Mama wa mtoto wangu anataka nimsomeshe

Mama wa mtoto wangu anataka nimsomeshe

mafoleni

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2016
Posts
220
Reaction score
372
Habarini wa ndugu,

Mimi ni mwanaume mwenye mke na mtoto mmoja. Tumeishi takribani miaka minne pamoja bila kufunga ndoa kwa sababu ya utofauti wa dini.

Mimi ni mkristo na yeye muislam nimehangaikia sana kuhusu kubadili dini lakini wazazi wake wamekataa katu katu.

Nimeamua tu tuishi hivi hivi japokua sipendi kabisa maana ni kama tunazini na kuendelea kuvunja amri ya sita kwa muda usiojulikana.

Kiukweli nashindwa kumuacha huyu binti kwa sababu tometoka nae mbali sana, tulipanga chumba na sasa tuko kwenye nyumba yetu.

Hoja ya msingi ni hii hapa.
AMENIAMBIA ANATAKA KUSOMA MWAKANI INABIDI NIANDAE ADA""
sasa tatizo linakuja baba yake hapendi kabisa mwanae aishi na mimi, mtoto wake yupo kwangu, akirudi kwao kuja huwa mpaka mizozo yani.

Na chuo anachotaka kusoma kipo huko huko kwao, je si naweza lipa ada halafu akimaliza wakaniachia manyoya! Au nilipe tu jamani. Nahisi naweza somesha mke wa mtu hapa.

USHAURI JAMANI. NILIPE MIZIGO?
 
Habarini wa ndugu, mimi ni mwanaume mwenye mke na mtoto mmoja. Tumeishi takribani miaka minne pamoja bila kufunga ndoa kwa sababu ya utofauti wa dini. Mimi ni mkristo na yeye muislam
Nimehangaikia sana kuhusu kubadili dini lakini wazazi wake wamekataa katu katu. nimeamua tu tuishi hivi hivi japokua sipendi kabisa maana ni kama tunazini na kuendelea kuvunja amri ya sita kwa muda usiojulikana. Kiukwel nashindwa kumuacha huyu bint kwa sababu tometoka nae mbali sana, tulipanga chumba na sasa tuko kwenye nyumba yetu.
Hoja ya msingi ni hii hapa..........!
AMENIAMBIA ANATAKA KUSOMA MWAKANI INABIDI NIANDAE ADA""
sasa tatizo linakuja baba ake hapendi kabisa mwanae aishi na mimi, mtoto wake yupo kwangu, akirudi kwao kuja huwa mpka mizozo yani. Na chuo anachotaka kusoma kipo huko huko kwao, je si nnaweza lipa ada halafu akimaliza wakaniachia manyoya! au nilipe tu jamani. Nahisi naweza somesha mke wa mtu hapa.
USHAURI JAMANI. NILIPE MIZIGO?
yaan jamani kama unampenda usingewaza hata unayowaza
siku hizi vijana hamjui tofauti ya kupenda na kutamani. sioni kama unapenda hapo
 
Kaka hapo tumia hekima ya MUNGU ili wewe usilipe hiyo ada ya chuo au gharama za chuo, kwa sababu kama angekuwa ni wa kwako au mke wako , au mwanamke anayekupenda kweli na muaminifu katika penzi lenu au uhusiano wenu kwa dhati kabisa angefanya jambo juu ya kuweka sawa imani zenu na kuwa na imani moja.
Nikiwa ninamaana angeonyesha nia , au hata kuchukua hatua ya kutafuta wazee ili waongee na kumuelewesha mzazi wake juu ya kufuata imani yako. Kwahiyo kilichopo hapo ni mpango wa kupata faida zaidi baada ya kujenga nyumba ya pamoja sasa anataka umlipie gharama za chuo kwa kivuli cha mke , lakini kweli hapo kitakacho fuata ni kilio. Nina maana bado moyoni mwake hayupo na wewe kama mume mtakayezeeka na kutunzana pamoja, bali unatumiwa tu na baada ya malengo yake kukamilika utaona vumbi tu.
Hebu tusome kwa pamoja Zaburi 45:10-11, imeandikwa, " Sikia, binti, utazame, utege sikio lako, Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako.
Naye mfalme(mume)atautamani uzuri wako, Maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie".
Sasa , kama kweli angekua anakupenda na kukubali kuwa wewe ni mume wake angekusikiliza na kukubali kubadilisha imani yake na kukufuata.
Nafikiri mpaka hapo utakuwa umepata jibu fulani juu ya future yako na mtoto wenu.
 
Habarini wa ndugu,

Mimi ni mwanaume mwenye mke na mtoto mmoja. Tumeishi takribani miaka minne pamoja bila kufunga ndoa kwa sababu ya utofauti wa dini.

Mimi ni mkristo na yeye muislam nimehangaikia sana kuhusu kubadili dini lakini wazazi wake wamekataa katu katu.

Nimeamua tu tuishi hivi hivi japokua sipendi kabisa maana ni kama tunazini na kuendelea kuvunja amri ya sita kwa muda usiojulikana.

Kiukweli nashindwa kumuacha huyu binti kwa sababu tometoka nae mbali sana, tulipanga chumba na sasa tuko kwenye nyumba yetu.

Hoja ya msingi ni hii hapa.
AMENIAMBIA ANATAKA KUSOMA MWAKANI INABIDI NIANDAE ADA""
sasa tatizo linakuja baba yake hapendi kabisa mwanae aishi na mimi, mtoto wake yupo kwangu, akirudi kwao kuja huwa mpaka mizozo yani.

Na chuo anachotaka kusoma kipo huko huko kwao, je si naweza lipa ada halafu akimaliza wakaniachia manyoya! Au nilipe tu jamani. Nahisi naweza somesha mke wa mtu hapa.

USHAURI JAMANI. NILIPE MIZIGO?
shauri zako waza tu ujinga wenzio wanalia sana kuomba ushauri at the end she will get married acha Mara moja mawazo hayo mara 1
 
Kuwa mmezaa pamoja isiwe ndiyo ya kukuzuia kufanya maamuzi sahihi ya maisha yako na mtoto endapo bado hata badili imani yake na kuungana na wewe kama mke mwema wako.
Familia bora ni ile iliyojaa amani mioyoni na kuwa na imani moja kama mnaenda kanisani basi wote kanisani, kama mnaenda msikitini basi wote mnaenda msikitini.
Na siyo kuwachanganya watoto mtakaowazaa kuwayumbisha katika imani, baba imani yake na mama imani yake, hapo ujue muda wowote ule ni sarakasi kwa kwenda mbele. Fanya maamuzi sasa ya future yako Kaka.
 
Wewe msomeshe kwa faida yake na mtoto, halafu mbona kama hujiamini Mkuu!!! Amekupenda, kaishi na wewe muda wote huo pamoja na changamoto lakini bado humuamini. Sasa kilichowaunganisha ni upendo sio dini, misimamo yenu yatosha. Muonyeshe na wewe kuwa unampenda na kumuamini
 
Kuwa mmezaa pamoja isiwe ndiyo ya kukuzuia kufanya maamuzi sahihi ya maisha yako na mtoto endapo bado hata badili imani yake na kuungana na wewe kama mke mwema wako.
Familia bora ni ile iliyojaa amani mioyoni na kuwa na imani moja kama mnaenda kanisani basi wote kanisani, kama mnaenda msikitini basi wote mnaenda msikitini.
Na siyo kuwachanganya watoto mtakaowazaa kuwayumbisha katika imani, baba imani yake na mama imani yake, hapo ujue muda wowote ule ni sarakasi kwa kwenda mbele. Fanya maamuzi sasa ya future yako Kaka.
sio lazima abadili ke hata yeye anaweza badili lamsingi upendo ndio utaompeleka shule na sio imani, kama unawaz kukukimbia utapata hasara gani kama nyumba atakuachia, atabeba na ghorofa lake. wanaume wa mikoani aisee hawajuwi hata mahaba.
 
Back
Top Bottom