Makosa katika Maisha Yetu

Makosa katika Maisha Yetu

Castle_Lite

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2016
Posts
3,299
Reaction score
6,379
Binadamu wote sio wakamilifu, mara kwa mara tumefanya matendo na tumesema maneno ambayo kwa namna moja yameweza kuleta madhara katika maisha yetu na wenzetu.

Watu wengi wanasema Makosa katika Maisha hayaepukiki, ndio maana kila mtu ameshawah kufanya makosa.
Tuachane na hayo.
Maana Yaliopita sio ndwele , tugange Yajayo.
Tujisamehe, tujifunze na kusonga Mbele.

Lakini pia Tuepuke kufanya tena makosa ambayo tunajua kabisa kuwa ni makosa. Ukijua jambo si sahihi, usilifanye. Hiyo ni kanuni rahisi, lakini yenye uwezo mkubwa wa kuokoa muda, pesa, heshima, mahusiano na hata ndoto na Malengo yako ya Maisha.

Nasema na wewe ambae Leo unaenda kufanya jambo au maamuzi ambayo unajua kabisa sio sawa na kuna kitu ndan mwako kinakukataza, lakin kwasababu ya tamaa, ubishi, hulka za kibinadamu na hasira uliyonayo bado umedhamiria kufanya.
Mungu akakupe ujasiri wa kushinda hiyo vita na Kufanya maamuzi yaliyo Sahihi.

Nikutakie Mapumziko mema ya Weekend.
 
Hivi ni kweli huwa tunachagua exactly au hutokea tu kama Bahati nzuri unapata mwema au Bahati mbaya unapata kipengele!?
Binafsi naona mwenza hutokea

Mimi naona Tunachagua,
Hatujui huko mbeleni mtu atageuka kuwaje ila kwa mwanzoni (uchumba na urafiki ) tunaangalia vigezo vya wenza wetu ndio tunakubali kuwa nao kama mume/mke.

Maana kila binadamu ana mapungufu.
Ila wengine unaona kabisa ni kama wamedhamiria kuwa wapungufu.
 
Kukosea ni sehemu ya maisha na ndio ubinadamu wenyewe

Upo Sahihi bro.

Ila Tuombe Mungu sana atuepeushe na makosa ambayo unajua kabisa ni kosa ila unashupaza shingo.

Au unajua kabisa nikifanya hivi kinaweza kugeuka na kuwa kibaya ila ukakaza Roho na kufanya.
 
Hata katika hayo ni ngumu kuchomoka, kwa mfano unajua tu kusema uongo ni kosa, lakini unapiga simu uko mnazi mmoja unasema niko Buguruni. Mungu atusaidie tu
Upo Sahihi bro.

Ila Tuombe Mungu sana atuepeushe na makosa ambayo unajua kabisa ni kosa ila unashupaza shingo.

Au unajua kabisa nikifanya hivi kinaweza kugeuka na kuwa kibaya ila ukakaza Roho na kufanya.
 
Nimejikuta nimeamka tu na kuwaza hilo.
Pengine kwasababu niko Sober.😂😂😂😂

(Bro min -me , alosto mbaya sana)
Anyway

Nasema na ww ambaye umepanga Leo kwenda kuzini na mume wa mtu, au mke wa mtu, na ww ambaye umepanga Leo ukaibe au ukadhuru watu kwa maneno au matendo yako Na kufitini rafiki na ndugu yako.

Nasema na ww ambaye umepanga leo ukaloge, ukashuhudie uwongo na ww ambaye unaenda Kulipiza Kisasi

Mungu akupe ujasiri uachane na hiyo roho ya Ubaya ubwela.
 
Binadamu wote sio wakamilifu, mara kwa mara tumefanya matendo na tumesema maneno ambayo kwa namna moja yameweza kuleta madhara katika maisha yetu na wenzetu.

Watu wengi wanasema Makosa katika Maisha hayaepukiki, ndio maana kila mtu ameshawah kufanya makosa.
Tuachane na hayo.
Maana Yaliopita sio ndwele , tugange Yajayo.
Tujisamehe, tujifunze na kusonga Mbele.

Lakini pia Tuepuke kufanya tena makosa ambayo tunajua kabisa kuwa ni makosa. Ukijua jambo si sahihi, usilifanye. Hiyo ni kanuni rahisi, lakini yenye uwezo mkubwa wa kuokoa muda, pesa, heshima, mahusiano na hata ndoto na Malengo yako ya Maisha.

Nasema na wewe ambae Leo unaenda kufanya jambo au maamuzi ambayo unajua kabisa sio sawa na kuna kitu ndan mwako kinakukataza, lakin kwasababu ya tamaa, ubishi, hulka za kibinadamu na hasira uliyonayo bado umedhamiria kufanya.
Mungu akakupe ujasiri wa kushinda hiyo vita na Kufanya maamuzi yaliyo Sahihi.

Nikutakie Mapumziko mema ya Weekend.
Binadamu ana akili sana lakini binadamu huyo huyo ni mvivu wa kufikiri

Binadamu akipata changamoto iliyo sababishwa na yasiyotarajiwa, (uncertainty), huamsha ubongo na kukabiliana na changamoto anapo fanya hivyo anaweza akakutana na ubunifu

Akili ya binadamu huhifadhi matukio iliyo yaona, nusa, sikia, fundishwa ama kwanjia yoyote ambayo mwanadamu amejaliwa nayo matukio hayo yanahifadhiwa kama mafile kwenye ubongo endapo atapa changamoto basi ubongo huchaka mafile yaliyo hifadhiwa na kupata suluhisho la jambo lake ama changamoto

Uwezo wa ubongo wa mwanadamu kuchakata taarifa ili kupata suluhisho ndiyo akili kumbe ubongo wako ukichakata haraka majibu yaliyo sahihi utaambiwa una akili sana

Changamoto nyingi tunazo zipata, (kabiliana nazo), husababishwa na binadamu

Binadamu anaweza kujisababishia changamoto kwasababu ya ujinga, uvivu, ulevi, uzembe, ushamba, uroho wa madaraka, upumbavu nitaje hizi tu kwasasa

Binadamu anaweza pia wasababishia wengine changamoto kwa bahati mbaya ama kwa makusudi
 
Binadamu ana akili sana lakini binadamu huyo huyo ni mvivu wa kufikiri

Binadamu akipata changamoto iliyo sababishwa na yasiyotarajiwa, (uncertainty), huamsha ubongo na kukabiliana na changamoto anapo fanya hivyo anaweza akakutana na ubunifu

Changamoto nyingi tunazo zipata, (kabiliana nazo), husababishwa na binadamu

Binadamu anaweza kujisababishia changamoto kwasababu ya ujinga, uvivu, ulevi, uzembe, ushamba, uroho wa madaraka, upumbavu nitaje hizi tu kwasasa

Binadamu anaweza pia wasababishia wengine changamoto kwa bahati mbaya ama kwa makusudi

Tuache ya Madhara ya bahat Mbaya,

Haya maneno /vitendo vya makusudi ambavyo tunajua matokeo yake yanaweza leta Madhara ndio haswa tunatakiwa kuyapunguza au kuyaacha.

Mungu atusaidie.
 
Back
Top Bottom