Malecela: Kingunge hana shukrani

Malecela: Kingunge hana shukrani

Lakini alisema kuna hadi waandishi wa habari kwenye orodha yake.

Anyway ngoja tuone hiki kimbunga kitaishaje.

Kwa mwelekeo ulivyo ndani ya ccm kuna uwezekano membe akapitishwa na cc yao,kwani naona nape keshaenda kwenye jimbo la membe kutia nia ya ubunge
 
kaongea vizuri tuache unazi na unafiki. huyu mzee kaona mbali japokuwa wana bifu kwa kuwa mamvi alimpiga kwenye dili la magar ya serikal ktk japan.
 
Mkuu na wengine hawa huku lazima kieleweke tu
View attachment 255994

Mnamdanganya nani nnyie kambi ya Membe. Membe kapewa pesa na waarabu hazina kipimo, ukichanganya na mahoteli yake na bado mnasema PESA SIO KILA KITU? Msituone kimya, watanzania tunajua kila kitu kinachoendelea. Chungu anachomega Rizwan hakiwezi kuwa na baraka hata kidogo. Damu ya watoto na machozi ya wazazi wao walioathirika kwa madawa ya kulevya ni laana tosha kwa kami hii.
Mngekuwa na busara hata hizo nia msingetangaza. CCM tuachieni Mchemba, Nyerere na Pinda watunishiane misuli
 
Kwa mwelekeo ulivyo ndani ya ccm kuna uwezekano membe akapitishwa na cc yao,kwani naona nape keshaenda kwenye jimbo la membe kutia nia ya ubunge

CC ya CCM haipitishi jina la mtu moja tu, inapendekeza majina tano, hivyo kama Membe atapitishwa na CC ya CCM yatakuwepo tena majina mengi 4 ya wana-CCM
 
View attachment 255993
Mwanasiasa mkongwe wa CCM mzee John Malecela amemshangaa mzee Kingunge na kumuita Yuda na msaliti, ndumilakuwili na mchochezi na hana shukrani hakumbuki alichofanyiwa na serikali ya Kikwete huyu Kingunge.

Anakusanya ushuru stendi ya Ubungo na maeneo mengine ya mji hela anazokusanya kila siku anampa nani au aliwashawahi kutoa msaada wowote kwenye kituo cha kulea watoto yatima? Mzee Malecela amesema Kingunge aache kabisa kuwachagulia mtu anayefaa kuwa Rais kazi hiyo ipo mikononi mwa CCM kwenye mkutano mkuu hata CHADEMA, CUF hufanya hivyo kwenye vikao vyao maalumu.

Mzee Malecela amesema kura ya veto iliyomtoa manyoya yeye wakati anagombea Urais ndio itakayotumika kuangalia mgombea mwenye Sifa zote zinazohitajika kwa Tanzania ya sasa na nyingine pia awe msafi, mpole, mchana Mungu mwenye maadili.

Malecela amesema Rais hawezi kupatikana kwa kelele za watu, porojo na maigizo; muda ukifika kila Mgombea atabeba msalaba wake.

Kwa matendo waliyoyafanya kugawa watu kwa kuwanunua kwa uchu wa madaraka, mbegu hiyo ni mbaya sana kwa Taifa kwani kuna uwezekano Taifa lilitagawanyika tusipokuwa makini na wasaka urais kwa nguvu.
Malecela is useless, alishindwa hata na kibajaji
 
...huyu anajikomba tuu si mamsap kapewa kacheo.....angekuwa na busara angeshindwa na kibajaji chenye akili za kuku kishingo ??
 
Sasa hawana pa kujificha zaidi ya kukiri kwamba CHADEMA NI KISMA CHA FIKRA NA NDIO NYOTA INAYOONGOZA NJIA.
 
View attachment 255993
Mwanasiasa mkongwe wa CCM mzee John Malecela amemshangaa mzee Kingunge na kumuita Yuda na msaliti, ndumilakuwili na mchochezi na hana shukrani hakumbuki alichofanyiwa na serikali ya Kikwete huyu Kingunge.

Anakusanya ushuru stendi ya Ubungo na maeneo mengine ya mji hela anazokusanya kila siku anampa nani au aliwashawahi kutoa msaada wowote kwenye kituo cha kulea watoto yatima? Mzee Malecela amesema Kingunge aache kabisa kuwachagulia mtu anayefaa kuwa Rais kazi hiyo ipo mikononi mwa CCM kwenye mkutano mkuu hata CHADEMA, CUF hufanya hivyo kwenye vikao vyao maalumu.

Mzee Malecela amesema kura ya veto iliyomtoa manyoya yeye wakati anagombea Urais ndio itakayotumika kuangalia mgombea mwenye Sifa zote zinazohitajika kwa Tanzania ya sasa na nyingine pia awe msafi, mpole, mchana Mungu mwenye maadili.

Malecela amesema Rais hawezi kupatikana kwa kelele za watu, porojo na maigizo; muda ukifika kila Mgombea atabeba msalaba wake.

Kwa matendo waliyoyafanya kugawa watu kwa kuwanunua kwa uchu wa madaraka, mbegu hiyo ni mbaya sana kwa Taifa kwani kuna uwezekano Taifa lilitagawanyika tusipokuwa makini na wasaka urais kwa nguvu.

FICTION TOPIC TO BE IGNORED/ MALECELA AIBUKIE WAPI ACHENI UONGO!!!/i
 
tuseme yote lakini huyu mzee ana pointi. hivi kingunge kwa nini asingetuli kusubiri vikaompaka akajidhalilishr pale arusha?
 
Huyu babake 'nanihi',si ndiyo Mwalimu Nyerere alisema ni MUHUNI?
 
Ukiona ndugu(CCM) wanagombana shika jembe ukalime.CCM siyo vyama vya upinzani vya bongo(Vitega uchumi).
Mkuu sijakuelewa ,unamaanisha serikali yetu ni mbovu kiasi Kwamba haiwezi kutofautisha chama cha siasa na kitega uchumi cha mtu na hivyo kuangalia nani apate ruzuku na nani ni kitega uchumi asipate
 
Kama hata kazi ya kukusanya ushuru kazi ambayo wengeweza kufanya hata watu wa kawaida,wanapewa akina Kingunge kama ulaji wao,sasa vijana na watoto wa masikini watafanya kazi gani?.

Kwa mtindo huu wa kupeana ulaji sidhani kama hata kodi ya serekali inalipwa kama inavyositahili.

Halafu watangaza nia wa CCM bila aibu, wamekazana kujinadi mkinichagua nitazalisha nafasi nyingi za ajira,utazalisha nafasi nyingi zipi za ajira wakati nafasi zenyewe ndio hizi mnazo peana ulaji,ambazo zingeweza kufanywa na vijana wa kawaida tu.
 
Back
Top Bottom