Makosa ya Upinzani

Nakubaliana na Mzee Mwanakijiji kwamba kutokana na mlolongo wa matukio yanayotokea nyumbani ni wazi kwamba vyama vyetu vya upinzani vingetumia fursa hii kujiimarisha na kijipambanua kwa wananchi kama vyama mbadala mbavyo vinaweza kutufikisha huko tunakotaka kwenda.

Bahati mbaya kama Zitto alivyogusia hii dhana ya SWOT analysis, inaonekana vyama vyetu vya upinzani mzani wa internal Weakness(udhaifu) umezidi Opportunities(fursa) zilizopo nje ya vyama vyao, kwa mfano katika hali ya kawaida unategemea nini, mwenyekiti wa taifa wa chama cha upinzani anapoitisha mkutano wenye ajenda ya kuwafukuza wanachama!,au kiongozi anapotuhumiwa kwa kufuja pesa za chama!

Mfano mzuri ni NCCR mageuzi historia inaonyesha wazi kwamba umaarufu wake uliporomoka kwa kufukuzana uanachama, TLP, UDP na vingine vingi, vyama vya upinzani mtaji wake ni wanachama, sasa mnapoanza kufukuzana hata imani ya wananchi kwa vyama vya upinzani inapungua kabisa.Kwa hivyo katika hali ya kawaida ni vigumu kuchukua fursa zilizopo wakati ndani ya vyama bado kuna migogoro isiyoisha.

Lakini pia tusiwakatishe tamaa bado wananafasi ya kujifunza, historia ina mengi ya kutufunza,tujifunze best practice from Ghana, Kenya, Rwanda hata Botswana....

Long live Tanzania.
 
Kama mnaziona hizo opportunities, mnawashawishi vipi wananchi kuwa mna uwezo wa kuongoza bila pasipo shaka?

Hata hivyo, Mh Zitto failure comes from within na waswahili wanasema kikulacho ki nguoni mwako. Muuaji wa upinzani ni upinzani wenyewe kuendekeza mambo yanayoipa system uwezo wa kuwafanyia hujuma. Sidhani kama Mrema alikuwa hajui uwezo wa serikali baada ya kutoka nje. Ila ndo hivyo tena ajilaumu mwenyewe

Mrema alijitolea lakini Watanzania mlimsaliti, hii inavunja sana moyo kuona mtu anajitolea halafu anakosa sapoti ya wananchi, nafikiri Mh Zitto yupo sahihi kabisa. Tatizo letu Watanzania ni kukosa focus Uongozi wa nchi sio Chama, chama ni sehemu ambayo mtu hupitia, kinachotakiwa ni yule mtu kuwa na watu wake kama policy makers, strategists, haiitaji sana chama as a whole, RAISI ANAHITAJI WATU WALA SIO CHAMA, kwa hiyo bwana Ndahani lazima ujue hivo vitu, kwani unafikiri Obama anahitaji chama chake ili aiongoze marekani, yeye anasubmit ajenda halafu inadebatiwa, kama inafaa inapita na kama haifai au haina maslahi na maisha ya wamarekani haipiti.

Tanzania kwa sasa hatuhitaji chama, tunahitaji watendaji, hata kama CCM ingekuwa na watendaji waadilifu kusingekuwa na hii shida, lakini kutokana na uozo wa hao watendaji ndo maana tunaona haifai.

So we need commited people then through what window sasa ndo tunataja chama Fulani, halafu ukumbuke kuwa ili chama kionekane kina nguvu ni pale kinaposhika dola, sasa kama hakijawahi kushika dola mtajuaje kuwa ni chama Mbadala, guys lets wake up.
 
Mimi nafikiri vyama vyetu vinashindwa kujitransform kutoka hali ya uanaharakati kuelekea uanasiasa.Hilo tatizo na mimi nanalo maana nimeshindwa kuwaelemisha wananchi ambao nawafikia wajisikie kuwa wao ndio msingi wa muundo wa serikali ndio maana kila vipindi vya uongozi vinapokwisha uchaguzi unafanyika.Nikiwa nimesomea biashara nimeshindwa kuwaelemisha kuwa hakuna kitu kiachitwa fedha ya serikali,bali ni fedha ya walipa kodi.
Kwa kifupi tusilaumu wanasiasa peke yao tunapaswa tujilaumu wenyewe,kwa kila nafsi kutojishughulisha kuboresha mchakato wa kidemokrasia kwenye nchi yetu.
 
Duh, umetupiga sana. Hata hivyo unfairly. Unapoangalia makosa ya kambi ya upinzani ni vema uangalie 'factors' za ndani na za nje. Katika SWOT analysis hizi ni fursa na vitisho. Hapo utaweza kutoa hukumu sahihi kabisa.

Vilevile ni muhimu sana kuangalia historia ya vyama hivi katika muktadha wa historia ya Tanzania na utamaduni wa kisiasa wa Watanzania. Vyama katika nyakati tofauti - kuanzia kina Marando na Bagenda, Mtei na Makani, Fundikira na Kasanga Tumbo na Mapalala na Seif walipoamua kujitoa mhanga na kuanzisha vyama - kumekuwa na hatu kadhaa zimepigwa katika kujenga dmeokrasia ya kweli katika nchi yetu.

Watu wanaiweka Tanzania katika mizania ya nchi nyingine jambo ambalo ni kosa kubwa maana Tanzania inapaswa kupimwa kutokana na historia yake. Zoezi la ujenzi wa Taifa na kuwa na Taifa moja chini ya uongozi mahiri wa Mwalimu lilifanywa katika misingi ya udikteta mkubwa sana na chini ya amri moja ya 'zidumu fikra za mwenyekiti'. Tanzania ikajenga jamii ya watu wanaoheshimu mamlaka bila kuhoji na hata vyama vingi vilipoanzishwa vilionekana ni vya wasaliti. Ni mtu mmoja tu mpaka sasa ambaye alikonga nyoyo za Watanzania na kuaminiwa - Augustino Lyatonga Mrema - lakini naye akavurugwa sana na dola, kuitwa pandikizi na kuondoa kabisa credibility yake katika jamii. Jamii imefanywa kuamini kuwa Mrema ni 'kichaa' na hana sifa ya uongozi. Hii ni kazi iliyopangwa na kutekelezwa kwa ustadi mkubwa kiasi kwamba leo ni watanzania wachache sana ambao wanakumbuka sacrifice ya Mrema katika ujenzi wa demokrasia nchini.

Tusipojifunza na kuelewa historia hii ya vuguvugu la demokrasia Tanzania tutaishia kulaumu watu kila kukicha bila kwenda mbele. CCM itaendelea kutawala na kila baada ya miaka mitano kutakuwa kinatokea chama kina nguvu na baadae kuangushwa, wabunge wenye nguvu na baadae kuangushwa na hata wanasiasa wenye mvuto na baadae kupakwa matope na kunuka.

Demokrasia hulindwa. Viongozi hulindwa zaidi ili kubakia kama alama ya harakati. Raila Odinga aliongoza harakati za mapinduzi Kenya mwaka 1982, akaswekwa lupango kwa miaka zaidi ya tisa na kuishi uhamishoni nchini Norway kwa miaka mingi. Akajiunga na chama cha baba yake mwaka 1992 FORD, kikavunjika na kuwa na FORD-K na FORD-A. Baba yake Mzee Jaramogi alipokufa Raila akataka kunyakua uongozi wa chama, akashindwa na Michael Kijana Wamalwa na Raila akaenda kuanzisha chama chake NDP. Akaivunja NDP na kuingia KANU kuwa Katibu Mkuu na akaipasua KANU vipande 2 na kuanzisha LDP. Akaingiza LDP katika muungano wa NARC na kumpa Kibaki Urais (literally alimpa Urais maana Kibaki alikuwa armchair leader of opposition). Akatoka NARC na kuanzisha ODM-K, akagombana na Kalonzo na kuanzisha ODM na leo ni Waziri Mkuu mwenye nguvu Kenya.
Mchakato wote huu Raila alionekana msaliti, mpenda vyeo na mtu wa vita. Lakini leo huna tena KANU na Raila alipata kuniambia, demokrasia Afrika itaimarika tu iwapo vyama vilivyoleta uhuru vitapasukapasuka na kuondoa ile claim yao ya sisi tulileta uhuru - hii ni claim ya CCM na hata kumkumbatia Mwalimu kama wao.

Lakini tuna kina Raila Tanzania? Mazingira ya kisiasa yanatoa fursa ya kujenga kina Raila?
Unawezaje kupewa dola ilhali vyombo vya dola havikuamini? Maana taifa haliongozwi na siasa tu. Idara za usalama na majeshi zina nafasi kubwa sana katika kuamua mustakabali wa nchi. Wanasiasa wa Tanzania ni mara ngapi tunajenga rappour na watu wa usalama ili angalau kujua wanawaza nini. Hakuna.

Mwanakijiji utaandika mpaka utachoka na kutulaumu mpaka utakasirika. Demokrasia ya Tanzania itajengwa kwa sober approach ya kutazama historia yetu na kujua 'political culture' ya Watanzania. Unatutaka tuchukue fursa inapotokea. Wazo murua kabisa. Lakini capacity ipo wapi? Wapo wap wanaofikiri na kuziona fursa? Wapo wapi watu wanaojenga scenerios na kujiuliza what if?

Tulianza vizuri zoezi la kujenga imani kwa wananchi kupitia Bunge. Tulifanikiwa kupata sizable number ya wabunge wa CCM na kujenga coalition nzuri na kupashana habari. Tukamezwa. Tukajikuta tumewauzia ajenda tukijua kabisa hawatafika nayo mbali.

Ndani ya CCM hivi sana wanachowaza ni nani atakuwa Rais ajaye kati ya Membe na Lowasa. Hakuna ajenda ya Taifa, hakuna vision pale. Lakini wanasiasa wa upinzani tunaimba nyimbo zao hawa mabwana na hata 'opinion makers' kama wewe Mwanakijiji mnaimba nyimbo zao.

Juzi nilisema hapa JF, lets be sober and scan the political situation objectively. Kinachoniumiza kichwa ni kwamba, kuna vijana wachache katika vyombo vyetu vya ulinzi na usalama wamechoka na bickerings za wanasiasa. Watataka ku restore order! Mzee Sarakikya aliiwahi kuniasa kuwa tusiruhusu hali hiyo itokee kwani ikitokea hawatarudi makambini! Ili isitokee kuna haja ya kufikiri vizuri - Ignore CCM

Kuna tofauti sana kati ya wanaopambana field na wanaopambana kwenye makaratasi! Na pia kuna tofauti kati ya wavulana na wanaume!

Hii article ni excellent na genius au msema hovyo kama mimi nachukulia kama dira, lakini wapi
 
Nakubaliana na Mzee Mwanakijiji kwamba kutokana na mlolongo wa matukio yanayotokea nyumbani ni wazi kwamba vyama vyetu vya upinzani vingetumia fursa hii kujiimarisha na kijipambanua kwa wananchi kama vyama mbadala mbavyo vinaweza kutufikisha huko tunakotaka kwenda,bahati mbaya kama Zito alivyogusia hii dhana ya SWOT .

Tatizo ni kuwa ni kwa kiasi gani mnavikubali vyama vya upinzani

Hawa wapinzani ndio kila siku mnawarudisha nyuma na kuwakatisha tamaa.

Intellectuality ya MKJJ ni kuandika article za CCM akina Sofia Simba, kumpa ushauri JK! Hakuna jipya, yaani kama CCM ikiondoka ghafla leo, basi akina MKJJ hawana cha kuandika. MKJJ ni kwa kiasi gani mnawakubali watu kama akina Zitto ni kwa kiasi gani huwa mnawatetea na watu mnaoona kwa makusudi kabisa wanavunja nia zao nzuri!

HAIWEZEKANI NYIE NDIO MNAWAVUNJA MOYO WAPINZANI NA KUIBEBA CCM LEO HII MUULIZE WAPINZANI WANAFANYA NINI!

MKJJ asipoandika kuhusu Lowasa, JK, RA basi ameshamaliza kazi, badili mfumo, badili vita, nakupa changamoto kwa sababu katika watanzania wenye upeo wa kuisaidia nchi YAO NA WEWE UMO, JENERALI, WEWE, LUSEKELO, achana na yule mnafiki wa England anayejifanya "ukijua hujui ndio utajua unajua sijui nini

Nakuandikia waraka huu ili mbadilike nyie kwanza kabla ya kuwashoot hawa wapinzani

Haya wapinzani wenyewe wapo? Akina nani? Akina Mbowe na Mtei? CUF, TLP? Mama yangu! Be honesty jamani

Wewe Zitto anzisha chama chako cha vijana, uwaweke kwa nguvu akina MKJJ, CHADEMA hamna kitu hapo, ZITTO LEO HII UNAWEZA KUANZIHA CHAMA NA IFIKAPO MWAKANI UNAZOA VIJANA WOOOTE, TATIZO VIJANA WAMEJENGWA KWENYE MISINGI YA KUTOAMINI VIONGOZI TENA, kwa hiyo kazi unayo mkuu! Kuwashawishi...

VIsiona ya JF ni nini?? Kama ni ukombozi hao akina FMES , KIbunango, na wana CCM wengine wanafanya nini humu?

Malumbano ya humu ni kuteteana wana CCM, SIPATI PICHA KUONA MKJJ ANASEMA SOFIA SIMBA AJIUZULU WAKATI CCM YOTE NI UOZO. WALA HUTAAMINI KUONA FMES ANAVYOWATETEA AKINA MALECELA WAKATI KAMA MELECELA ANGEKUWA MSAFI ANGEKUWA AMESHAONDOKA CCM!!

Humu ndani mabishano ni mafisadi wa CCM na wale wenye uafadhali!

ACHA CCM waendelee kutawala mpaka tutakapojifunza

peace
 
Nakubali kabisa aliyoyasema mh. Zitto, kila mtu kila sehemu CCM, inapaa CCM, ni matangazo ya bure inayoyapata kuwafikia watanzania, wapinzani imefikia wakati waeleze ni nini watafanya, waseme nini watafanya mazuri kwa tanzania bila hata ya kuzungumzia ccm, sisi ndiyo tutakao chambua baada ya kusikia hizi pande mbili, tatizo kubwa la watu wengi niliongea nao ukiwasikilza wanasema, bora umpe utawala mtu alaiyekula tayari, ukimpa mwenye njaa kwanza atajishibisha.

Yaani haya ya vyama vya upinzania hayana tofauti na ndugu zangu waislam, wao wanakaa misikitini na kuanza kuichambua biblia, sasa kwa mtu kama mimi ambaye biblia naijuwa ningependa kusikia yale ambayo si ya dini yangu hapo ningepata ulinganisho, lakini always sijui ccm mafisadi sioni anayekamatwa wala kufungwa, vyama vya upinzani kweli vijipange.
 
Mzee Mwanakijiji,

nimeona katika Article ya
Dorothy J. Solinger "
ENDING ONE-PARTY DOMINANCE: KOREA, TAIWAN, MEXICO

kuna maneno mazuri kwa nini vyama hivi vya upinzani vinaweza kushika utawala Mwandishi anasema na nukuu:

"These opposition victories should be regarded not simply as the product of a finally freed-up, democratically expressed public will, but as the outcome of a lengthy process of unraveling of single-party domination, first unleashed long before by the decision to allow “limited elections” and then given a critical boost by the perhaps necessary result of those elections, a split in the ruling party"


Wakati ule upinzani ulipoanza katika nchi yetu, Hayati Baba wa Taifa (RIP) aliwahi kulonga kuwa "Wapinzani wa CCM watatoka ndani ya CCM". Kwa wakati huo, yalikuwa ni maneno ya Onyo kwa CCM lakini pia kimtazamo hayakumaanisha taswira mzuri kwa vyama hivyo ambavyo leo hii CCM inajivuna kuwa yenyewe ndio iliyokuza demokrasia nchini. Hivi ni wapi upinzani ungetokea kama sio ndani ya chama kkinachotawala au kilichopo madarakani?....

Kwa nchi zenye siasa za busara kama Marekani, Uingerteza, Ujerumani nk, uwezi kusikia chama kinaitwa chama cha Upinzani, .....Labda muundo wa siasa zetu ndo tatizo, na hili hata kwa mwananchi wa kawaida linampa hofu, ukisikia chama kinaitwa "Cha Upinzani" fikra ya haraka ni kuwa "Kina pingana na maendeleo"

Utakumbuka siku zile za awali za kuzaliwa Upinzani, CCM walipata ushidi kwa kuwa moja ya ITIKADI katika kampeni ilikuwa ni kuwatishia wananchi juu ya uchanga na upinzani kwenye maendeleo kwa vyama vipya....(vyama vya Upinzan). Katika zama zile,ukiwa kwenye chama cha upinzani ilionekana kama "Mumiani" (mnyonya damu enzi zile za miaka ya 70-80) na wanachi waliweza kukuogopa kama ukoma. Hivi ni nane alipaswa kuviimarisha vyama hivi kama sio CCM, hiyo ndio hoja ambayo kwa CCM mpaka leo ni kitendawili?

Binafsi napata tabu sana kutofautisha "Upinzani na Utawala" .......sijui ikitokea CCM haiatapoong'ka madarakani nayo itakuwa Chama cha Upinzani au mfumo utabadilika?

Ukiangalia sasa kwa siasa tunazoendea kwa mfano wa karibu huu wa Kenya na Zimbabwe wa kushirikiana kutawala (coalition Government), utaona kwa haraka kuwa hakuna upinzani hata kidogo katika siasa za nchi zetu, labda upinzani ni pale tu chama chako kinapokuwa nje ya madaraka....nadhani ipo haja ya mfumo wa utawala kuangaliwa upya. wakati katika nchi zetu, serikali shirikishi inachukuliwa kuwa ni dhambi mpaka ilazimishwe, kwa nchi zilizoendelea inachukuliwa kama ni jambo la lazima ili kuleta chachu katika utawala........
 
Ongeeni chochote mnachotaka. Lakini mimi naamini kabisa Nyerere aliunda taifa la makondoo Tanzania.

Haya mengine ni matokeo tu.
 
In a nutshell,we are passive people and our history backs us up.
Where did cowards of the Nguni people run to?
And where did losers in the Bantu succession disputes flee to?
The skulkers of Bantu leaders' harsh control?
Need I say more?


it is our passivity that has fueled the negativity and political immaturity!
 
sasa kama RAIS MTARAJIWA Tanzania ni FREEMAN MBOWE then ujue kuna tatizo Tanzania

sielewi kwa nini CHADEMA hawataki kumpa nafasi ZITTO KABWE

Lakini hiyo nayo ndio demokrasia ya CHADEMA aua UPINZANI
 
Upinzani upo lakini sio kweli kwamba wanatanguliza pesa mbele, matumizi yao katika kujitangaza na kujiimarisha yanahitaji pesa nyingi kuliko vyanzo vyao walivyo navyo. Wamebenwa sawasawa kila mahali, na ni vigumu kumwondoa aliyekalia kigoda unajua, kwa sababu aliye kwenye utawala tayari anazo influence kubwa na nyingi kuliko wewe unayemkosoa.

Ni Daudi tu aliyefanikiwa kumtungua Goliath, naye ni kwa sababu alitumia Jina la Bwana Mungu wake, otherwise asingethubutu. Mpangilio wa siasa za TZ ni complex na ni dume. Wapinzani wanachomekewa wasalama wa Taifa ambao ni CCM damu. Vyombo vya dola na system zote zimeshikiliwa na CCM na hukilinda chama hicho. Kueneza siasa za CCM hutumia mali ya serikali japo chama kina pesa na mali kupindukia ambayo kwa kweli haikuwa ya chama kimoja. Mwente njaa hawezi kupigana na aliyeshiba.

Taratibu wapinzani watajijenga na kuenea hata kama ni kwa mbinde. Mbona CHADEMA wamemudu kusambaa sehemu kubwa nchini huku Bara na CUF kule visiwani? Unajuaje, labda hata hizo opportunities ambazo zingewafaa wapinzani zinapikuliwa na wanaccm wenyewe kiaina tu kutupumbaza wananchi?

Leka
 
sasa kama RAIS MTARAJIWA Tanzania ni FREEMAN MBOWE then ujue kuna tatizo Tanzania

sielewi kwa nini CHADEMA hawataki kumpa nafasi ZITTO KABWE

Lakini hiyo nayo ndio demokrasia ya CHADEMA aua UPINZANI

Mi nilidhani Januari Makamba ndio anapikwa kuwa raisi?
 
Duh, umetupiga sana. Hata hivyo unfairly. Unapoangalia makosa ya kambi ya upinzani ni vema uangalie 'factors' za ndani na za nje. Katika SWOT analysis hizi ni fursa na vitisho. Hapo utaweza kutoa hukumu sahihi kabisa.

Vilevile ni muhimu sana kuangalia historia ya vyama hivi katika muktadha wa historia ya Tanzania na utamaduni wa kisiasa wa Watanzania. Vyama katika nyakati tofauti - kuanzia kina Marando na Bagenda, Mtei na Makani, Fundikira na Kasanga Tumbo na Mapalala na Seif walipoamua kujitoa mhanga na kuanzisha vyama - kumekuwa na hatu kadhaa zimepigwa katika kujenga dmeokrasia ya kweli katika nchi yetu.

Watu wanaiweka Tanzania katika mizania ya nchi nyingine jambo ambalo ni kosa kubwa maana Tanzania inapaswa kupimwa kutokana na historia yake. Zoezi la ujenzi wa Taifa na kuwa na Taifa moja chini ya uongozi mahiri wa Mwalimu lilifanywa katika misingi ya udikteta mkubwa sana na chini ya amri moja ya 'zidumu fikra za mwenyekiti'. Tanzania ikajenga jamii ya watu wanaoheshimu mamlaka bila kuhoji na hata vyama vingi vilipoanzishwa vilionekana ni vya wasaliti. Ni mtu mmoja tu mpaka sasa ambaye alikonga nyoyo za Watanzania na kuaminiwa - Augustino Lyatonga Mrema - lakini naye akavurugwa sana na dola, kuitwa pandikizi na kuondoa kabisa credibility yake katika jamii. Jamii imefanywa kuamini kuwa Mrema ni 'kichaa' na hana sifa ya uongozi. Hii ni kazi iliyopangwa na kutekelezwa kwa ustadi mkubwa kiasi kwamba leo ni watanzania wachache sana ambao wanakumbuka sacrifice ya Mrema katika ujenzi wa demokrasia nchini.

Tusipojifunza na kuelewa historia hii ya vuguvugu la demokrasia Tanzania tutaishia kulaumu watu kila kukicha bila kwenda mbele. CCM itaendelea kutawala na kila baada ya miaka mitano kutakuwa kinatokea chama kina nguvu na baadae kuangushwa, wabunge wenye nguvu na baadae kuangushwa na hata wanasiasa wenye mvuto na baadae kupakwa matope na kunuka.

Demokrasia hulindwa. Viongozi hulindwa zaidi ili kubakia kama alama ya harakati. Raila Odinga aliongoza harakati za mapinduzi Kenya mwaka 1982, akaswekwa lupango kwa miaka zaidi ya tisa na kuishi uhamishoni nchini Norway kwa miaka mingi. Akajiunga na chama cha baba yake mwaka 1992 FORD, kikavunjika na kuwa na FORD-K na FORD-A. Baba yake Mzee Jaramogi alipokufa Raila akataka kunyakua uongozi wa chama, akashindwa na Michael Kijana Wamalwa na Raila akaenda kuanzisha chama chake NDP. Akaivunja NDP na kuingia KANU kuwa Katibu Mkuu na akaipasua KANU vipande 2 na kuanzisha LDP. Akaingiza LDP katika muungano wa NARC na kumpa Kibaki Urais (literally alimpa Urais maana Kibaki alikuwa armchair leader of opposition). Akatoka NARC na kuanzisha ODM-K, akagombana na Kalonzo na kuanzisha ODM na leo ni Waziri Mkuu mwenye nguvu Kenya.
Mchakato wote huu Raila alionekana msaliti, mpenda vyeo na mtu wa vita. Lakini leo huna tena KANU na Raila alipata kuniambia, demokrasia Afrika itaimarika tu iwapo vyama vilivyoleta uhuru vitapasukapasuka na kuondoa ile claim yao ya sisi tulileta uhuru - hii ni claim ya CCM na hata kumkumbatia Mwalimu kama wao.

Lakini tuna kina Raila Tanzania? Mazingira ya kisiasa yanatoa fursa ya kujenga kina Raila?
Unawezaje kupewa dola ilhali vyombo vya dola havikuamini? Maana taifa haliongozwi na siasa tu. Idara za usalama na majeshi zina nafasi kubwa sana katika kuamua mustakabali wa nchi. Wanasiasa wa Tanzania ni mara ngapi tunajenga rappour na watu wa usalama ili angalau kujua wanawaza nini. Hakuna.

Mwanakijiji utaandika mpaka utachoka na kutulaumu mpaka utakasirika. Demokrasia ya Tanzania itajengwa kwa sober approach ya kutazama historia yetu na kujua 'political culture' ya Watanzania. Unatutaka tuchukue fursa inapotokea. Wazo murua kabisa. Lakini capacity ipo wapi? Wapo wap wanaofikiri na kuziona fursa? Wapo wapi watu wanaojenga scenerios na kujiuliza what if?

Tulianza vizuri zoezi la kujenga imani kwa wananchi kupitia Bunge. Tulifanikiwa kupata sizable number ya wabunge wa CCM na kujenga coalition nzuri na kupashana habari. Tukamezwa. Tukajikuta tumewauzia ajenda tukijua kabisa hawatafika nayo mbali.

Ndani ya CCM hivi sana wanachowaza ni nani atakuwa Rais ajaye kati ya Membe na Lowasa. Hakuna ajenda ya Taifa, hakuna vision pale. Lakini wanasiasa wa upinzani tunaimba nyimbo zao hawa mabwana na hata 'opinion makers' kama wewe Mwanakijiji mnaimba nyimbo zao.

Juzi nilisema hapa JF, lets be sober and scan the political situation objectively. Kinachoniumiza kichwa ni kwamba, kuna vijana wachache katika vyombo vyetu vya ulinzi na usalama wamechoka na bickerings za wanasiasa. Watataka ku restore order! Mzee Sarakikya aliiwahi kuniasa kuwa tusiruhusu hali hiyo itokee kwani ikitokea hawatarudi makambini! Ili isitokee kuna haja ya kufikiri vizuri - Ignore CCM

An intelligent way of looking at matters like this, safi mheshimiwa Zitto

Mwanakijiji amelalamika, usikosee na wewe ukalamika, njoo na approach ya kufikia kule unapotaka kwenda

Nina mawili

Mosi, umetupa nini Raila aliwahi kukwambia kuhusu umuhimu wa kupasusua vyama vilivyoleta uhuru, je Chadema na upinzani mnao mpango gani kwenye kufanikisha hilo, kwanini usiingie na wewe humo CCM ili kuipasupasua. Au mnasali na kufunga ili ipasukepasuke yenyewe maana huko nako ni kumuenzi baba wa taifa kwani alishawai kuliomba taifa lifunge ili kuiombea Kenya

Pili, ndani ya CCM wanawaza nani atakua raisi baada ya Kikwete, hakuna vision kama Taifa, sawa. Ndani ya upinzani mnawaza nini kama alternative, na ili kuwa specific ndani ya Chadema as far as vision ya Taifa is concerned

La mwisho ambalo ni general, miaka 17 baada ya kuanza kwa mfumo wa vyama vingi, je una-deliver kile kilichotarajiwa? je tunauhitaji? je nguvu ya kuleta changamoto kwa serikali kwa sasa inatoka upinzani au ndani ya CCM yenyewe kupitia kwenye first eleven ya SITA. kama inatoka ndani hatuoni kuwa ingekuwa bora zaidi kubaki na ule ule mfumo wa chama kimoja kinachoweza kuwaletea wananchi yale wanayotarajia

Demokrasia hasa ni nini, ni kubadili uongozi wa nchi kila mara, kubadili vyama vinavoongoza serikali kila mara, au kuwa na uongozi unao-deliver kwa wananchi. Je libya au misri kuna demokrasia? mimi nasema NDIO, wewe je?
 
Mfano wa akina Raila kwa Tanzania hauwezekani. Alijaribu Mrema kuutumia akashindwa. Na sio mfano mzuri wa kuigwa. Ni bora twende Ghana tuone wapinzani kule wanafanyaje mambo yao

Mara nyngi natatizwa sana na dhana hii sijui kwa kiswahili niiteje lakini kwa kiingereza ni "Copy and Paste". Hili naona nitatizo letu kubwa Tanzania na hatupendi ku-originate vitu vyetu wenyewe ili viweze ku match na particularities zetu. Hapa utaona watu wana sema "Raila wa Tanzania", Tuende Ghana tukajifunze and so on.

Nionavyo mimi bila kukubali responsibility yetu watanzania kama individuals tusitegemee kubadilika karibuni. Mabadiliko yeyote kutokea nijambo gumu sana na somebody has to pay a price for it, for old is always Gold na watu wanahofu fulani ya kubadilika ni normal kwa every humanbeing. Sasa hata CCm wangekuwa malaika hawawezi kukubali kubadilika kirahisi lazima kuwe na driving force to that change. The question is who is to lead and be a driving force for that change? Mchezo ninao ona ni kila mtu anafikiria somebody will sacrifice for and agree to lead to bring that change ndo maana utaona macho yetu yana kimbilia kwa wale ambao angalau wanaonyesha kuwa na mwelekeo wa ku lead the change.

Mwanakijiji juzi juzi hapa was talking about the "Meshack, Abednego and Shadrack" of Tz. And that is the problem maana ukiangalia hao hapo juu hawaku fanya reference kwa kitu chochote isipokua imani yao na hawaku copy kutoka kwa mtu yeyote bali walisimamia walichokiamini regardless of the outcome.

Sasa either of the two is possible for our situation either change iletwe kwa lazima na mazingira na hapo ndo huwa inatokea kama explosion kwasababu vitu vinakuwa out of hand haviwezekaniki tena na watu wanasema enough is enough nakama kesi na iwe....Jambo ambalo si zuri sana

ama

Watu wenye maono wajitolee kuwa hao watatu hapo ili waweze ku risk for majority na hapo kuna wawili watatu ku-pay price kama Mheshimiwa Mrema lakini wakipata mass support reward inakuwa kwa every body.

Maoni kwa vijana wa Taifa hili tuunge jitihada zetu na kusaidia kuleta programmed change. Hii mambo yakuacha vitu viende kwa gravity vita cost wengi na kuvirudisha kwenye normal state inaweza ikawa kitendawili. Itakuwaje hivi? Ni kwa kila moja wetu kukataa kutumiwa kwa faida binafsi na kukubali realities njaa ya siku moja isitukoseshe urithi wa miaka yote kwetu na vizazi vyetu. Tuungane na wale wanaoonekana kukataa faida binafsi na wote tutajikuta sehemu moja bila kuambiwa kwani kila mwanadamu ana utashi tofauti ni uvumilivu wa kukaa na njaa.
 
I'm lost....what's this supposed to mean?

Plane-Crash.gif
 
Mara nyngi natatizwa sana na dhana hii sijui kwa kiswahili niiteje lakini kwa kiingereza ni "Copy and Paste". Hili naona nitatizo letu kubwa Tanzania na hatupendi ku-originate vitu vyetu wenyewe ili viweze ku match na particularities zetu. Hapa utaona watu wana sema "Raila wa Tanzania", Tuende Ghana tukajifunze and so on.

Nionavyo mimi bila kukubali responsibility yetu watanzania kama individuals tusitegemee kubadilika karibuni. Mabadiliko yeyote kutokea nijambo gumu sana na somebody has to pay a price for it, for old is always Gold na watu wanahofu fulani ya kubadilika ni normal kwa every humanbeing. Sasa hata CCm wangekuwa malaika hawawezi kukubali kubadilika kirahisi lazima kuwe na driving force to that change. The question is who is to lead and be a driving force for that change? Mchezo ninao ona ni kila mtu anafikiria somebody will sacrifice for and agree to lead to bring that change ndo maana utaona macho yetu yana kimbilia kwa wale ambao angalau wanaonyesha kuwa na mwelekeo wa ku lead the change.

Mwanakijiji juzi juzi hapa was talking about the "Meshack, Abednego and Shadrack" of Tz. And that is the problem maana ukiangalia hao hapo juu hawaku fanya reference kwa kitu chochote isipokua imani yao na hawaku copy kutoka kwa mtu yeyote bali walisimamia walichokiamini regardless of the outcome.

Sasa either of the two is possible for our situation either change iletwe kwa lazima na mazingira na hapo ndo huwa inatokea kama explosion kwasababu vitu vinakuwa out of hand haviwezekaniki tena na watu wanasema enough is enough nakama kesi na iwe....Jambo ambalo si zuri sana

ama

Watu wenye maono wajitolee kuwa hao watatu hapo ili waweze ku risk for majority na hapo kuna wawili watatu ku-pay price kama Mheshimiwa Mrema lakini wakipata mass support reward inakuwa kwa every body.

Maoni kwa vijana wa Taifa hili tuunge jitihada zetu na kusaidia kuleta programmed change. Hii mambo yakuacha vitu viende kwa gravity vita cost wengi na kuvirudisha kwenye normal state inaweza ikawa kitendawili. Itakuwaje hivi? Ni kwa kila moja wetu kukataa kutumiwa kwa faida binafsi na kukubali realities njaa ya siku moja isitukoseshe urithi wa miaka yote kwetu na vizazi vyetu. Tuungane na wale wanaoonekana kukataa faida binafsi na wote tutajikuta sehemu moja bila kuambiwa kwani kila mwanadamu ana utashi tofauti ni uvumilivu wa kukaa na njaa.


Ndugu yangu njaa inatuua na kutufanya vipofu. Hakuna mafanikio bila kujitoa mhanga. Ila kuendekeza usanii kama wa CCM ni hatari sana.

Hata hivyo naungana na Zitto kwamba wapinzani wamefanya mambo makubwa sana kuliko wengi wetu tunavyoweza kutambua. Mazingira yaliyiowekwa na CCM-serikali yanataka mtu uwe kichaa kukabiliana nayo. Kuna watu wameyakabili kwa hiyo tuwatie moyo na pia tutafute nini tunaweza kufanya ili tutoke hapa tulipo.
 
Zitto,

""Tatizo la upinzani ni kuiga mambo mengi kama wanavyofanya CCM""

Na muunga mkono mshika dau "Engineer wa Kyela"kuhusu hilo hasa kushindwa kwa vyama vya upinzani kujitofautisha na CCM kwenye maamuzi yao,wao na CCM kama uchumi tungewaita "homegenious products"!

Uchaguzi na maamuzi ya CCM kila siku huwa ya kiimla kama ambavyo uamuzi wa wazee wa CHADEMA walipoibaka demokrasia ili kumpa ushindi wa chee mwenyekiti mteule Mbowe dhidi ya mgombea Zitto Kabwe;au maamuzi ya kukera ya watu wachache ndani ya CUF kupingana na sauti ya UMMA dhidi ya kumtambua Rais Karume kwa gharama chee ya kupewa nyadhifa ndani ya serikali kwa baadhi ya vigogo wa CUF!

Kama alivyosema M.K na wengine waliotangulia,vyama vyetu vya upinzani lzm wawe sera tofauti na hizi za CCM,then wasiwe rahisi kukubali kutekwa na hila za CCM kama ambavyo CUF kila mwaka wanapodanganywa na kwa kuhaidiwa serikali hewa ya mseto znz!
 
Back
Top Bottom