Malecela: Kingunge hana shukrani

Malecela: Kingunge hana shukrani

Hivi mwenyekiti wa sasa alikikuta chama vipande vipande kama hivi au yeye ndiye kakigawa!?
Na je, tumlaumu mzee Kingunge, Malecela na wataofatia (yaani vipande) au tumlaumu mgawaji!?
Kikubwa kabisa: Watanzania tutakuwa watu wa ajabu kiasi gani kuwakabidhi nchi watu waliogawanyika kiasi hiki!?
Maana hakuna tena vya Irani ya Chama kama zamani bali kila mtangaza nia ana irani yake, na tumeona hata kwa awamu iliyotangulia.
 
Huyu kamshindwa Lusinde yule kichaa atawezana na Lowassa kweli kwa mziki tuliouona jana! Hii ngoma ya magamba lazima ipasuke mwaka huu. Naona karata pekee waliyonayo wapambe wa Membe ni kumkata jina Lowassa kabla hajafika mbali, sidhani kama atakubali kwa nilivyoona jana

ukweli ni bora kabisa cc ya ccm ikalikata jina la EL mapema maana inaonyesha kama vile waTZ wote tuko mazuzu. inawezekanaje kweli fisadi badala ya kwenda mahakamani sisi tunamshangilie aende ikulu? huu uzuzu kweli tunahitaji mtu wa nje kutufungua akili?
 
kuwa kambi la lowasa ni kuwa msaliti? ila kuwa kambi ya membe au wassira ndio SIO usaliti?! sielewi vile!

Kuwa kambi ya lowasa ni usaliti kwa wa TZ. Ni juzi tu tulishangilia anajiuzuru kwa aibu kwa kashfa ya RICHMOND na tumekuwa tunaishutumu Serikali ya JK na vyombo vyake kwa kutokumfikisha mahakamani. Leo ni chombo gani kimemsafisha na kumuona msafi na anastahili sio tu kuwa Rais bali hata kuwa mgombea?

Hivi hatuoni kama tunajitia aibu waTZ kushabikia uchafu na watu wachafu kuwaona ndio mashujaa?

Tubadirike jamani, mustakabali wa hii nchi uko vichwani mwetu, tukijitia hamnazo tunaununua utumwa wenyewe
 
View attachment 255993
Mwanasiasa mkongwe wa CCM mzee John Malecela amemshangaa mzee Kingunge na kumuita Yuda na msaliti, ndumilakuwili na mchochezi na hana shukrani hakumbuki alichofanyiwa na serikali ya Kikwete huyu Kingunge.

Anakusanya ushuru stendi ya Ubungo na maeneo mengine ya mji hela anazokusanya kila siku anampa nani au aliwashawahi kutoa msaada wowote kwenye kituo cha kulea watoto yatima? Mzee Malecela amesema Kingunge aache kabisa kuwachagulia mtu anayefaa kuwa Rais kazi hiyo ipo mikononi mwa CCM kwenye mkutano mkuu hata CHADEMA, CUF hufanya hivyo kwenye vikao vyao maalumu.

Mzee Malecela amesema kura ya veto iliyomtoa manyoya yeye wakati anagombea Urais ndio itakayotumika kuangalia mgombea mwenye Sifa zote zinazohitajika kwa Tanzania ya sasa na nyingine pia awe msafi, mpole, mchana Mungu mwenye maadili.

Malecela amesema Rais hawezi kupatikana kwa kelele za watu, porojo na maigizo; muda ukifika kila Mgombea atabeba msalaba wake.

Kwa matendo waliyoyafanya kugawa watu kwa kuwanunua kwa uchu wa madaraka, mbegu hiyo ni mbaya sana kwa Taifa kwani kuna uwezekano Taifa lilitagawanyika tusipokuwa makini na wasaka urais kwa nguvu.

Kama ni KWELI basi huyu mzee malecela HAFAI kuishauri CCM. Kama anajua huyu mzee Kingunge anakusanya pesa bila hata kulipa ushuru nk kwan nini hajawahi KULISEMA au kulikemea? Huyu ni mnafiki kabisa na ana visa kwani yeye alinyamazishwa kwa kutokuwa na uadalifu!
 
..ccm adui yao ni wao wenyewe....watanyukana mpaka kieleweke...maana anguko lao ndio hivyo laja....hawaoni wala hawasikii.....wao wamekalia rushwa na ubinafsi...ndio maana maigizo yao sasa wala siyashangai....maana najua fika hili ndilo anguko lao.....watamalizana wao wenyewe kwa wenyewe....
 
CCM watu wa ajabu sana,mbona mnanyukana wenyewe kwa wenyewe?busara iko wapi?itoshe tu kwa mgombea kutoa sera zake na kutangaza nia,acheni kutupiana mawe mchana kweupe,ndio kusema hata UKAWA wanaweza kutupiana mawe?Ni vyema kila mmoja akatangaza sera zake halafu mviachie vikao vya chama viamue nani anafaa,muungwana anakuwa na akiba ya maneno,kama mnaumbuana wenyewe kwa wenyewe hamuoni mnawarahisishia UKAWA kazi?Labda mnapigwa upofu au ndio mambo ya mnara wa Babel,tatizo ni urais tu?Rais ni mmoja tu,hamuwezi kuwa marais wote,hilo mkubali.
 
CCM watu wa ajabu sana,mbona mnanyukana wenyewe kwa wenyewe?busara iko wapi?itoshe tu kwa mgombea kutoa sera zake na kutangaza nia,acheni kutupiana mawe mchana kweupe,ndio kusema hata UKAWA wanaweza kutupiana mawe?Ni vyema kila mmoja akatangaza sera zake halafu mviachie vikao vya chama viamue nani anafaa,muungwana anakuwa na akiba ya maneno,kama mnaumbuana wenyewe kwa wenyewe hamuoni mnawarahisishia UKAWA kazi?Labda mnapigwa upofu au ndio mambo ya mnara wa Babel,tatizo ni urais tu?Rais ni mmoja tu,hamuwezi kuwa marais wote,hilo mkubali.

Wakinyukana wewe kinakuuma nini?
 
well said,kingunge hana hadhi ya kutushawishi kiongozi anayetufaa.kwani kipindi chote cha uongozi hajawahi kushauri maswala na changamoto yoyote tulizowahi kukabiliana kama taifa .hakutumia busara au hekima za uzee ila katika ili la umoja wa kifisadi,muungano wa majambazi anashauri kumkumbatia huyu mamvi.zingatia maslahi ya taifa babu .ulitegemewa baada ya kifo cha baba wa taifa utafaa hata kwa asilimia chache ukatuangusha ukashindwa kuwa jasiri.ujasiri umeupata wapi leokama si ujasiri wa rushwa/ufisadi
 
Teeeeh,teeeeh,teeeeh,vita yapanzi faraja ya kunguru kwani hujipatia msosi ki ulaini,hivyo ukawa wawe tayari kukabidhiwa injhiii

Kabisa mkuu, ukawa njia nyeupeeeee, kiulaini. Kama kusukuma mlevi yaani.
 
Huyu kamshindwa Lusinde yule kichaa atawezana na Lowassa kweli kwa mziki tuliouona jana! Hii ngoma ya magamba lazima ipasuke mwaka huu. Naona karata pekee waliyonayo wapambe wa Membe ni kumkata jina Lowassa kabla hajafika mbali, sidhani kama atakubali kwa nilivyoona jana
hAKUNA MUZIKI WOWOTE HIYO JANA. Watu wote pale walipelekwa kwa hela, posho, nauli kama ana muziki wowote aende bila kuwalipa watu tuone kama atapata watu
 
Huyu Mzee mwaka 1995, 2005 alitumia fedha kibao na zote zililiwa .. finali uzeeni sasa .. Membe hawezi kuwa Rais wa nchi hii ... hana mvuto, si mtendaji ...
 
Back
Top Bottom