Malecela: Kingunge hana shukrani

Malecela: Kingunge hana shukrani

View attachment 255993
Mwanasiasa mkongwe wa CCM mzee John Malecela amemshangaa mzee Kingunge na kumuita Yuda na msaliti, ndumilakuwili na mchochezi na hana shukrani hakumbuki alichofanyiwa na serikali ya Kikwete huyu Kingunge.

Anakusanya ushuru stendi ya Ubungo na maeneo mengine ya mji hela anazokusanya kila siku anampa nani au aliwashawahi kutoa msaada wowote kwenye kituo cha kulea watoto yatima? Mzee Malecela amesema Kingunge aache kabisa kuwachagulia mtu anayefaa kuwa Rais kazi hiyo ipo mikononi mwa CCM kwenye mkutano mkuu hata CHADEMA, CUF hufanya hivyo kwenye vikao vyao maalumu.

Mzee Malecela amesema kura ya veto iliyomtoa manyoya yeye wakati anagombea Urais ndio itakayotumika kuangalia mgombea mwenye Sifa zote zinazohitajika kwa Tanzania ya sasa na nyingine pia awe msafi, mpole, mchana Mungu mwenye maadili.

Malecela amesema Rais hawezi kupatikana kwa kelele za watu, porojo na maigizo; muda ukifika kila Mgombea atabeba msalaba wake.

Kwa matendo waliyoyafanya kugawa watu kwa kuwanunua kwa uchu wa madaraka, mbegu hiyo ni mbaya sana kwa Taifa kwani kuna uwezekano Taifa lilitagawanyika tusipokuwa makini na wasaka urais kwa nguvu.
Kingunge ni janga ndani ya CCM.
 
ccm anamwita ccm mwenzie adui!? huu mwaka ni wetu makamanda big up Dr. Slaa
 
Sasa sana Mzee malecela nakubaliana na hoja yako,kwa mtu kama Mzee kingunge kupanda kwenye jukwaa la lowasa nitatizo kwa ccm na kwake mwenyewe maana anadai yeye ni muumini wa ukomonisti sasa iweje apande kwenye jukwaa la ubepari ama Mzee kingunge amebadili muelekeo nakuwa bepari wazwaz maana tunajua kama yeye ni bepari wakujificha kupitia familia yake aibu itakukuta Mzee kingunge
 
huyu mzee alishindwa na yule kichaa mwenye IQ sawa na dental formula ya kuku..
 
huyu mzee alishindwa na yule kichaa mwenye IQ sawa na dental formula ya kuku..genetic factor haiongopi,akili mbovu kamrithisha bonge le mutuz.
 
kuwa kambi la lowasa ni kuwa msaliti? ila kuwa kambi ya membe au wassira ndio SIO usaliti?! sielewi vile!
 
Kila mtu CCM ni opportunists tu. Hakuna cha maana.
 
View attachment 255993
Mwanasiasa mkongwe wa CCM mzee John Malecela amemshangaa mzee Kingunge na kumuita Yuda na msaliti, ndumilakuwili na mchochezi na hana shukrani hakumbuki alichofanyiwa na serikali ya Kikwete huyu Kingunge.

Anakusanya ushuru stendi ya Ubungo na maeneo mengine ya mji hela anazokusanya kila siku anampa nani au aliwashawahi kutoa msaada wowote kwenye kituo cha kulea watoto yatima? Mzee Malecela amesema Kingunge aache kabisa kuwachagulia mtu anayefaa kuwa Rais kazi hiyo ipo mikononi mwa CCM kwenye mkutano mkuu hata CHADEMA, CUF hufanya hivyo kwenye vikao vyao maalumu.

Mzee Malecela amesema kura ya veto iliyomtoa manyoya yeye wakati anagombea Urais ndio itakayotumika kuangalia mgombea mwenye Sifa zote zinazohitajika kwa Tanzania ya sasa na nyingine pia awe msafi, mpole, mchana Mungu mwenye maadili.

Malecela amesema Rais hawezi kupatikana kwa kelele za watu, porojo na maigizo; muda ukifika kila Mgombea atabeba msalaba wake.

Kwa matendo waliyoyafanya kugawa watu kwa kuwanunua kwa uchu wa madaraka, mbegu hiyo ni mbaya sana kwa Taifa kwani kuna uwezekano Taifa lilitagawanyika tusipokuwa makini na wasaka urais kwa nguvu.

Hapo nanyamaza umri wangu ni mdogo sana
 
Wakati wa sakata la Escrow, profesa Anna Tibaijuka alinukuliwa akisema, 10M zilikua hela zake za mboga, tulipokua tunafanya digest ya hiyo statement hapa kazini kwetu niliwaambia hivi wenzangu; "Wakati wa kinyang'anyilo cha kumpata mgombea form ccm, tutajua nani hasa anaeongoza kupiga pesa za nchi hi, hiyo statement ya huyo mama haijatoka tu hiv hivi, anayo siri Fulani moyoni mwake, tusubiri" Wameisha anza kuumbuana, si tayari mzee malecela kasha sema hapo, kumbe pesa za Ubungo terminal hua zinaingia mfukoni mwa mtu na sio serikalini; halafu kucha kutwa, watu wanaenda kuomba msaada nje ya nchi na pesa tunaziacha hapa hapa, bado kidogo tutamjua na anae miliki Car parking system za miji yote mikubwa nchi hi. Ya Kakobe naona yanaanza kutimia mdogo mdogo
 
Sasa hawana pa kujificha zaidi ya kukiri kwamba CHADEMA NI KISMA CHA FIKRA NA NDIO NYOTA INAYOONGOZA NJIA.

Chadema wangekuwa ni dira wangeshindwa kutangaza mgombea hadi Leo? They are nothing other than Makuwadi wa Mafisadi wa CCM.
 
Wewe umejitahidi kuchambua hao watatu yaani mwigulu, nyerere na pinda atleast ndani ya hicho chama ndo hawajachafuka na ingawa mi siyo mwanachama kama ningepewa nafasi ya kupendekeza jina moja Kati ya hao basi ni mwigulu japo inabidi apunguze ukada anapoongoza nchi! Pamoja na hayo kuna swali gumu kwamba je akipita na kuwa Rais atakuwa huru kutekeleza anayosema au atafuata chama? Nikifika hapo basi huwa sioni sababu ya kuchagua mgombea yeyote ndani ya chama hicho.
 
tungekuwa na wazee wengi waliostaafu wenye kujitoa na kukemea uovu unafanywa na waliopo kwenye madaraka nchi ingepona. lakini vizee vingi viko kama kingunge, nimekuwa visaka tonge. Havina misimamo na vinachangia kuitumbukiza nchi kwenye dimbwi la maafa
 
Mwaka huu magamba mnakazi Ukawa wakiwakosa basi it will take twenty years kurudisha hari kwa Watanzania.
 
Back
Top Bottom