nanukuu tu ''Ushauri- tuwe makini na "Agente provocatuers" au in English "provocation agents" nyakati kama hizi. Calmness is the best protection against provocations. Nadhani mmenipata"
Watanzania wengi tunatabia ya kufuatilia upepo unakoelekea na si unapotokea, nimekuwa mfuatiliaji mzuri sana wa ''Detective movies'' nukuu hiyo hapo juu kwangu mie ni Bonge la ''Clue'' sintoufuata upepo uendako nafuatilia utokako!! Siasa zetu kwa sasa zinahitaji umakini sana, haya matukio ya kutekwa waandishi wa habari, wanasiasa kuhusishwa na ugaidi ni mambo ambayo naamini yanafanyika kwa kiwango cha hali ya juu sana iwe yanafanywa kweli au ya kupandikiza! kwa mara ya kwanza nilistuka sana baada ya kuiona video ''Rwakatale' simhukumu kwani ukweli utajulikana mahakamani, kwajinsi maelezo yalivyokuwa mle ilkuwa kama naagalia FBI movies vile na kwa sasa huenda mbinu hii ya ''kutia mtu wasiwasi'' kutisha kwa maneno au vitendo vya kuteka vikaendelea kwani huenda inawafaidisha wanaosingiziwa au kusingizia!! what makes it more interesting na movie hii ni kuwa wahusika ni CCM/SERIKALI na CHADEMA ( mhukika mkuu hajajulikana bado), kwa undani zaidi kuna wahusika wengine wadogo wadogo toka pande zote mbili ambao wamegawanyika na kuishia kutoa siri za wanaodaiwa kuwa wahusika wakuu.... hawana umoja hawa!! hawana siri hawa!! kitu kinacholeta utamu wa movie hii... naamini kutakuwa na mwisho wake ambao ni kuelekea 2015. Kibaya zaidi ni kuwa huenda wahusika wakuu hawatambui kuwa mwisho wa movie hii ni kuwa STELINGI ATAKUFA!!!! napita......