Enyi wadada na wamama wa kileo,tufunge tumwombe Mungu atusaidie tuje kuwa mama wakwe wema wenye upendo wa kweli sio wa kinafiki.Naandika tu lakini nilishamwachia Mungu afanye anavyopenda yeye ila sasa ninazidi kuumizwa.
Hivi kina dada wa humu niambieni,wewe ukiwa na mimba huwa unamwambia mama mkwe? Yamenikuta sikusema ila hua naenda kusalimia wakwe zangu na tumbo wanaliona,sasa mama anasema why sijamwambia maana ndio nimejishaua tunaongea nae kwenye simu yuko mkoani nikajidai nimechoka ila this week ndio naweza kutua mzigo mama,looooh!!! najuta anashangaa kwani wewe ni mjamzito?mbona hujawahi kuniambia!
Niko mama sasa si hua unaniona jamani,anasema nilipaswa nimwambie. Mwenzenu hata mama yangu hua simwambii ananionaga tu tumbo hilo.
Ninachoshangaa ni mimba ya pili ya kwanza pia sikusema waliniona tu.Naumiaje sasa changanyia sipendwi na mama mkwe !Nimelia tu mwenyewe nimefuta machozi nimezama JF kujifariji!
Msiniponde maana mume ndo kashaniponda anasema nijitakia kulia kwani wewe ni mgeni na mama mkwe wako!wali sikuambii nyamaza na kilichokufanya umpigie ni nini?kaondoka akirudi namnunia live!!
Msimtukane mume wangu,nitaumia zaidi,sorry kwa mipaka.
PLEASE PRAY FOR MAMA WAKWE WOTE NA SISI PIA TUWE NA UPENDO WA KWELI!!inafsi ninaupendo sana na wakwe zangu,ni basi tu mama huwa ananikwaza sana.
All in all jukwaa sio lake, hii ipelekwe MMU.
pole mwaya. kama na wewe unamjua mkweo achana na kujikomba. ukishusha kitu muache mwanae aseme mama tumejaaliwa mtoto. ukimuona kaja mkenulie meno (mtori si ananunua mwanae, wewe inakuuma nini?)
Dada, hebu twende taratibu maana umeongea mengi hapa. Tuanze na "blue". Dada usiangalie upande mmoja tu wa mama mkwe, hebu angalia na upande wako je, umejiombea na unajiona una tabia ambazo hazimuudhi mama mkwe? Kumekuwa na tabia ya wanawake wengi kujijengea imani kuwa mamamkwe ni mbaya tu siku zote. Hawafikirii kuwa naye ni binadamu ana mapungufu yake na anatakiwa apate upendo sawa na ule wewe unaoutamani kutoka kwake.
"green" Dada ulipokuwa na mimba hukumwambia mama yako mzazi? Kwa nini usimtreat mamamkwe kama mama yako mzazi? Mama Mkwe wako angefurahi kama ungemshirikisha una mimba, yeye kama mama angeweza kuwa huru kuongea na wewe kuhusu mimba na kupanga mipango mbalimbali kabla ya mtoto hajazaliwa; hii haijalishi eti alikuwa anaona tumbo, kwa hiyo ulitaka yeye aanze kuongea na wewe kuhusu mimba yako kwa kuwa ameona tumbo?? kwa kutokumwambia ulimfanya afunge mdomo na ajisogeze pembeni maana hukutaka kumshirikisha kama ambavyo ungemshirikisha mama yako. Kumbe hii ni mara ya pili na hujajifunza tu kosa lako? Inaonekana hauko karibu hata na mama yako mzazi, pole ila ni vizuri hasa kwa kipindi cha mimba mama yako/mamamkwe ukawasogeza karibu.
Huna sababu ya kulia; jisogeze kwa mama zako. HAKUNA KAMA MAMA. jifunze katika hili tofauti na hivyo utajihesabu unachukiwa na mamamkwe na kuishia kulia kwa makosa yao uliyoyatengeneza mwenyewe. Bila shaka sijakuponda ila nimekwambia ukweli. ZINDUKA jijengee maisha na familia ya amani kwa mikono yako
Na umri wote huu, kumbe bado kuna vitu kibao vya kunishangaza.....
Hivi unamwambia mama mkwe habari za ya mimba ili iweje?? Yeye ni mtaalamu wa magonjwa ya akina mama kwamba atakuwa ndo consultant wako??
Wenye mimba wana raha na amani, kwa nini kijihangaisha na watu wengine??
Watu inabidi wajue kuwa ndoa ni ya watu wazima, labda kama wanataka kuendelea kudekezwa na wazazi!!
Babu DC!!!
Na umri wote huu, kumbe bado kuna vitu kibao vya kunishangaza.....
Hivi unamwambia mama mkwe habari za ya mimba ili iweje?? Yeye ni mtaalamu wa magonjwa ya akina mama kwamba atakuwa ndo consultant wako??
Wenye mimba wana raha na amani, kwa nini kijihangaisha na watu wengine??
Watu inabidi wajue kuwa ndoa ni ya watu wazima, labda kama wanataka kuendelea kudekezwa na wazazi!!
Babu DC!!!
yeye alinyamaza ila akajisemelesha. sijui alitaka mama mkwe amuuguze?
ndo hayo ya mamaz' gal, mimba itasimuliwa hadi style iliyoingilia mweeh!
afu weeh babu umenitapeli. ile issue aisee, nna mpango wa kujitwika mimba ya mapacha hapa ntakuacha ubungo, ohooo!
labda huyo mama ni mkunga au daktari!
Dada, hebu twende taratibu maana umeongea mengi hapa. Tuanze na "blue". Dada usiangalie upande mmoja tu wa mama mkwe, hebu angalia na upande wako je, umejiombea na unajiona una tabia ambazo hazimuudhi mama mkwe? Kumekuwa na tabia ya wanawake wengi kujijengea imani kuwa mamamkwe ni mbaya tu siku zote. Hawafikirii kuwa naye ni binadamu ana mapungufu yake na anatakiwa apate upendo sawa na ule wewe unaoutamani kutoka kwake.
"green" Dada ulipokuwa na mimba hukumwambia mama yako mzazi? Kwa nini usimtreat mamamkwe kama mama yako mzazi? Mama Mkwe wako angefurahi kama ungemshirikisha una mimba, yeye kama mama angeweza kuwa huru kuongea na wewe kuhusu mimba na kupanga mipango mbalimbali kabla ya mtoto hajazaliwa; hii haijalishi eti alikuwa anaona tumbo, kwa hiyo ulitaka yeye aanze kuongea na wewe kuhusu mimba yako kwa kuwa ameona tumbo?? kwa kutokumwambia ulimfanya afunge mdomo na ajisogeze pembeni maana hukutaka kumshirikisha kama ambavyo ungemshirikisha mama yako. Kumbe hii ni mara ya pili na hujajifunza tu kosa lako? Inaonekana hauko karibu hata na mama yako mzazi, pole ila ni vizuri hasa kwa kipindi cha mimba mama yako/mamamkwe ukawasogeza karibu.
Huna sababu ya kulia; jisogeze kwa mama zako. HAKUNA KAMA MAMA. jifunze katika hili tofauti na hivyo utajihesabu unachukiwa na mamamkwe na kuishia kulia kwa makosa yao uliyoyatengeneza mwenyewe. Bila shaka sijakuponda ila nimekwambia ukweli. ZINDUKA jijengee maisha na familia ya amani kwa mikono yako
Mh pole mwenzangu hawa wa mama wakwe hatauwapendeje hawapendeki,me wa kwangu ananiweka roho juu km break ya fire....
yeye alinyamaza ila akajisemelesha. sijui alitaka mama mkwe amuuguze?
ndo hayo ya mamaz' gal, mimba itasimuliwa hadi style iliyoingilia mweeh!
afu weeh babu umenitapeli. ile issue aisee, nna mpango wa kujitwika mimba ya mapacha hapa ntakuacha ubungo, ohooo!