Mama mkwe ananipiga mizinga balaa

Mama mkwe ananipiga mizinga balaa

Mr mgeni

JF-Expert Member
Joined
Apr 27, 2014
Posts
1,222
Reaction score
810
Wandugu natumai mko poa,

Huyu mama mkwe wangu jama ananinyima raha hasahasa pale simu yake itapoita imekuwa kama fomula akinipigia ni mizinga ya hela tu, hana shida kivile anajiweza lakini anataka kula vyangu tu, nimemchoka.Nailea familia ya mke wangu kuliko yangu.

Nipeni ushauri nifanye nini ili mizinga ipungue?
 
Wandugu natumai mko poa,
Huyu mama mkwe wangu jama ananinyima raha hasahasa pale sim yake itapoita imekua kama fomla akinipigia ni mizinga ya hela tu,hana shida kivile anajiweza lakini anataka kula vyangu tu,nimemchoka.Nailea familia ya mke wangu kuliko yangu.nipeni ushauri nifanye nini ili mizinga ipungue?

Kwa uandishi huu ni haki yako kupigwa mizinga maana na yeye kakuona wa UDOM.
 
Nipe namba ya Mkeo niongee nae.. Tatizo litaisha.
 
Kama huna mwambie sina hali ngum heri lawama kuliko fedheha
 
Mizinga yake ya ujananii siipatii picha kama hadi ukubwani analiendeleza.
Na kama mnavyojua mtoto wa nyoka ni nyoka..maji hufwata mkondo. huyo mtoto wake nae vipi mkuu enzi za uchumbaa
 
Mizinga yake ya ujananii siipatii picha kama hadi ukubwani analiendeleza.
Na kama mnavyojua mtoto wa nyoka ni nyoka..maji hufwata mkondo. huyo mtoto wake nae vipi mkuu enzi za uchumbaa
acha kabisa ni zaidi ya mama ake ila kwakuwa nilimpenda sikuona hasara yeyote
 
Msome shida zake, kama anapiga kuomba pesa ya mboga, akipiga kausha unarudisha ile mida watu wameshakula na unamwambia ulikuwa busy.
Si afadhali ingekua mizinga ya hela ya mboga,kikubwa zaidi ana kimkweche chake flan basi utasikia,mwanangu sina hela ya mafuta nataka niende Kibaha nikaangalia shamba langu la mananasi
 
wewe ndio uliokosea tangu mwanzo. ulitumia formula isiyo sahihi,kama mwanzo ulimwambia akipata shida akuombe unategemea nini,ujifunze usitoe ahadi wakati ukiwa Na furaha.

Hii naitumia sana,sijawahi mwahidi mtu yeyeto kwamba nitamsaidia.

#Naamanisha...ata kipindi nasomeshwa na mzazi (namanisha kusomeshwa tena kwa garama saaaana) siku wahi kumwahidi chochote.

leo namtunza na kumuhudumia kuliko alivyo dhani.
 
acha kabisa ni zaidi ya mama ake ila kwakuwa nilimpenda sikuona hasara yeyote
Kama unauwezo mpe..ila kama unaona anakunyonya anza kwa kumwambia mambo ni mabaya..akiona hivyo siku 1 2 3 atajiongeza ila mtoto wake asisikie eeeh
 
Si afadhali ingekua mizinga ya hela ya mboga,kikubwa zaidi ana kimkweche chake flan basi utasikia,mwanangu sina hela ya mafuta nataka niende Kibaha nikaangalia shamba langu la mananasi
Kuna mtu ananisumbuaga sana kwa vibomu, mazingira niliyoyaweka ni kuwa nikiwa kazini siwezi kupokea simu na voice box siku zote iko full. Nilikutana nae akaniambia nidelete voice box. Hajui kuwa yeye ndio chanzo chake.
 
Aibu itabidi ikutoke, siku moja kaa nae umweleze jinsi hali ilivyo ngumu na vibomu vyake vinakuweka kwenye tension.
 
Aisee..Huyo mama mkwe mbona shidaa,kama ana uwezo kwa nini anataka byako. Wazazi wengine wanatia aibu kuombaomba,maisha yamebadilika sana. Yani unakuta mtu anakuvizia ikifika mwisho wa mwezi tu kizinga hichooo. Cha msingi hapo ni kumpotezea,akikupiga kizinga muambie hali yako mbaya. Itafikia point atachoka.. Kuomba hela ni kazi ila kwa wengine aibu hawana
 
We utakuwa unamuonea aibu..Mi mama mkwe uwa nampiga kiswahili hadi mwenyewe anafurahi..Sa hivi ameshanizoea..Basi maisha yanasonga
 
Aibu itabidi ikutoke, siku moja kaa nae umweleze jinsi hali ilivyo ngumu na vibomu vyake vinakuweka kwenye tension.
sorry to bring this up,nadhani nawe itabidi uapply hili kwenye kile kisa chako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom