonea huruma mama yetu.
Ilibidi mama Amina aanze kazi ya kumbembeleza mama aliyekuwa akilia kilio cha kwikwi. Nilipowaangalia dada zangu kila mmoja alikuwa akilia.
Kwa kweli ilikuwa simulizi yenye kuumiza na kuupasua moyo bila ganzi. Baada ya mama kunyamaza aliendelea kuzungumza kwa sauti ya kilio na kuzidi kuniumiza.
"Kwa kweli sikuelewa sababu ya kifo cha baba yenu, nilijiuliza labda dawa niliyompa kunywa ndiyo iliyochangia kifo cha baba yenu na kama ni ile nilikosea sehemu nini? Niliumia mara mbili baada ya kuhaingaika kote kumbe natafuta kumuua mume wangu."
Kufikia hapo tena mama akaanza kulia tena.
Nilishindwa kujizuia nilijikuta nikisema kwa sauti bila kujielewa:
"Mama hujamuua baba, ulifanya kwa ajili yetu lakini bahati mbaya ikatokea iliyotokea."
"Hapana wanangu bila mimi msingekuwa yatima."


Itaendelea Alhamisi ijayo.....
 
sajosojo

si ufungue uzi wako, acha kutuaribia utamu anaotuletea MziziMkavu

au unadhani hatujui kuwa tunaweza soma kwingine?????????????????

acha kupost hii, story muwege na heshima wakati mwingine unaboa sana. wewe unadhani uondo asingeuanzisha humu tungejua story hii, nenda katafute ingine ya kuja kuweka.
bibie mzurimie Muache huyu.@sajosojo anatafuta umaarufu juu ya mgongo wangu hawezi kuupata kamwe.
 
Last edited by a moderator:
halafu nimegundua story aliyotumja sajosojo haivutii kuisoma kama hadithi, anakopi kwa kukosea!!!!!!
 
Mama Yangu Adui Yangu - 49-


ILIPOISHIA;
"Mmh! Yaani baba yenu alipolala ha..ha...ku...amka tena."
Mama alianza kulia kilio cha kwikwi kitu kilichofanya wote tulie kilio cha kimya kwa kutokwa machozi huku tukizidi kumuonea huruma mama yetu.
Ilibidi mama Amina aanze kazi ya kumbembeleza mama aliyekuwa akilia.
Nilipowaangalia dada zangu kila mmoja alikuwa akilia.
Kwa kweli ilikuwa simulizi yenye kuumiza na kupasua mioyo bila ganzi. Baada ya mama kunyamaza aliendelea kuzungumza kwa sauti ya kilio na kuzidi kuniumiza.
"Kwa kweli sikuelewa sababu ya kifo cha baba yenu, nilijiuliza labda dawa niliyompa kunywa na kama ni ile nilikosea sehemu gani. Niliumia mara mbili baada ya kuhangaika kote kumbe nilitafuta kumuua mume wangu."
Kufikia hapo mama akaanza kulia tena.
Nilishindwa kujizuia nilijikuta nikisema kwa sauti bila kujielewa:
"Mama hujamuua baba, ulifanya kwa ajili yetu lakini bahati mbaya yakatokea yaliyotokea."
"Hapana wanangu bila mimi msingekuwa yatima."
SASA ENDELEA...


"Si kweli, wangapi mayatima si kwa tukio kama lako?" nilihoji.
"Lakini bila mimi baba yenu asingekufa."
"Angekufa kwa kitu kingine, mama toka ulipoanza kuzungumza sijaona sehemu uliyochangia kifo cha baba. Mama tunakuomba uondoe wazo hilo," dada mkubwa alisema.
"Basi wanangu baada ya msiba tulifanya kila kitu na kumlaza baba yenu katika nyumba yake ya milele. Nilikonda kwa mawazo, lakini ninyi ndiyo mlionifanya nisimame imara ili kuhakikisha nawasomesha na hamtetereki kimaisha.
"Sijui niseme nini, lakini baada ya kifo cha baba yenu vitu vingi vilijulikana. Alikuwa na gari na nyumba pia malipo yote ya kazini kwake nilipata.
Baada ya kupata vitu vyote hivyo nilimalizia nyumba ya Mwaija na kuipangisha. Naweza kusema nilifanya kosa kukueleza Mwaija baba yako alikuachia nyumba kubwa.
"Hilo naomba nikiri nilifanya kosa, nimekula fedha yako bila kukushirikisha kwa miaka yote hiyo. Lakini leo nitakukabidhi kila kitu.
"Kupitia mali alizoacha baba yenu niliweza kuwasomesha wote ila sikutaka msome sana kwa vile mngeondoka na kuniacha peke yangu. Hapo ndipo nilipoanza kufanya makosa makubwa.
"Baada ya Zamda na Rehema kuolewa niliona nyumba inapwaya na kujikuta nikipata wazo la kuwarudisha nyumbani, hapo ndipo nilipokwenda kwa mtaalamu na kuzisambaratisha ndoa zenu na ninyi kurudi nyumbani bila kujua mimi ndiye mbaya wenu. Niliweza kuwafanya kuzichukia ndoa kitu kilichokuwa furaha yangu.
"Nilifanya hivyo kwa Mwaija ambaye nilikuwa nampenda sana, wewe ndiyo sikutaka kabisa uondoke nyumbani. Yote yaliyokutokea niliyafanya mimi mama yako.
"Wanangu nachukua nafasi hii kuwaombeni radhi kwa yote niliyowafanyia pia namuomba Mwenyezi Mungu anisamehe kwa kila baya nililowafanyia. Sijui bila mama Amina, wanangu wangeendelea kuishi maisha gani.
"Mwanangu najua nimewaumiza bila ya ninyi kujua, naomba mnisamehe nipo chini ya miguu yenu."
Mama alisema huku akinyanyuka kitini ili apige magoti. Tulinyanyuka wote na kumuwahi kabla hajapiga magoti na kumwambia tumemsamehe.
Baada ya zoezi lile, mama Amina alizungumza:
"Nina imani mmemsikia vizuri mama yenu, siku zote mtu akigundua kosa lake na kutubu hata Mungu umsamehe. Mama yenu kagundua makosa yake na leo kayasema yote bila kuacha kitu.
"Kwa vile mmemsamehe nawaomba muishi kama zamani, mpendeni mama yenu. Alifanya vile kwa mapenzi mazito kwa wanaye lakini akawa anaharibu.
"Namshukuru Mungu kwa upande wangu nimemaliza kazi yangu nina imani kila mmoja ameona mabadiliko," mama Amina alituambia.
"Ni kweli," tulijibu kwa pamoja.
"Mimi nafikiri sina cha zaidi, nashukuru tumemaliza salama acha nikimbie," mama Amina alitaka kutuaga.
"Mama Amina tunashukuru kwa kila ulilotufanyia, nina imani si kwa uwezo wetu bali ni Mungu ndiye aliyetuongoza kukujua wewe na kututoa kwenye kiza kizito.
"Kwa upande wa mama bado tunampenda sana tena sana. Alichotueleza hakitapunguza upendo wetu kwake. Tunampenda mama leo, kesho kwa vile kilichofanyika ni funzo si kwake hata sisi tutazaa na kutorudia makosa.
"Mama ondoa unyonge lililopita limepita, tumshukuru Mungu kwa kulifungua mapema kabla hujafa. Inawezekana tukio hili lilikuwa likitukumbusha kumrudia Mungu wetu.
"Namalizia kumshukuru tena mama Amina wewe si mganga tu bali ni sehemu ya familia yetu. Sisi hatuna cha kukulipa bali Mungu ndiye mwenye uwezo huo.
Wadogo zangu hatuna budi kumtunza mama yetu kwa vile amebakia kama jicho letu. Tusimuwekee kinyogo bali tumpende na kumtunza," dada mkubwa alisema kwa hisia kali mpaka machozi yakamtoka.
"Mama nakupenda nitaendelea kukupenda," dada Rehema alisema maneno mafupi.
"Mama nataka kukuambia mapenzi yangu kwako ni makubwa sana, nataka kukueleza chanzo cha matatizo yangu niliyajua muda mrefu toka nikiwa na Beka.
"Lakini bado sikuwa tayari kukuchukia mama yangu, niliamini unatupenda japokuwa sikupenda maisha tuliyokuwa tukiishi, nilijitahidi niwe tofauti na dada zangu.
"Nilikuwa na bahati iliyoishia na matatizo, hata baada ya kugundua sababu ya matatizo yangu bado moyo haukukubali mama unaweza kuwa adui yetu.
"Nimehangaika kuupata ukweli bila mafanikio, na nilipoupata bado niliendelea kukupenda mama yangu, nilitamani kukueleza lakini niliogopa.
"Inawezekana wote hamkujua kikao hiki kimeitishwaje, nataka kuwaeleza, mimi ndiye niliyemfuata mama Amina na kumuomba aitishe kikao hiki ili kuufungua moyo wa mama uliokuwa na mzigo mzito ila sijui kwa dada zangu kwa vile niliyajua haya mapema.
"Mama inawezekana ukaona nimekuvunjia heshima kwa kukulazimisha kuyasema mambo mazito kwetu. Mama naomba unisamehe nilifanya hivyo kwa ajili ya kukuweka huru.
"Nilijua unaumia na kuendelea kuteketea kama mshumaa, huwezi kujua hali uliyokuwa nayo ilitutesa sana wanao kiasi gani. Lakini leo nataka kukuambia toka moyoni kuwa tumezaliwa upya," nami nilimalizia.
"Asanteni wanangu, narudia kusema namshukuru Mungu kunipa watoto wenye mapenzi ya dhati na mama yenu. Nimejifunza kitu nina imani kila kitu ni uweza wa Mungu.
"Mama Amina nashukuru sana mdogo wangu, Mungu atakulipia, narudia wanangu mnisamehe sana."
"Tumekusamehe mama," tulisema kwa pamoja.
***
Kikao kiliisha salama kwa watoto wote kuiswafi mioyo yetu kwa mama. Kwa upande wangu niliutua mzigo mzito ulionielemea moyoni mwangu na kuwa huru huku nikiendelea kumshukuru Mungu.
Furaha ilirudi katika nyumba yetu, dada yangu aliolewa harusi kubwa na mwingine anaendelea na kazi huku akiwa na bwana ambaye alimuahidi kumuoa.
Namalizia kwa kumshukuru mama Amina kwa msaada wake wa hali na mali kuhakikisha anapigania afya yangu mpaka leo hii ninayotoa ushuhuda huu nina afya njema na watoto watatu, wawili wa kike na mmoja wa kiume.
Dada zangu wote wana mtoto mmoja mmoja.
Pia namshukuru sana mwandishi wa mkasa huu kwa kukubali kupoteza muda wake kuandika mkasa mzito kama huu. Mungu atamlipia kwa kazi yake ya kujituma bila kuchoka.
Mwisho kabisa nawashukuru wasomaji wote kwa kupoteza muda wao kufuatilia simulizi yangu mpaka leo ambapo nahitimisha mkasa huu, Mungu atawalipa pia nina imani kuna kitu mmejifunza hasa wazazi nina imani mmeona madhara ya ushirikina.
Wapeni uhuru watoto wenu waishi maisha yao hata kama mnawapenda sana. Naomba kwa leo niishie hapa Mungu awabariki, ahsanteni.


Kwa kunifuatilia hadithi yangu na kuacha shughuli zenu nawapendeni nyote .


MWISHO!
 
MziziMkavu, ahsante sana kwa hadithi nzuri, unajua sisi wafanyakazi tunakuwa busy hata magazeti hatuna muda wa kusoma, so atleast ukipata muda wa kurefresh ndio unasoma jf. Thanks so much, may you live loooong!
 
Back
Top Bottom