mzenjiboy
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 907
- 387
Waziri Mkuu wa Malaysia punde hivi ameihakikishia dunia ya kuwa ndege yao imeangukia katika bahari ya Hindi, hii ni kwa mujibu wa experts wa satellite.
=============================================
=============================================
Ndege ya Malaysia MH320 ilitoweka ikiwa na abiria 239 baada ya kuruka kutoka uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur tarehe 8 mwezi huu.
Aidha tangazo hilo limekuja huku juhudi za kutafuta mabaki ya ndege hiyo Kusini mwa Bara Hindi zikimalizika kwa siku ya tano bila mafaniko.
Waziri mkuu wa Malaysia amesema kuwa ndege hiyo ilianguka Kusini mwa Bahari Hindi, bila ya manusura wowote.
Aliambia waandishi wa bahari kuwa udadisi uliofanyiwa data ya Satelite kutoka Uingereza ndio umewathibitishia kwamba ndege hiyo ilimalizia safari yake Magharibi mwa mji wa Perth mbali na eneo lolote la kutua.
Ameomba vyombo vya habari kuheshimu familia za watu waliokuwa ndani ya ndenge hiyo, akisema kuwa anasikitishwa sana kwani kipindi chote walichosubiri taarifa njema , mwishowe imekuja kuwa taarifa mbaya hata zaidi.
Ndege ya Malaysia MH-370, ilipoteza mawasiliano wiki mbili zilizopita na meli za nchi mbali mbali pamoja na ndege zimekuwa zikitafuta angalau mabaki ya ndege hiyo bila ya kupata chochote.
chanzo:http://www.bbc.co.uk/swahili/habari/2014/03/140324_malaysia_.shtml
"They have told us all lives are lost," relative of missing passenger tells CNN Malaysia Airlines Flight 370 went down over the southern Indian Ocean An Australian aircraft spots two objects: one circular, the other rectangular Earlier, a Chinese plane saw "two relatively big floating objects," Xinhua reports.
Source:CNN