Mama karibu Mwanza tarehe 08 kwa kampeni (Anza na watu wa Mwauwasa na TANROD)

Mama karibu Mwanza tarehe 08 kwa kampeni (Anza na watu wa Mwauwasa na TANROD)

tausi2020

Member
Joined
Jul 5, 2025
Posts
67
Reaction score
92
Wananchi wanataka usimame hadharani juu ya mambo mawili makuu ambayo yamegeuka mateso makubwa na fedheha kwa jiji:

  1. Maji – Takribani mwezi mzima chanzo cha Butimba kimeharibika. Ulizindua mradi huu kwa matumaini, lakini hali imeendelea kuwa mbaya zaidi:
    • Hata mgao wa siku mbili kwa wiki uliokuwepo awali haupo tena.
    • Juzi, baada ya kelele nyingi za wananchi, maji yalirudi lakini kwa spidi sifuri (0).
    • Wananchi wanateseka sana: wananunua maji kwa shilingi 2,000, wengine hawana kabisa. Hii ni hali ya fedheha na mateso yasiyo na kifani.
    • Mama, uliza hadharani: Hii ni uzembe wa makusudi au kuna wanaokuhujumu? Huu ni wakati wa kutoa kauli kali ya utenguzi – wananchi hawawezi kuendelea kuvumilia mateso haya.
    • Piga marufuku mradi wa uuzaji maji kwa magari unao fanywa na Mwauwasa hi ndo iadsbsbisha wazembee kutoa maji ili watu wanunue.
  2. Barabara – Hali ya Mabatini na Mkuyuni ni aibu kubwa. Ni vipande vidogo tu, lakini mkandarasi hafanyi kazi kwa uharaka. Foleni zimekuwa mateso ya kila siku, watu wanasota masaa barabarani. Hii ni barabara kuu ya jiji, haiwezekani ikakaa mwaka mzima bila kukamilika.
    • Mama, ukifika Mkuyuni, simama hadharani na utembelee vipande hivyo. Wananchi wanataka majibu ya papo kwa papo.
👉 Mama, ukitatua tatizo la maji na barabara, hakuna atakayebaki na hoja Oktoba – kaulimbiu yenu itafanya kazi moja kwa moja.

Tunasisitiza pia usimame na kusikiliza wananchi uso kwa uso katika maeneo haya: Buhongwa, Mkolani, Nyegezi Stend, Mkuyuni na Mabatini.
 
Kwakweli barabara za Mwz zimechoka hasa Mwz- Shinyanga kadhalika Mwz - Musoma mitaani nako zimeharibika mno ukizingatia mji ulivyokuwa na idadi ya watu na vyombo vya usafiri kutoka Usagala inahitaji kuanzia njia 4 kama sio sita kuelekea mjini na njia ya Musoma nayo.
 
Wananchi wanataka usimame hadharani juu ya mambo mawili makuu ambayo yamegeuka mateso makubwa na fedheha kwa jiji:

  1. Maji – Takribani mwezi mzima chanzo cha Butimba kimeharibika. Ulizindua mradi huu kwa matumaini, lakini hali imeendelea kuwa mbaya zaidi:
    • Hata mgao wa siku mbili kwa wiki uliokuwepo awali haupo tena.
    • Juzi, baada ya kelele nyingi za wananchi, maji yalirudi lakini kwa spidi sifuri (0).
    • Wananchi wanateseka sana: wananunua maji kwa shilingi 2,000, wengine hawana kabisa. Hii ni hali ya fedheha na mateso yasiyo na kifani.
    • Mama, uliza hadharani: Hii ni uzembe wa makusudi au kuna wanaokuhujumu? Huu ni wakati wa kutoa kauli kali ya utenguzi – wananchi hawawezi kuendelea kuvumilia mateso haya.
    • Piga marufuku mradi wa uuzaji maji kwa magari unao fanywa na Mwauwasa hi ndo iadsbsbisha wazembee kutoa maji ili watu wanunue.
  2. Barabara – Hali ya Mabatini na Mkuyuni ni aibu kubwa. Ni vipande vidogo tu, lakini mkandarasi hafanyi kazi kwa uharaka. Foleni zimekuwa mateso ya kila siku, watu wanasota masaa barabarani. Hii ni barabara kuu ya jiji, haiwezekani ikakaa mwaka mzima bila kukamilika.
    • Mama, ukifika Mkuyuni, simama hadharani na utembelee vipande hivyo. Wananchi wanataka majibu ya papo kwa papo.
👉 Mama, ukitatua tatizo la maji na barabara, hakuna atakayebaki na hoja Oktoba – kaulimbiu yenu itafanya kazi moja kwa moja.

Tunasisitiza pia usimame na kusikiliza wananchi uso kwa uso katika maeneo haya: Buhongwa, Mkolani, Nyegezi Stend, Mkuyuni na Mabatini.
Hapo mwanza anakuja kuomba kura tu haji kama rais kwahiyo hakuna hasira au lolote atakalo fanya zaidi ya kuahidi na kuomba kura.

Hata hivyo kweli kwa akili yako unadhani wana siasa wako serious na shida zenu hasa hawa wanaotubagaza.
 
Maji changamoto wakati ziwa mnaliona? Bora Dar walalamike bahari ina chumvi.
MWAUWASA jipu.
 
Nasikia Mwanza wanahaha kupata maji. Hata ya kuchambia hamna wakati wako na fresh water lake.
Mwanza mjilaumu wenyewe. Serikali haihusiki kwenye huu ujinga.
 
Mpe nafasi amalize matatizo hayo na mengine yeye ni nguli wa kutatua matatizo 👍
Oktoba ...
 
Back
Top Bottom