Kinder,
1) Nadhani, kama umesoma post yangu vizuri, nimesema nimeisikia habari hii Jana baada ya kuisoma kwenye Mtanzania na kwenye Mtandao wa Jamii Forum. Ni logic ya kawaida tu huwezi kuitolea Taarifa jambo usilofahamu. Nimesema Mama Zitto hakumjulisha hata Mwenyekiti wa Chama, sasa Chama kingelifanya muujiza gani?
2) Suala la Dr. Slaa kutaka kumdhuru Zitto, unataka nieleze nini wakati Zitto, mwenyewe ameisha sema na kunukuliwa na vyombo vya habari kuwa "haamini" habari hizo? Akili ya kawaida tu inatosha kukuonyesha kuwa ni upuuzi kungangania tamthilia iliyotokea miezi takriban 8, haijawahi kuripotiwa polisi wala na anayedhaniwa kutaka kuuwa, au na hao wanaojidai ni mashahidi wa kuiona kwa macho yao. Jiulize, kwanini walianza kuitoa stori hiyo kwa nguvu zote baada ya kuingia chama hasimu na Chadema. Ungelisoma filosophia ningelikuambia fanny conclusion by "inference",
3) Habari ya Mama Zitto kusema wahusika aliwaona Mwanza... Si la Chama. Nadhani ustaarabu wa kawaida ni kumwomba Mama Zitto amtaje huyo mtu wa Mwanza kwa jina, aeleze walikutana mahali na katika Mazingira gani. Si swala la Chama wala la Katibu Mkuu. Aidha, Kama alisema ni kada wa Chama, ni jukumu la Mama Zitto kuombwa kuweka hadharani viashiria vilivyomfanya "ahisi" kuwa ni "kada wa Chadema".
Mama Zitto ni mjumbe wa Kamati Kuu, kwa nafasi yake Nina hakika anafahamu au anapaswa kuwafahamu macadam wengi wa Chadema kwa kuwa anashiriki shughuli nyingi za Chadema. Nilivyosema ni kuwa kwa majukumu yangu ya Katibu Mkuu nimefanya uchunguzi wetu wa ndani, na kugundua kuwa hakuna kijiwe kinachojengwa na katika eneo la Tabata. Nimepata mawasiliano yote yaliyokuwa yanafanyika, na baada ya kuzungumza na Mama Zitto na Sabula na viongozi wetu wa Tabata ni dhahiri kulikuwa na hill Chafu ya kuichafua Chadema. Ndio maana nimeingia kwa ID yangu bila maficho kwa kuwa ni jukumu langu la Kikatiba kuwaeleza wanachama wetu, wapenzi wetu na wananchi kwa ujumla.
Mimi sijasema Mama Zitto kavamiwa au hakuvamiwa, ila nilichosema, Chadema Kama Chama haikuhusika kama ilivyotaka kuonyeshwa na baadhi ya watu kwa malengo Yao binafsi. Mwenye macho huambiwi tazama, wairaq tunasema mwenye "busara humtambua mwewe mwenye mimba angali angani..." sina hakika Kama nimetafsiri sahihi, lakini nadhani inaeleweka.
Chadema ni chama makini hakiwezi kuingizwa tu kwenye mitego ya hovyo hovyo. Tunaanza na Mungu, Tunabaki na Mungu na Tutamaliza na Mungu.