Mama Fulani, Nitakupenda Mpaka Kifo Kitakapotutenganisha!

Najua Bado sijakuoa ila Nina uhakika wa Kukuoa Kwa Mapenzi yake Mwenyezi Mungu!

Ulikuja Katika Maisha yangu wakati ambao nahitaji mapenzi ya mwanamke kwa kiasi kikubwa!

Ni wewe uliyerudisha Nafsi ya upendo iliyopotea baada ya kutokea kuumizwa na wanawake niliowahi kuwapenda!

Ni wewe uliyerudisha thamani ya upendo ndani ya Nafsi yangu!

Mwili na Nafsi yangu imenenepa kwa sababu yako, umenifanya kuwa bora mpaka wanawake wengine wananitamani!

Siku zote nakuombea kwa Mwenyezi Mungu azidi kukupa uzima wa Afya ya mwili na roho!

Si Juzi ulinambia Nisome wakorintho 1, 13...4-7, nimesoma mama na kilichomo mle ntakitimiza!

Nami Nakuahidi, Nitakupenda Kama Mke Wangu, Nitakulinda Kama Binti Yangu na Nitakuheshimu Kama Mama Yangu!

Nitakupenda Mpaka Kifo Kitakapotutenganisha!

Ni mimi Alfred!
Siku ikifika wewe lazima utajinyonga huyo ni shetani amekuwekea chambo ukisha jaribu kumeza ndoani anakumaliza kimbia haraka.
 
Humu ndani watu wanataka uelezee ubaya wa ndoa/mahusiano tu.Ukielezea mazuri utaskia "penzi jipya hilo"mara "subiri utakuja kulia".Jamani mahusiano hayatakiwi kuwa na nyakati za furaha?
 
Mbona povu mkuu? Unataka kutuambia umetembea na wanawake wote hapa duniani?

Yani wewe kukutana na malaya akakutenda ndo unataka sisi tusiwapende wake/wapenzi wetu?
Toa uharisho wako apa
 
Hahahaaaa....... Limbwata likikolea bwana hadi raha..huyu sangoma kiboko.
 
Humu ndani watu wanataka uelezee ubaya wa ndoa/mahusiano tu.Ukielezea mazuri utaskia "penzi jipya hilo"mara "subiri utakuja kulia".Jamani mahusiano hayatakiwi kuwa na nyakati za furaha?
Asante kwa Mchango Murua Kabisa Ndugu!
 
Mama fulani , ntamtafuta anipe maujanja, mana sio kwa sifa hizo anazopewa. Baba fulan nipe namba yake
 
wakorintho 1, 13, 4-7

4 Upendo+ ni wenye ustahimilivu+ na wenye fadhili.+ Upendo hauna wivu,+ haujigambi,+ haujivuni,+ 5 haujiendeshi bila adabu,+ hautafuti faida zake wenyewe,+ hauchokozeki.+ Hauweki hesabu ya ubaya.+ 6 Haushangilii juu ya ukosefu wa uadilifu,+ bali hushangilia pamoja na kweli.+ 7 Huhimili mambo yote,+ huamini mambo yote,+ hutumaini mambo yote,+ huvumilia mambo yote.+
 
Hongereni, na mpendane kweli kweli. Hii ahadi ni rahisi kuitamka ila ngumu sana kuitekeleza. Hivyo muombe sana Mungu awasaidie muishi kadri ya ahadi hiyo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom