Malalamiko: Tigo Tanzania

Hao no wabahitishaji sana,mimi nimeshindwa kabisa kuwapigia watu wenye namba za tigo toka nje. Wataacha niachwe na mke maana wamenisababishia matatizo makubwa.
 
Ndugu zangu wana jamii f.Tarehe 27/11/2014 niliweka vocha ya sh 3500 kwenye simu na kisha kujiunga na kifurushi cha wiki cha 3500 lakini paka leo hawajanipa huduma hiyo nimewapigia mara 2 wakiniambia subiri kidogo wanakata simu baada ya hapo napiga simu nasubiliwa kuunganishwa kwa muda wa dk 19 na sek 38 na bila kuunganishwae.Nahisi hawa jamaa wa tigo kuna kamchezo wanacheza kawizi wizi,nilishawahi kusikia tabia yao hii kwa mtu mwingine sasa imenitokea mwenyewe,sisemi muache kutumia tigo la hasha ila Nawashahuri wadau kuweni makin na mtandao huu. hii pesa lazima warudishe hata kama itanigharimu zaidi

Mkuu haya makampuni ya simu ni zaidi ya Escrow ila hakuna cha kufanya naona sirikali wamewapa baraka zote.
 
Kweli tigo ni wezi kabisa mi nilishangaa siku moja nimekatwa hela yangu eti nimejiunga na ujumbe wa mahabati cjui, yaani nilichukia hamna mfano at this age mi mambo ya mahabati ya nini?na sijajiunga na siwezi jiunga na huduma ya kidwanzi hivyo. Sasa hivi wananitumia msg nikaunganishwe postpaid kwakuwa matumizi yangu ni makubwa na siendi ng'o maana huko ndio nitaibiwa zaidi.
 
Pumbaff sana eti wanakuambia zima simu toa line hii ni akili au matope kabisaa mtu mzima mnamdanganya mchana kweupeeee
 
Mimi pia nimekua victim wa Tigo.. nilijiunga kifurushi cha elf29 kwa mwezi,ambacho ndo huwa natumia mara zote..nilijiunga tarehe 25/10..kufikia tarehe 11/11 nikajikuta siwezi kutumia internet MB 800 zimeisha!!!nikashangaa kwasababu sina matumizi makubwa ya internet zaidi ya kubrowse mitandaoni mara chache..ila nikasema pengine kweli matumizi yangu yalikua makubwa..nikajiunga tena kifurushi cha elf29 tarehe hiyo 11 jioni, kufika tarehe 15 nikashangaa tena wananiambia sina kifurushi cha internet
!!!!nilishangaa kwasababu huwa sidownload wala kufanya matumizi makubwa ya internet..Nikaamua kupiga simu customer care,akapokea kaka mmoja,kumueleza shida yangu akaniambia ndo matumizi yako yamemaliza MB..nikamwambia sijafanya matumizi extra zaidi ya ya siku zote na how come kifurushi cha mwezi kiishe chini ya siku5?? akauliza unatumia simu aina gani?nikamwambia S5..Akasema S5 inamatumizi makubwa ya internet..Nikauliza kwanini isiwe siku zote iwe mwezi huu tuu??akanijibu kama huwezi matumizi ya hiya simu nunua simu za bei rahisi..akanikatia ni simu..aisee I was so much disappointed especially majibu ya yule kaka. . .imagine we ni mteja unaibiwa hela zako afu unapewa majibu kama hayo na wahusika..nilichogundua inawezekana kuna MB na dakika zetu tunaibiwa sana kwenye mitandao ya simu ili tununue tena..natamani hata kuhama mtandao ila nahofia nitapoteza watu wangu wa muhimu.
 
wakuu m mwenyewe niliambiwa nitume namba yangu kwenye ukurasa wao wa fb,cha ajabu hadi leo hawajanijibu kitu,ila Kwa kuwa kazi yangu uniwezesha kuonana na viongozi wetu hususani wabunge na kwa kuwa hiki kimekuwa kilio kikubwa kwa watanzania ntajaribu kufikisha ombi hili kwao tuone wao wakiwa kama waakilishi wetu watatusaidiaje? maana m vocha yangu hadi leo sijui hatima yake ila meseji zao za promosheni wananitumia kama kawaida hawa pap watoto ila mitandao ya simu kaeni mkijua wananchi tumewachoka dawa yenu tunaichemsha.Sasa na nyie mtafutiwa namna ya kushtakiwa ili muhimili wenu usiingiliwE
 
hakuna mtandao wenye afadhali.... voda ndo nuksi.. airtel kwa walio mikoani maeneo mengi hawajafunga 3G....
 
akanijibu kama huwezi matumizi ya hiya simu nunua simu za bei rahisi..akanikatia ni simu..aisee I was so much disappointed especially majibu ya yule kaka. . .imagine we ni mteja unaibiwa hela zako afu unapewa majibu kama hayo na wahusika..nilichogundua inawezekana kuna MB na dakika zetu tunaibiwa sana kwenye mitandao ya simu ili tununue tena..natamani hata kuhama mtandao ila nahofia nitapoteza watu wangu wa muhimu.

Huyo aliekujibu hivyo ajichanganye siku aniropokee, nitamjazia fomu ya likizo kabisa nimtafute anijibu live.
Uzuri huwa wanajitambulisha mapema na wengine huwa wanajisahaulisha mie huwa nauliza vizuri ili nikipiga tena narejea maelekezo ya fulani.

Kuibiwa MB TUNAIBIWA SANA TU , kuwashikisha adabu tunaweza tukidhamiria lwa dhati.
 
Yaani jinsi navyoudharau huh mtandao. Kwanza cm yake ni Nokia tochi , pili naweka vocha kiwango cha juu ni 2000 , najiunga zile dakika za tsh 999 two days. Baada ya hapo nakaa hata siku NNE au tano mwenye kupiga apige ila Mie mmmmh . Siwaamini tangu Mwanzo hawa . Sana sana ni Tigo pesa tu Basi. Siwafagilii kabisa
 
Yani kweli kabisa TIGO NI WEZI.
Nimeacha kabisa kujiunga kwa mtindo wa kuongeza salio kwanza.

Kwa sababu mfano nikiweka 5,000 nikajiunga kifurushi cha sh. 3,500 salio linabaki 1,500.

Ila cha ajabu ndani ya masaa yasiyozidi matatu ukiangalia salio hukuti ile 1,500. Unakuta imepungua SANA tu. Inapunguaje hadi kuisha kabisa wakati bado kifurushi chako kipo full?

Nilichoamua huwa najiunga direct toka tigo pesa.
 
mpaka sasa,silazi salio,naweka 500 au 250 kwa njia tigo pesa na kujiunga hapo hapo.ndio dawa yao,nikitaka intanet ya uhakika naweka airtel.nacheza namba zote,tigo nipo kiasi,airtel na voda, kila moja kwa ubora wake.
 
Tigo ni majanga, wanasema ukijiunga na huduma ya usiku unapewa 30 GB lakini nilipojiunga hata 1GB haikuisha internet ikaawahaifunguki. Huu is wizi jamani yaani nimekatisha usingizi wangu bure...
 
Mimi walikula pesa yangu ya tigo pesa mtu alinitumia baada ya siku kama nne nilimpigia jamaa anasema katuma nikiangalia salio hakuwa nikawapigia wakasema liliingia ikanibidi ni dawnlord taarifa zangu za tigo pesa mwezi mzima kuangalia hakuna pesa siku ya hiyo tarehe kuwapigia wasema limeingia mpaka leo hawakanipa pesa yangu
 
Nadhani haiku na haja ya kulalama dawa nikuhama kimya kimya mitandao ipo mingi tz Mwishoe wataona wateja wamepungua wataboresha huduma "hela ya kwako bado unanyanyaswa na huduma"
 
Nimeamka Leo Asubuhi Mida Hii Nikaangalia Salio Langu.Nikakutana Na Ujumbe Mzuri Kabisa JIACHIE NA SMS ZA BURE MITANDAO YOTE KILA SIKU .HAKUNA KUJIUNGA ,MWAMBIE NA MWENZIO. Basi nikaamua kutuma message lakini cha ajabu SALIO LANGU LIMEKATWA.Nimesikitika Sana Kwa Kweli.Hivi Nyie Mtandao Wa Tigo Kwa Nini Mnadanganya Wateja Wenu?
 
HONGERENI TIGO, HONGERENI VODA , HONGERENI PIA ZAIN NA ZANTEL NA MENGINEYO YALIYOPO. Mpokee hongera zangu za maksudi kabisa. Takriban wiki Moja sasa Bundle za Internet za Tiggo zimekuwa zikiyoyoma kwa speed ya jet. ukijiunga baada ya sekunde hamna kitu. si hilo tu bali pia wamekuwa wakikuingizia manyimbonyimbo ya mlio na wanakukata juu kwa juu hata hujui. logwa uandike sms wakati huna salio unafurumshiwa sms nyingi za huna salio hadi inbox inajaa. moja ya shughuli walizotuzawadia watu hawa ni kibarua cha kufuta ma sms taka mengi sana. njoo kwenye Tigopesa au m-pesa, waweza tuma laki ukakatwa 500tu na ukatuma elfu themanini ukakatwa elfu mia mbili. lakini mbali na ushenzzi wote huu bado nawapongeza kwa utu kwa sababu No body control them. Serikali kupitia TCRA Imechapazake usingizi, makampuni haya yanafanya yatakavyo. unaweza kuamini ukijisajili kwenye wimbo wa msanii unakatwa Tsh320, 70%(224) inaishia kwenye makampuni haya, 30%(Tsh96) inakwenda kwenye kampuni mfadhili wa msanii. kwenye kampuni hilo wanakomba 20%(Tsh64) na ten percent ya tsh320 ndo inakwenda kwa msanii yaani Tsh32. lakini bado haitoshi msanii haipati hiyo Tsh32 kamili inaundergoes makato hapo ya Vat,charges mbalimbali hadi mkononi msanii anaambulia Tsh23.5. Kazi za msanii zinapigwa roba ya kufa mtu na hapana anayesema, ashukuru hata kwa hicho kiduchu anacho ambulia wakiamua anaweza pata zero kabisa na nobody complain, nobody cares.

nchi hii mamlaka zenye dhamana na wananchi zimeshagoma kuwatetea watanzania. hongereni makampuni ya cm, lakini fanyeni tu ubinaadam ivoivo tuenedelee hadi tutapopata Rais kwenye nchi hii
 
Nimeamka Leo Asubuhi Mida Hii Nikaangalia Salio Langu.Nikakutana Na Ujumbe Mzuri Kabisa JIACHIE NA SMS ZA BURE MITANDAO YOTE KILA SIKU .HAKUNA KUJIUNGA ,MWAMBIE NA MWENZIO. Basi nikaamua kutuma message lakini cha ajabu SALIO LANGU LIMEKATWA.Nimesikitika Sana Kwa Kweli.Hivi Nyie Mtandao Wa Tigo Kwa Nini Mnadanganya Wateja Wenu?


Hawa jamaaa yani ni majambazi ya mchana kweupe yan kwa kweli hiiii nchi hiiii basi tu
 
Sijajua TCRA wanasubiri watu waende ofisini kwao wapeleke karatasi ndio wajue kuwa ni malalamiko?
hawa watu wanaolalamika hapa wanaweza kuwa contacted na kusaidia uchunguzi ili kujua mbivu na mbichi

Maskini Tanzania …
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom