Mama ana chawa wake?

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,759
699,085
Chawa ni nani?

Hilo ni jina la Kiswahili, kiingereza ni lice na kwa jina la kitaalam ni Phthiraptera
Kiasili chawa ni aina ya wadudu wadogo tambazi wanaopenda kuishi kwenye miili ya binadamu wachafu na baadhi ya wabyama wafugwao wasiotunzwa kwenye mazingira safi

Chakula chake rasmi ni damu anayonyonya toka kwenye mwili wa binadamu au mnyama (hawa wa kufugwa) na akifanikiwa kupenya kwenye vidole vya miguu michafu hujichimbia kwenye ile ngozi laini na kugeuka funza na kutaga mayai humo

Funza ana mzio na watu wasafi! Kamwe hawezi kuweka makazi yake kwa watu safi wanaoishi kwenye mazingira safi.. Pepo yake ni kwenye mwili, mchafu wenye nywele chafu, kucha chafu,nguo chafu, humo hufanya makazi yake na kutaga mayai yake! Hufyonza damu kwa ajili ya chakula, na huwasha ngozi.. Ule muwasho wake ukijikuna upele hufuata.. Huleta na magonjwa mengine pia!

Kwa kifupi chawa si mdudu mwema maana ana hasara nyingi kuliko faida na mtu kufananishwa ama kuitwa chawa kama sio sifa mbaya basi ni dhihaka kubwa ama ni tusi au ni kejeli

Wahenga wana usemi wao kwa kutumia lahaja wanapotaka kumuelezea mtu mbaya.. Usemi huu asili yake ni chawa mwilini... Unasema hivi! Kikulacho ki nguoni mwako!

Nilipomsikia bi mkubwa akisema ana chawa wake niligutuka kwa mshtuko na fadhaa kubwa, maana kila kinachoonekana kwa macho ya nyama kina replica ya kiroho!

giphy.gif


Happy new year BELOVED TANGANYIKA
 
Siajabu hata hawaelewi kwamba chawa ni parasite ni kama kupe kwa mnyama kazi yake ni kunyonya Damu ndio hapo ujue statistics zinaposema Tanzania tuna low IQ below average ni ukweli, kwani huyo parasite mnyonya damu anachukuliwa kama sifa yaani ni sifa kuitwa parasite, kwa Mtanzani ni kitu positive kuitwa parasite halafu tunagegemea tutatue complex problems za 21 st century na uwezo huo? No wonder hakuna maji, umeme wala chakula cha kutosha, halafu wanatoa takwimu kujisifu uchumi unakuwa huku wanakata umeme masaa 12 kwa siku.

Go figure hii nchi watu wana very low IQ!
 
Siajabu hata hawaelewi kwamba chawa ni parasite ni kama kupe kwa mnyama kazi yake ni kunyonya Damu ndio hapo ujue statistics zinaposema Tanzania tuna low IQ below average ni ukweli, kwani huyo parasite mnyonya damu anachukuliwa kama sifa yaani ni sifa kuitwa parasite, kwa Mtanzani ni kitu positive kuitwa parasite halafu tunagegemea tutatue complex problems za 21 st century na uwezo huo? No wonder hakuna maji, umeme wala chakula cha kutosha, …

Go figure hii nchi watu wana very low IQ!
Ni familia moja na kunguni papasi na viroboto
 
Chawa alitaka kumaanisha ana mbwa wake ambao watang'ata wanaobeza ama kutukana, kwa hio sio mstahimilivu kisiasa, anapenda kusifiwa sana. Angepaswa aseme mimi ntaziba masikio mkiongea yenu mimi napiga kazi, kuogofya ni udhaifu mkubwa sana
 
Je binadamu anaweza kuwa chawa? Mdudu Chawa yuko kwenye kundi la vimelea (parasites) wakiishi kwa kutegemea damu toka kwa viumbe hai kama binadamu na wanyama! Sifa pekee inayomtofautisha chawa na vimelea wengine ni kwamba yeye ni lazima makazi yake yawe mwilini na huo mwili lazima uwe mchafu!

Binadamu kuitwa chawa lazima awe na tabia zote za chawa! Chakuumiza ama cha kufurahisha ni kwamba chawa huwa hana mwisho mwema!
head_louse_home2.jpg
 
Back
Top Bottom