Mali za Kijerumani

kuna vijana walijitoa mhanga kule loliondo wakachimba miezi kadhaa wlipofanikiwa wakakuta chini kuna room ukawa mziki jinsi ya kuingia huko ila kabla hawajafaninkiwa wakakamatwa na wanajeshi. Serikali kipindi cha Mkapa wakawaita wajerumani wakaja kuchukua kiulaini sijui serikali ilipewa nini, mali zipo nyingi sana
 
kuna kazi namalizia kiwangwa baada ya week narudi kuleta ushuhuda ila ngumu sana.nilipanga niende j'pili ila kuna kazi nyingine nafanya,kama ungekuwa au upo hapa dar ningekuambia tufuatane ukajifunze kwa vitendo.ila safari ipo sooon

Wewe kijana,kuwa makini mambo si rahisi namna hiyo,
 

mkuu si muda mrefu nimetoka saiti vijana wanapiga kazi na kwa uhakika kabisa nashuhudia uwepo wa mali pale.
 
MIE binafsi nimeshiriki kuzichimba huko kondoa irangi maeneo ya vijijini kunaitwa king'ang'a ,ila kiukweli hawa jamaa walitumia akiri sana michoro ipo ila pia mingine ya kukupoteza .Mwisho wa siku nilikata tamaa kwani nilivunja mazege mpaka nikahisi kifo kwani kuna manyaya nikahisi hawa watu wameweka mabomu.
 
kuna kazi namalizia kiwangwa baada ya week narudi kuleta ushuhuda ila ngumu sana.nilipanga niende j'pili ila kuna kazi nyingine nafanya,kama ungekuwa au upo hapa dar ningekuambia tufuatane ukajifunze kwa vitendo.ila safari ipo sooon

Ukifika Kiwangwa msalimie zimwi la nchi.
 

Ni kweli mjerumani mmoja alikuja na ramani pale misigiri-sekenke alipoisoma akachukua watu wakamsaidia kuchimba chini akatoa miche ya dhahabu kibao kila shimo ambalo lilimiminiwa zege kali sana, kulikuwa na sefu za dhahabu tano sehemu tofauti pale
 
Hii sio dhana, ni kweli! Ninafahamu baadhi ya location ambapo treasure zipo.. Pia nimefanya biashara hiyo, tatizo sikuwahi kufanikiwa. Kila unapopata mali (sio madini) ukipeleka sokoni unaambiawa sio.. Wajerumani wanatumia spray flani hivi kuweza ku-easen utoaji wa hizo mali.. Walivyozihifadhi walitumia mizimu na teknolojia ya sayansi.. Its too risky bzness na pia ni illegal, simshauri mtu afanye! Tuiache serikali ifanye, maana ni pekee itakayoweza, ikishirikiana na wajerumani.. Kwa maana kuna sehemu (sijafika lakini nimesikia) walitega na mabomu..

Hizo hazina ni nyingi zaidi kanda ya ziwa!

Kwa uchunguzi wangu nimepata kumjua mtu mmoja tu aliyewahi fanikiwa kwa shughuli hizi, alipata pesa uncountable, in 10yrs, sasa hivi ni maskini wa kutupwa!..

I knw inn and out of this project-bzness!! Na vitu vingi nimeviona na kuvishika! Uchawi mwingi.

TUFANYE KAZI HALALI.. NO SHORT CUT IN LIFE.
 

Shukran hapo umenena tufanye kazi ki wazi na halali hayo ni ya haraka na mazingaombwe poa km kuna ukweli basi nasema mungu awabarikie mfanye nyie ila muwe na tahadhari na matapeli
 
Inasemeka hata shule ya old moshi ya zamani sasa ni kolila inayomilikiwa na kkkt kuna kanisa pembeni ni makaburi ya wajerumani alf kuna handaki mlango wa kuingilia upo ndani ya jengo la shule pia kunasehemu kama mnala full zege yawezekana nako kuna mali pia
 

Mhhh.....
 
Hapo zamani sana vitu kama almasi,rubi,na vingine vingi vya thamani vilikuwa ni madini yaliyotapakaa juu ya ardhi kama mawe ya kawaida wakoloni hawa waliweza kuokota kwa wingi jinsi walivyopenda huku wenyeji tukichezea bao bila kufahamu kama ni mali,kwa vyovyote kwa wingi huo isingekuwa rahisi kuondoka na mizigo yote
 
Mbona hakuna anayeleta ushahidi pasi na mashaka kuwa wamefanikiwa kupata hizo

Mali kwa mfano mtu aseme

Sehemu mfano Iringa wamepa sanduku lenye mali pia na aina mfano dhahabu
almasi n.k
 
BUT U CAN SPEND IT AS "ADVENTURE TOUR" WAKATI WA LIKIZO JUST LIKE LEiSURE
 
Naona dalili ya kuibuka Mwaisapila wa pili!
 
Hi bro uhakika bado hauko
Kweli tunaambiwa kuna mali nyingi za thamani kubwa walakin mengi au wengi wao ni wazushi mimi huwa nafatilia sana hz sehemu walakin sijawahi kuona yoyote kati ya hao alifanikiwa. Nadhani ni hadithi tu na uhakika bado hauko

Kweli inawezekana ni stori tu lakini kuna kipindi pale Singida kulikuwa na uchimbaji wa kufuatilia thamani hizona watu walikuwa wanatoana kafara sana, mimi nakubaliana na mtoa mada na maeneo mengi yake waliweka vitu visivyoweza kuhamiskika kwa urahisi mfano: Makanisa, Magereza na kadharika. mfano Gereza moja hivi kule Urambo-Tabora kuna habaria za kuaminika kuwa kulikuwa na machimbo ya madini.
 
Kweli mimi pia nimesikia kwa Bwana mmoja ambaye yeye alisafiri na mjerumani wa kike na msome hasa walienda morogoro milimani yaliyofanyika ni mambo ya hatari mfano walienda sehemu wakakuta makaburi na wakaamrishwa wapake masizi then huyo mama kaenda sehemu kama kuna hifadhio ya madini na nahisi ilikuwa kama madini ya mercury na mmoja wa wana kijiji alikimbia toka milimani kwa kuogopa hali hiyo,kimsingi kuna baadhi ya madini wamehifadhi kwa alama maalum
 
Hadithi hizi hazikuanza hivi karibuni! Huko Tukuyu, Mbeya kuna ziwa linaitwa Kibisi ambalo halina sehemu inayooneka kwa macho kama inaingaza maji ziwani humo au kutoa ambalo Wajerumani baada ya kushindwa vita ya pili ya dunia walitupa hazina kubwa ya mali ambayo upatikanaji wake ni mgumu kwani kila anayezamia na kutaka kuitoa anakumbana na mauzauza mengi ikiwemo kutokewa na joka kubwa linalotisha!

Inasemekana kuna wazungu walijaribu kuitoa hazina hiyo wakashindwa baada ya mmoja wao kuzamia huku akiwa amefungwa vifaa maalumu pamoja na minyororo ya kufungia masanduku ya chuma yanayosemekana yapo chini ya ziwa. Mzungu huyo hakurudi juu wala masanduku na kupotelea chini ya ziwa na kuwafanya wenzake kuondoka kwa majonzi makubwa badala ya furaha!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…