Kijakazi
JF-Expert Member
- Jun 26, 2007
- 6,443
- 8,953
Pamoja na ukweli kwamba wanaotajwa kuhusika na haya mambo ya Escrow ni wengi ktk Serikali ya raisi Kikwete, lkn ni mmoja tu ndio amekuwa akishambuliwa kila siku kwa kejeli na saa saa nyingine mpaka matusi naye ni Mama Tibaijuka, na ukiangalia sana utaona ya kwamba hakuna sababu nyingine yoyote ya maana zaidi ya ubaguzi dhidi ya Wanawake - Mfumo Dume!
Kama ilivyokuwa kwa Mwanamuziki Flora Mbasha ambapo watu walimshambulia bila hata kujua ukweli, Jamii nzima ikageuka kuwa hakimu na kumhukumu mama Mbasha na kumkingia kifua Mumewe, walimlaumu mama Mbasha kwa kila baya lililoikumba ndoa yao!
Sijasikia Jaji Werema, Chenge,waziri Muhongo au hata Raisi Kikwete mwenyewe wakishambuliwa kwa kiasi ambacho mama Tibaijuka amekuwa akishambuliwa! Hii ndiyo sababu inayonifanya niamini anashambuliwa kwa kuwa ni Mwanamke!
Hakuna jamii Dunia Hii inayodharau Mwanamke kama hii yetu, na iko kila mahali nchini mwetu!
Najua Mama Tibaijuka analijua hili na ametoka mbali, amepitia na kuyashinda mengi hata hili nalo pia atalishinda!
Kama ilivyokuwa kwa Mwanamuziki Flora Mbasha ambapo watu walimshambulia bila hata kujua ukweli, Jamii nzima ikageuka kuwa hakimu na kumhukumu mama Mbasha na kumkingia kifua Mumewe, walimlaumu mama Mbasha kwa kila baya lililoikumba ndoa yao!
Sijasikia Jaji Werema, Chenge,waziri Muhongo au hata Raisi Kikwete mwenyewe wakishambuliwa kwa kiasi ambacho mama Tibaijuka amekuwa akishambuliwa! Hii ndiyo sababu inayonifanya niamini anashambuliwa kwa kuwa ni Mwanamke!
Hakuna jamii Dunia Hii inayodharau Mwanamke kama hii yetu, na iko kila mahali nchini mwetu!
Najua Mama Tibaijuka analijua hili na ametoka mbali, amepitia na kuyashinda mengi hata hili nalo pia atalishinda!