Ndugu zangu wana jamii f.Tarehe 27/11/2014 niliweka vocha ya sh 3500 kwenye simu na kisha kujiunga na kifurushi cha wiki cha 3500 lakini paka leo hawajanipa huduma hiyo nimewapigia mara 2 wakiniambia subiri kidogo wanakata simu baada ya hapo napiga simu nasubiliwa kuunganishwa kwa muda wa dk 19 na sek 38 na bila kuunganishwae.Nahisi hawa jamaa wa tigo kuna kamchezo wanacheza kawizi wizi,nilishawahi kusikia tabia yao hii kwa mtu mwingine sasa imenitokea mwenyewe,sisemi muache kutumia tigo la hasha ila Nawashahuri wadau kuweni makin na mtandao huu. hii pesa lazima warudishe hata kama itanigharimu zaidi
akanijibu kama huwezi matumizi ya hiya simu nunua simu za bei rahisi..akanikatia ni simu..aisee I was so much disappointed especially majibu ya yule kaka. . .imagine we ni mteja unaibiwa hela zako afu unapewa majibu kama hayo na wahusika..nilichogundua inawezekana kuna MB na dakika zetu tunaibiwa sana kwenye mitandao ya simu ili tununue tena..natamani hata kuhama mtandao ila nahofia nitapoteza watu wangu wa muhimu.
Nimeamka Leo Asubuhi Mida Hii Nikaangalia Salio Langu.Nikakutana Na Ujumbe Mzuri Kabisa JIACHIE NA SMS ZA BURE MITANDAO YOTE KILA SIKU .HAKUNA KUJIUNGA ,MWAMBIE NA MWENZIO. Basi nikaamua kutuma message lakini cha ajabu SALIO LANGU LIMEKATWA.Nimesikitika Sana Kwa Kweli.Hivi Nyie Mtandao Wa Tigo Kwa Nini Mnadanganya Wateja Wenu?