My brother
Mentor kama kawaida yako kuibua hoja fikirishi. Kwa ulichokieleza hapo juu umemaliza kila kitu.
Kwa ufupi, nilipanga maishani nisiwe na mahusiano yeyote zaidi ya mke wangu. Ulipofika wakati nilipata binti mkristo akaishia kunichanganya nikavundua nilikua bado chekechea kwenye tasnia ya mahusiano. Kosa kubwa nililolifanya, nikahamishia kusudi langu la kumuoa binti wa kiislam niliyekua namfaham kitambo lakini hatukuwa na chochote kati yetu, zaidi ya heshima kubwa ya kaka na dada.
Nilimuuliza uko tayari kubadili dini? Akasema hana tatizo ila itabidi awaulize wazazi wake. Aliwasilisha wazo kwao mzee wake alilikubali kwa shingo upande kuogopa kumuumiza mtoto wake mpendwa.
Kosa lingine, tukaanzisha mahusiano na kukubaliana kupata mtoto kabla ya kufikia muafaka suala la dini na ndoa. Nilikua nimeweka malengo nikiwa na umri flan niwe na mtoto.
Baada ya mtoto, binti akagomz kubadili dini na toka alipojifungua tulikua tunaishi wote. Kwa ufupi tumesumbuana na hilo nikaenda kwao msimamo wa mzee ukabaki palepale, wananipenda sana ila nibadili dini. Miaka minne ilitosha kufikia tamati nikaacha kila kitu na kuanza upya.
Mke wangu wa sasa analiewewa hilo toka mwanzo na alisema hatopenda kuona mtoto anapata shida. Nalipa kodi yao ya nyumba, nikamshauri asome, akasoma certificake kwa sababu alitaka kubadili fani nyingine, nikamsomesha diploma, amefanya vizuri na sasa akitaka kuendelea ntamsomesha.
Ntafanya hivyo hadi atakapopata mtu wa kumuoa kwa sababu ya mtoto.
Namshukuru Mungu tumejaliwa watoto na huyu mke wangu maizha yanaendelea.
Ndio maana nikamshauri jamaa, kama anauwezo, amsomeshe kwa manufaa ya mwanawe kwamba huyo ni mama wa mtoto wake.
Kwenye kujifunza, laiti tungeweza kukaa mbali na mahusiano kabla ya kuoa kama imani zinavyorushauri, dunia ingekea sehem salama na bora kwa kiasi kikubwa mno.