Leo kwenye post ya kada wa chama cha Mbowe ndugu Yericko Nyerere nimeona post inayoelezea kada mwenzie Malisa Godlisten akilalamikia kulamba Block toka kwa Mheshimiwa Nape huko Twitter. Mimi sifurahishwi kabisa na mambo ya watu kupigana block mitandaoni kwasababu ni mwanzo wa chuki na upotevu wa amani. Sio jambo dogo kama linavyochukuliwa. Ikitoka block ya mtandaoni itafuatia block ya nje ya mtandao ambayo ni mbaya sana.
Nimemwonea huruma Malisa kwa kilichomkuta ila naye akumbuke kuwa hana tofauti na Nape kwenye suala la block. Tena inawezekana Nape ana unafuu kuliko Malisa. Huyu kada wa CHADEMA ukitoa maoni tofauti na yake unakula block fasta. Wahanga wa hii tabia yake mbaya ni wengi sana. Malisa hana uvumilivu wowote wa kisiasa na dikteta aliyejificha kwenye mwamvuli wa kusaidia watu.
Kama ameamua kuwa msaidiaji wa wenye shida kupitia watanzania wenzake basi ajikite zaidi huko badala ya ku-block watu ambao pia huchangia pesa kila anapotoa wito. Malisa anafanya mazuri mengi ila anaharibu kwa kitu kidogo ambacho ni kutoruhusu mawazo tofauti kwenye mada zake anazopost. Tabia aliyo nayo Malisa ndo tabia ya madikteta wote waliowahi kuwepo duniani na waliopo kwa sasa.
Namkumbusha kijana huyu kubadilika kwa sababu tabia hii ikiendelea itazaa tabia nyjngine mbaya zaidi ya kutotaka kupingwa kwa lolote. Yeye akiitwa coward atafurahi? Kuhusu kusaidia wenye shida tuendelee kumuunga mkono.
Nimemwonea huruma Malisa kwa kilichomkuta ila naye akumbuke kuwa hana tofauti na Nape kwenye suala la block. Tena inawezekana Nape ana unafuu kuliko Malisa. Huyu kada wa CHADEMA ukitoa maoni tofauti na yake unakula block fasta. Wahanga wa hii tabia yake mbaya ni wengi sana. Malisa hana uvumilivu wowote wa kisiasa na dikteta aliyejificha kwenye mwamvuli wa kusaidia watu.
Kama ameamua kuwa msaidiaji wa wenye shida kupitia watanzania wenzake basi ajikite zaidi huko badala ya ku-block watu ambao pia huchangia pesa kila anapotoa wito. Malisa anafanya mazuri mengi ila anaharibu kwa kitu kidogo ambacho ni kutoruhusu mawazo tofauti kwenye mada zake anazopost. Tabia aliyo nayo Malisa ndo tabia ya madikteta wote waliowahi kuwepo duniani na waliopo kwa sasa.
Namkumbusha kijana huyu kubadilika kwa sababu tabia hii ikiendelea itazaa tabia nyjngine mbaya zaidi ya kutotaka kupingwa kwa lolote. Yeye akiitwa coward atafurahi? Kuhusu kusaidia wenye shida tuendelee kumuunga mkono.