VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Kutokana na kutoonekana kwenye kampeni za mumewe, Dr. John P. Magufuli, Mama Janeth Magufuli ametumiwa ujumbe na CCM ili ajiunge kwenye kampeni za Dr. Magufuli. Ujumbe huo wa kichama ulitumwa kupitia wanamama manguli chamani ili kwenda kumpigia kampeni mumewe na kufanya ayafanyayo Mama Regina Lowassa, mke wa mgombea wa CHADEMA Edward Lowassa.
Katika kikao hicho cha kichama na kirafiki ili aafiki, Mama Magufuli aligoma kujiunga kwenye timu kampeni za mumewe zinazoendelea kurindima nchi nzima. Mama Magufuli, aliyesemekana kuwa mkali, alisema kuwa aachwe aendelee kufundisha wanafunzi wake wa Mbuyuni Primary School kwakuwa yeye si mwanasiasa. Mama Magufuli amewadokeza wapeleka ujumbe kuwa amekubaliana na Dr.Magufuli juu ya uamuzi wake wa kutoambatana naye kwenye kampeni.
Wajumbe waliopeleka ujumbe wa chama walibaki kimya na kurudisha majibu hayo ya mgomo. Turufu ya mwisho ya kumshawishi Mama Magufuli kujiunga kwenye kampeni imebaki kuwa Mama Maria Nyerere ambaye anatajwa kuwa na uwezo wa kumshawishi Mama Magufuli. Mama Magufuli atakutanishwa hivi karibuni na Mama Nyerere nyumbani kwa Hayati Mwalimu Nyerere Dar es Salaam ili kuyaweka sawa mambo hayo.
Inampasa Mama Magufuli aige mfano na awe kama Mama Regina Lowassa!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Katika kikao hicho cha kichama na kirafiki ili aafiki, Mama Magufuli aligoma kujiunga kwenye timu kampeni za mumewe zinazoendelea kurindima nchi nzima. Mama Magufuli, aliyesemekana kuwa mkali, alisema kuwa aachwe aendelee kufundisha wanafunzi wake wa Mbuyuni Primary School kwakuwa yeye si mwanasiasa. Mama Magufuli amewadokeza wapeleka ujumbe kuwa amekubaliana na Dr.Magufuli juu ya uamuzi wake wa kutoambatana naye kwenye kampeni.
Wajumbe waliopeleka ujumbe wa chama walibaki kimya na kurudisha majibu hayo ya mgomo. Turufu ya mwisho ya kumshawishi Mama Magufuli kujiunga kwenye kampeni imebaki kuwa Mama Maria Nyerere ambaye anatajwa kuwa na uwezo wa kumshawishi Mama Magufuli. Mama Magufuli atakutanishwa hivi karibuni na Mama Nyerere nyumbani kwa Hayati Mwalimu Nyerere Dar es Salaam ili kuyaweka sawa mambo hayo.
Inampasa Mama Magufuli aige mfano na awe kama Mama Regina Lowassa!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam