Mama wa mtoto wangu anataka nimsomeshe

Mama wa mtoto wangu anataka nimsomeshe

Msomeshe kwa sababu unawekeza kwa mtoto wenu. Kumbuka tunatembea tumekufa...usipokuwepo kesho je?

Sent from my HUAWEI TAG-TL00 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu kama anakupenda na mnaishi pamoja lazima abadili dini, wapende wazazi au wasipende.
Pili kama hutambuliki kwao na anataka umsomeshe, basi mwambie unasubiri ruhusa ya wazazi wake mwanamke, kama wakikubali umsomeshe basi wakubali abadili dini umuoe kabisa, lah sivyo basi zoezi hilo ni gumu, ni sawa na kucheza kamali.
Lakini mwisho wa yote unaweza kumsomesha tuu, bila shaka kwamba kwako ni faida kwa namna zote. Yaani akikuacha mwanao atafaidi na akiwepo basi ni faida pia.
 
Msomeshe kama Mzazi wa mtoto wako, sio kama mke wako. Kama uwezo upo lakini.

Kumbuka huyo ni Mama wa mwanao, haitakaa ibadilike. Popote atakapoenda na hali yeyote atalayokuwa nayo, anabaki kuwa mama wa mwanao.

Pia hatujui kesho zetu zitakuaje, kati yenu nani atatangulia mbele ya haki. Utamuacha mtoto kwenye hali gani?

Hili sio lazima ujibu, sema ukweli, mkikutana si mnapasha? Usicheze na kuishi miaka minne na mtu.
 
msomeshe kwa faida ya mwanao, we ni binadam waweza patwa na majanga (kufa) ukashindwa somesha mwanao ila mama yake ukimuandaa atamsomesha huyo binti.
Binti ni nani hapo,mama au mtoto?maana sijui jinsia ya mtoto hadi wakat huu.
 
Eti, kale ka msemo kasemako "mke hasomeshwi!" kana maana gani?
[emoji176][emoji182]
 
Kabla ya yote nikukumbush kuwa asilimia kubwa ya wanawake wanaosomeshwa na wapenz wao huwa wakimaliz masomo na mahusiano hufa,ivyo jiandae kwa yote
Duh. .

Hizi tafiti jamani...!??
 
Anakutoroka huyo Mkuu...

Be careful.
 
Msomeshe kama Mzazi wa mtoto wako, sio kama mke wako. Kama uwezo upo lakini.

Kumbuka huyo ni Mama wa mwanao, haitakaa ibadilike. Popote atakapoenda na hali yeyote atalayokuwa nayo, anabaki kuwa mama wa mwanao.

Pia hatujui kesho zetu zitakuaje, kati yenu nani atatangulia mbele ya haki. Utamuacha mtoto kwenye hali gani?

Hili sio lazima ujibu, sema ukweli, mkikutana si mnapasha? Usicheze na kuishi miaka minne na mtu.


Hili nalo halina uhakika 100% pia mkuu!
 
msomeshe kwa faida ya mwanao, we ni binadam waweza patwa na majanga (kufa) ukashindwa somesha mwanao ila mama yake ukimuandaa atamsomesha huyo binti.
acha mawazo mgando wewe nani kakwambia kusoma ndio kushika pesa
hiyo hela ya kusomesha akipigia mahesabu ananunua ata virikuu vitavyoweza kumsokmesha huyo mtoto ata kama jamaa akiwa hayupo.
 
Wewe msomeshe kwa faida yake na mtoto, halafu mbona kama hujiamini Mkuu!!! Amekupenda, kaishi na wewe muda wote huo pamoja na changamoto lakini bado humuamini. Sasa kilichowaunganisha ni upendo sio dini, misimamo yenu yatosha. Muonyeshe na wewe kuwa unampenda na kumuamini
amwamini naniiii? mwanamke au kiumbe kingine?, acha kumdanganya
 
Dini ni moja ya vitu vilivyoletwa barani Africa na watu weupe baada ya kuja kutunyonya na kuchukua mali zetu.Kwa hiyo asilimia kubwa sisi binadamu tumeathiliwa na dini kutokana na mazingira mfano watu wengi wa kanda za pwani ni waislamu na wale wa kanda za juu na Mbeya waliowengi ni wakristo.Nyie kilichowaunganisha ni mapenzi ya dhati na sio dini. Ushauri wangu kama uwezo unao msomeshe mama wa watoto wako kwa kutenda ihsani na pia kwa ajili yenu na watoto wenu.
 
Kwa hiyo mkuu unamaanisha jamaa ni haramu kwa huyo mwanamke?then mbona basi asirudi kwa babake kuendelea na maisha yake!
Hawa jamaa huwa wanadharau sana.
We talk with them lakini wanachotufikiria ni kibaya sana
 
Mlipie mkuu hata akiondoka ni mama wa mtoto hawezi kuja kumtupa mwanae mtasaidiana kwenye malezi
Hii ndiyo point ya msingi, huwezi jua ya mbeleni anaweza kwama kimaisha au akatangulia lakini kama amemjengea mama msingi bora basi hata mwanae atakuwa katika mikono salama
 
Pambana na ndoa kwanza. Kama wazazi hawataki, je mke mwenyewe anataka au nae hataki?
 
Hili nalo halina uhakika 100% pia mkuu!

Basi aende kwanza kwa mkemia kuondoa shaka.

Inaonyesha wanamawasiliano mazuri tu isipokua suala la ndoa. Jamaa anataka amsomeshe kama mke mtarajiwa kitu ambacho hakiwezekani.

Mimi ni mhanga wa hili jambo. Nilisomesha na naendelea kuwahudumia japo nimeoa na wife anasisitiza kutokuwasahau. Ilikua ni mambo hayohayo ya dini.
 
Basi aende kwanza kwa mkemia kuondoa shaka.

Inaonyesha wanamawasiliano mazuri tu isipokua suala la ndoa. Jamaa anataka amsomeshe kama mke mtarajiwa kitu ambacho hakiwezekani.

Mimi ni mhanga wa hili jambo. Nilisomesha na naendelea kuwahudumia japo nimeoa na wife anasisitiza kutokuwasahau. Ilikua ni mambo hayohayo ya dini.

Hebu funguka zaidi mkuu huenda tukapata cha kujifunza.

Kuna msemo huwa napenda kuutumia: It takes more than love for two people to be together. Hata kama mnapendana lazima muangalie na 'other compatibilities' kama zipo kabla hamjaanza mahusiano.
Changamoto aliyonayo huyu ndugu ni kuwa alishaanza kuogelea baharini sasa inakuwa ngumu kutoka. Hayo ya dini waliyajua tangu mwanzo mwa mahusiano wao. Labda walidhani binti akipata mimba wazazi watakubali. lakini pia, je binti mwenyewe msimamo wake ni upi? Sijasoma mtoa mada ameelezeaje msimamo wa binti. Ndiyo maana wachangiaji wengi - suprisingly, hata wa kike - wamepatwa hofu juu ya hitaji la mama wa mtoto wake.

Thread kama hizi huwa nazipenda kwa ajili ya kufundishia vijana wetu ambao bado hawajafikia huku mbali;

USHAURI KWANZA KWA MTOA MADA: Kama kweli mnapendana na mnataka kuwa pamoja, jua msimamo wa huyo mama wa mwanao kwenye hili kwanza.

FUNZO KWA WENGINE: Msikimbilie kusema mnapendana tu. Angalieni kama na mengine mna-nia moja.
 
My brother Mentor kama kawaida yako kuibua hoja fikirishi. Kwa ulichokieleza hapo juu umemaliza kila kitu.

Kwa ufupi, nilipanga maishani nisiwe na mahusiano yeyote zaidi ya mke wangu. Ulipofika wakati nilipata binti mkristo akaishia kunichanganya nikavundua nilikua bado chekechea kwenye tasnia ya mahusiano. Kosa kubwa nililolifanya, nikahamishia kusudi langu la kumuoa binti wa kiislam niliyekua namfaham kitambo lakini hatukuwa na chochote kati yetu, zaidi ya heshima kubwa ya kaka na dada.

Nilimuuliza uko tayari kubadili dini? Akasema hana tatizo ila itabidi awaulize wazazi wake. Aliwasilisha wazo kwao mzee wake alilikubali kwa shingo upande kuogopa kumuumiza mtoto wake mpendwa.

Kosa lingine, tukaanzisha mahusiano na kukubaliana kupata mtoto kabla ya kufikia muafaka suala la dini na ndoa. Nilikua nimeweka malengo nikiwa na umri flan niwe na mtoto.

Baada ya mtoto, binti akagomz kubadili dini na toka alipojifungua tulikua tunaishi wote. Kwa ufupi tumesumbuana na hilo nikaenda kwao msimamo wa mzee ukabaki palepale, wananipenda sana ila nibadili dini. Miaka minne ilitosha kufikia tamati nikaacha kila kitu na kuanza upya.

Mke wangu wa sasa analiewewa hilo toka mwanzo na alisema hatopenda kuona mtoto anapata shida. Nalipa kodi yao ya nyumba, nikamshauri asome, akasoma certificake kwa sababu alitaka kubadili fani nyingine, nikamsomesha diploma, amefanya vizuri na sasa akitaka kuendelea ntamsomesha.

Ntafanya hivyo hadi atakapopata mtu wa kumuoa kwa sababu ya mtoto.

Namshukuru Mungu tumejaliwa watoto na huyu mke wangu maizha yanaendelea.

Ndio maana nikamshauri jamaa, kama anauwezo, amsomeshe kwa manufaa ya mwanawe kwamba huyo ni mama wa mtoto wake.

Kwenye kujifunza, laiti tungeweza kukaa mbali na mahusiano kabla ya kuoa kama imani zinavyorushauri, dunia ingekea sehem salama na bora kwa kiasi kikubwa mno.
 
Back
Top Bottom