Malalamiko ya Malofa kwa Papal Nuncio

Malalamiko ya Malofa kwa Papal Nuncio

Ni takribani siku nne, kumekuwa na mjadala mzito umeibuka baada ya taarifa kuwa vijana wawili wanaodai kuandika barua ya malalamiko kwa Balozi wa Vatican (Papal Nuncio), Archbishop Angelo Accatino wakimshtaki Padre Charles Kitima. Tukio hili limeibua maswali makubwa si tu juu ya madai yenyewe, bali zaidi juu ya uelewa mdogo wa taratibu na mchakato rasmi wa Kanisa Katoliki la Roma katika kushughulikia tuhuma za mwenendo mbaya wa makasisi na watumishi wake.
View attachment 3521377
Kanisa Katoliki haswa la Roma, ni moja ya sehemu zenye utofauti mkubwa sana na taasisi za kisiasa au majukwaa ya kijamii, haliongozwi kwa makelele ya televisheni, Instagram, Facebook au TikTok, hotuba za kinafiki au malalamiko ya maneno ya kuongea vijiweni.
View attachment 3521378
Vatican haisikilizi malalamiko ambayo ni “verbal”, wala haifanyi maamuzi kwa misingi ya presha ya vyombo vya habari, hata kituo kama EWTN ambacjo ndio chombo kinachorusha taarifa za kikatoliki bado huwa kinakula za kichwa wakienda vibaya. Kanisa Katoliki lina utaratibu wa kisheria (canon law) unaohitaji nidhamu, utambulisho, na ushahidi sio porojo.
View attachment 3521382
Tatizo la msingi kwa vijana hawa wawili, Stanslaus Nyakunga pamoja na mwenzake Elia Phaustine linaonekana kuwa ni kutokuelewa kabisa nani anaandika, kwa nani, na kwa msingi upi.
View attachment 3521381
Barua yoyote inayokwenda kwa Papal Nuncio lazima ianze kwa kujitambulisha kikamilifu: jina kamili, mawasiliano, jimbo (diocese) wanakotoka, na parokia (parish).
View attachment 3521377
Lakini pia hata hali yao ya kikanisa—je, wamebatizwa? Je, ni Wakatoliki halali na hai? Kanisa Katoliki haliwezi kushughulikia kwa uzito malalamiko ya mtu ambaye hata hajathibitisha uhusiano wake wa kimsingi na Kanisa lenyewe au Makandokando?
View attachment 3521379
Wakatoliki wanaelewa vyema, fuatilia maziko ya mkatoliki halisi na mtu ambaye sio mhuni utaelewa. Lakini pia je mmepata ushauri kutoka kwa Viongozi wa VIWAWA katika parokia zenu mkiwa kama vijana wa kanisa?
View attachment 3521389
Ni muhimu kusisitiza jambo moja linalopuuzwa sana: kuvaa Rozari shingoni hakumfanyi mtu awe Mkatoliki. Ni wazi kuwa rozari takatifu ni chombo cha sala, ila si kitambulisho cha imani ya mtu.
View attachment 3521390
Ukatoliki halisi unatambuliwa kwa sakramenti, hasa sakramenti ya ubatizo, pamoja na Ekaristi takatifu. Bila uthibitisho wa hilo, mlalamikaji anabaki kuwa ni makandokando tu, mtu mzushi anayetoa maoni kwa Mama Kanisa pasipo kuhusika moja kwa moja na Kanisa.
View attachment 3521384
Ukiachana na Roman Catholic kuna wale wa wakatoliki wa Mashariki kama, Maronite , Melkite, Syro-Malabar, pamoja na Syro-Malankara ambao wote hawa wanatumia Rosari takatifu kwenye kusali. Hivyo suala la Stanslaus na mwenzake Elia kuvaa rozari sio kigezo kuwa ni wakatoliki.
View attachment 3521377
Zaidi ya hapo, mchakato wa Kanisa ni wa ngazi. Malalamiko dhidi ya padre huanza kwa askofu wa jimbo husika. Mfano, kama wakatoliki wanaosali Parokia ya Moyo Mtakatifu wa Yesu, wna wasiwasi na Padri Stephen Mvili, basi wanaanza kupeleka malalamiko yao kwa Askofu Mhashamu Romanus Mihali.
View attachment 3521385
Kama askofu anahusika au ameshindwa kuchukua hatua, ndipo malalamiko yanaweza kupelekwa kwa ngazi ya juu zaidi—ikiwemo Papal Nuncio. Kuruka hatua hizi bila sababu nzito ni sawa na kujaribu kukata rufaa bila kesi ya awali.
View attachment 3521382
Barua ya malalamiko pia haiandikwi kwa lugha ya jazba, kejeli au lawama za jumla. Vatican inahitaji taarifa za ukweli: tarehe, mahali, matukio mahsusi, mashahidi kama wapo, na ushahidi wowote unaoweza kuthibitishwa. Maneno ya “inasemekana”, “nilisikia fulani akisema” au “kijiwe fulani cha kahawa wanasema” hayana uzito wowote katika mfumo wa Kanisa Katoliki.
View attachment 3521387
Kimsingi, kilichojitokeza hapa ni funzo pana kwa waumini na jamii kwa ujumla: Kanisa Katoliki ni taasisi ya karne nyingi yenye taratibu zake, si jukwaa la mitandao ya kijamii.
View attachment 3521388
Haki ndani ya Kanisa haipatikani kwa makelele, bali kwa kufuata njia na utaratibu. Bila hivyo, hata malalamiko ya kweli yanaweza kupotea njiani—si kwa sababu hayana msingi, bali kwa sababu hayakuwasilishwa kwa namna iliyo rasmi.
View attachment 3521387
Mwisho, sauti ya waumini ni muhimu, lakini sauti hiyo lazima iambatane na nidhamu, utambulisho na ukweli. Bila hivyo, barua yoyote, hata ikifika Vatican, inaweza kubaki kuwa karatasi tu isiyo na uzito wa kisheria wala wa kichungaji.
View attachment 3521386
Ila nina imani kabsa kuwa Stanslaus na mwenzake Elia sio waumini wa Kanisa la Roman Catholic, nina uhakika wa 100%, wangekuwa wakatoliki wangefahamu namna ya kuwasilisha malalamiko yao bila kuita press za kipuuzi.
View attachment 3521383
Kwa muktadha huu ilikuwa ni halali kabsa na busara kwa Archbishop Jude Thaddeus Rwai’chi OFMCap kusema kuwa hawa ni Malofa.
Hata attention wanayopewa hao malofa hawaistahili. It’s a waste of time!
 
Ben Saanane, Soka, Mdude na Polepole wako wapi??
Hapo umeorodhesha
Nani aliwateka? Leta fact na ushahidi usiokuwa na shaka ili sasa tuungane kuwapinga hao watekaji
Mfano useme kuwa polepole alitekwa na fulani na ushahid wa huyo mtekaji ni huu!
Mbna simple tu?
 
Hapo umeorodhesha
Nani aliwateka? Leta fact na ushahidi usiokuwa na shaka ili sasa tuungane kuwapinga hao watekaji
Mfano useme kuwa polepole alitekwa na fulani na ushahid wa huyo mtekaji ni huu!
Mbna simple tu?
Wekeni tume huru ya uchunguzi mletewe ushahidi wote.
 
Hapo umeorodhesha
Nani aliwateka? Leta fact na ushahidi usiokuwa na shaka ili sasa tuungane kuwapinga hao watekaji
Mfano useme kuwa polepole alitekwa na fulani na ushahid wa huyo mtekaji ni huu!
Mbna simple tu?
Hivi huwa mnapata wapi ujasiri wa kupinga mambo yaliyo wazi ipo siku tutazitafuta hizi ID zenu kwenye majina halisi tumalizane mtaani..
 
Hivi huwa mnapata wapi ujasiri wa kupinga mambo yaliyo wazi ipo siku tutazitafuta hizi ID zenu kwenye majina halisi tumalizane mtaani..
Umefanya nimecheka kwa sauti 😃
 
Hao ni Malofalofa kweli, yamenunua rozari za buku mbili yakaenda kuandika barua isiyo na mantiki eti tunamwandikia Pappa, Shenzi nyinyi huyo Pappa ana mambo million ya kushughulika nayo. Usikute hajui km kuna huyo mmemshitaki kama anaexist.
Mishamba na malofa nyinyi tafuteni kazi ngumbaru nyie.
 
Hivi huwa mnapata wapi ujasiri wa kupinga mambo yaliyo wazi ipo siku tutazitafuta hizi ID zenu kwenye majina halisi tumalizane mtaani..
Huwa nawambia kila siku humu jina langu halisi ni KERATO MOMBAA na kuna members humu wananifahamu halisi. sina jina feki, napatkana hapa dar es salaam, nasali kanisa kuu anglican la mtakatifu albano alilokuwa anasali jaji mkuu mstaaf augostino ramadhani, njoo hata leo utanikuta nipo hapa kwa jina hlo au unataka nikwamby ninapoishi ili uje?
MIMI SIWEZI JIFICHA, VP UNATAKA UNITAFUTE AU NIKUSAIDIE KUNITAFUTA? AU TUPEANE MAWASILIANO AU NAMBA YA NIDA?
 
Hao ni Malofalofa kweli, yamenunua rozari za buku mbili yakaenda kuandika barua isiyo na mantiki eti tunamwandikia Pappa, Shenzi nyinyi huyo Pappa ana mambo million ya kushughulika nayo. Usikute hajui km kuna huyo mmemshitaki kama anaexist.
Mishamba na malofa nyinyi tafuteni kazi ngumbaru nyie.
Lofa mwingine kaulizwa anasali parokia gani, yeye kaanza kutoa historia ya Mtakatifu kuanzia alivyopata kuitwa mwenye heri mpaka Mtakatifu 😃 Kitendo cha kusema nasali parokia ya Mtakatifu Bakhita yeye kaanza kuleta stori 😃
 
Back
Top Bottom