Makwapa yawe safi jamani

Makwapa yawe safi jamani

Wewe utakuwa unapanda daladala na wasaka nyoka au wale Wakurya wa Kipunguni wanaowahisha mayai K'koo...

Hebu pita kwenye mablog ya wadada wenzako kina Dina uone namna wadada wenzako wanavyoweweseka kutafuta tiba ya kuzuia kiharufu beberu cha kwapa...

Kutwa mwajisugua na makoko ya ugali au kama haitoshi mkienda kwa mangi gengeni kutwa mwamaliza malimao na ndimu kwa sababu ya kwenda lipiga swaki kwapa...

Ebu usinivunje mbavu mie...wewe unachogomea ni nini, kuwa wanaume hili haliwahusu? Kipi nafuu, kwapa lililo safi though jeusi au kwapa lililofugwa afro?
 
Msikariri mambo, Unaweza ukawa nayo na isiwe tabu.
Kuwa 'nahiyo-makitu' Ni swala moja na kuwa Msafi
(Kwa maana ya kutokuwa na maharufu ya ajabujabu swala lingine kabisa)
Hata Marekani na Ulaya kipindi flani (90's) na hata baadhi sasa, Hiyo ni fasheni kabisa na Mabrazamen hawaoni soni kuyaonyesha kabisa hayo Manyoya ya kwapa.
Tatizo: Unayatunzaje,unasafishaje jumlisha na hali ya hewa ya kitropiki tulionayo ambayo inasababisha kutiririsha majasho muda mwingi, Ongezea ukosefu wa sabuni na mafuta sahihi pia Ma-deodorant yanayoendana na hali ya hewa yetu.
Lakini mimi binafsi, Sitaki hata kuyaona kwangu wala kwa 'Waziri mkuu' wangu.
 
hahahaha rafiki bora umewaambia wengne unakuwa nao kwenye daladala wakipanua mikono yao washike chuma la gari hiyo harufu itokayo uko utaomba konda akushuke kituo ambacho hujatarajia kushuka na tabia hiyo ya uchafu wanayo WANAUME huwaga hawajinyoi kabis mpaka kunakuwa kwa njano utadhani wamewekea yai viza, ni vyema bandugu tukawa wasafi jamani

siku hizi kuna dawa za kuondolea vinyweleo kwapani na ni bei poa sana marafiki tununue tuwe wasafi jamani



Usafi wa makwapa muhimu jamani mtu unakuta kawekeza nywele miezi na miezi hata kuzifyeka hamna basi najua wengne ni hurka ya mtu unakuta hawez kukumbuka bas mpenz wake chukua jukumu la kumsaidia kunyoa muwekee na marashi mazuuuri ndio maana wanasema kumtunza mwenzio ni jukumu lako tuepushe majasho na harufu mbaya za makwapa kama unaona uvivu cku iz kuna dawa za kupaka tu kwapani zinatoka zenyewe ni mtazamo Wang jaman
 
Hahahhaaaa jamani Tyta ah mi nilikuwa nina kikombe cha chai pembeni hamu yote imeniisha! Hebu nitoeni ushamba, mbona kuna wanaodai wanaume wakiwa na hii kitu makwapani ndio "sexy"?

You made my Day ...asantee sista!
 
Aise mmenifurahisha sana Leo na makwapa duuuh
 
Back
Top Bottom