Makongoro Nyerere Kugombea Urais-2015

Makongoro Nyerere Kugombea Urais-2015

Wewe tatizo lako linafahamika, unamatatizo na chuki ambazo ni zao la jinsi ulivyolelewa... Kama Makongoro tatizo lake ni pombe, basi asingekuwa anakunywa pombe angekuwa mtakatifu. Kwa uwezo wa kuongoza ni kiongozi ambaye akipewa nafasi atatisha..... Humfaham mtu unamwongelea kwa tetesi tu.

mako ...is bright ...lakini issue ya Pombe ni tatizo ambalo watu wa Usalama WAMEFUZWA namna ya kumdhibiti kiongozi mlevi Kama walivyofunzwa kukaa na kiongozi mpenda mabibi ...Iko hivi kwa kuwa Nchi haziongozwi na malaika...so state organs are prepared for either scenarios kwa kuwa nchi ni Za kidemokrasia ....
USA ...secret service wamefunzwa hadi kukaa na Rais Dull ..yaani mbumbumbu ....na hata Rais mwenye usahaulifu ...wote .....mtu pekeee ambaye wamefundishwa kummaliza akishika dola ni Rais msaliti au muuza Nchi ...au mtoa Siri ...
Ingekuwa Tanzania haya yanaruhusiwa kaundikwa ...wasaidizi wa Rais wangekuja kuandika ....waliwezaje kukaa na Rais ..." Mlevi " Mkapa ...bila watu kujua ....
Rais easy going ...mwenye marafiki hadi wavuvi ambao akiwaona hata barabarani anataka kusalimiana nao ..kwa Kifupi mtu wa watu kupitiliza Kama Mwinyi ...
Au wameweza VIPi kudhibiti Tabia ya Rais Kama Kikwete ambaye akiona sketi a nachanganyikiwa kabisa ...na hajielewi ....

There are different ways of dealing with both leaders and people are trained to do that ...kwa kuwa wana Amini kuwa demokrasia Inaweza Kuleta Ikulu mtu yeyote average kuwa Rais ...

Someni Biography Za Marais Kama Boris Yeltsin ...Kim Jong IL .,Mao , Ronald Regan ..Ford ...hata soma Juu ya Rais Kama Jomo Kenyatta ambaye Siku Za mwisho alikuwa anaweza kupitiwa na usingizi mzito Kati Kati ya mkutano wa HADHARA na namna maafisa wake waliyoweza ku deal na Hali Hiyo bila watu waliokaa chini kujua ....na anaondolewa kupitia ,Lango wa nyuma ....na hata kuweza kurudishwa baadaye kuhutubia
 
Itakumbukwa kwamba kumekuwa Na mtifuano mkubwa ndani ya chama cha mapinduzi juu ya nani atakayepeperusha bendera ya ccm kwenye uchaguzi mkuu 2015. Kwa taarifa zisizo rasmi mtoto Wa hayati mwl Nyerere muasisi Wa taifa bwana makongoro Nyerere ndiye anayepogiwa upatu zaidi kugombea katika nafasi hiyo nyeti. Wakati hayo yanaendelea bado yupo mtu ambaye wafuasi wake wanaamini kuwa ndiye rais wao anayesubiri kutangazwa naye si mwingine Bali ni ndugu Edward lowassa. Swali kubwa linalobaki bila majibu juu ya namna ya kumtuliza Mzee huyu mwenye uchu Wa kuongoza kwa namna yoyote ile.

Kama makongoro atasimamishwa atakutana Na Changamoto kubwa 2
1. Atapata upinzani mkubwa kutoka ndani ya chama ambacho ki mfumo kimekuwa Na vigogo wengi ambao ni watuhumiwa wa kashfa mbalimbali za ufisadi
2 atakumbana Na upinzani mkali kutoka kwa Mgombea Wa ukawa kwani makongolo ni mtu asiue Na legacy yoyote ile tofauti Na title ya Kuwait mtoto Wa Nyerere peke yake
 
Hakuna mgombea wa ccm ambaye hatapata upinzani wa ndani na nje.!. Hili naomba uliwekee muhuri.

Ninaomba wanaccm waliozowea kidumu wakasahau taaluma zao, anzeni kujikumbusha ili mtafute kazi za kufanya kwa sababu ccm haipo tena!.

Si Makongoro, wala nani. Ccm ilishakufa siku nyingi za kikwete!. Makongro mnamsingizia tu, sana sana semeni kweli mnataka ahitimishe mazishi kama vile mtu akifariki anavyokwenda kuzikwa nyumbani kwao!.
 
Hakuna facts,Mwl Nyerere was marxists and leninsts je mtoto anaufuasi huo au ccm wanadanganya??,politics needs platform revolutions,je mtoto wa mwl mbona hajawah fanya haya??
 
bora ya Makongoro atawasikiliza wazee kama kina Warioba kuliko hao wengine
 
Ccm bwana mh mpaka huruma nawaonea,,, ina maana wamekosa mtu mwingine mpaka wakamkimbilie makongoro kule butiama duuuuh makubwa haya

Kweli simba akikosa nyama hata nyasi atakula




Hapo kuna mtu hawamtaki wanamuogopa nyooooo

Wanatafuta weak chairman wampelekeshe wafiche uharamu wao

Filamu nzuri sana


Najua comrade wao pekee anakunywa maziwa mahali
 
Makongoro Nyerere kama anaonekana anafaa,basi wangemchagua awe mwenyekiti wa CCM ili akakisafishe tu hicho chama kama kweli anaubavu huo.Chama kimechafuliwa kupita kiasi, hata kama yeye ni msafi vipi lazima walioshika matope watamchafua tu na baada ya muda tutamuona kuwa na yeye ni wale wale.sidhani kama kuna msafi katika CCM,Muda umefika na ni mwaka huu kuangalia nje kabisa ya hili sanduku, mtu anayefaa kuongoza kama raisi wa nchi hii kubwa na si raisi wa CCM na mafisadi.
 
Papa1
Ha Ha Ha ! Mkuu nimecheka sasa pointi yako moja "tezi dume"
 
Mnapenda sana Hadithi za Vijiweni.Huu uoga wenu wa Usalama wa Taifa unatoka wapi? Kila mtu siku hizi anakuja na mambo ya ajabu,baada ya kuangaliwa kama yeye watu wanajiuliza kama ni Usalama wa Taifa.Who is Usalama wa Taifa? Hakuna yeyote leo anayeweza kusimama na kujitapa kuwa yeye ni Usalama wa Taifa?.Idara hiyo imekufa kitambo,kazi zote za Idara hiyo zinafanywa na TAKUKURU.Kwenye Idara kumebaki Walinzi wa Viongozi tu,ambao kwa kawaida hawawezi kujenga Hoja kwa sababu wamejengewa tabia ya kutojiamini na kuwa watu wa NDIO Mzee.Wanakimbizana kwenye Ma-corridor ya MOFA kutafuta safari za kwenda nje ili wainue kipato chao.Hapa tulipofikia inabidi tujenge Upya Uzalendo na kuijali Nchi kuliko Umimi uliopitiliza Kiwango.
Makongoro hawezi kuchaguliwa hata ndani ya CCM kubeba bendera ya CCM katika mbio za kinyang'anyiro cha Urais.CCM wanajua fika kwa kufanya hivyo itakuwa kuwapa njia rahisi Wapinzani kushinda Uchaguzi wa Rais.Makongoro hata hii nafasi aliyonayo sasa ya Ubunge wa EA ameipata ili kutoa nafasi kwake na familia ya Mwalimu kujisikia kuwa bado CCM inawakumbuka,kama si hivyo asingeweza kuipata,sifa zake za Uongozi ni hafifu mno.
mkuu umenena vyema wabongo ni wepesi kukubali kila kitu ukiambiwa huyu usalama wa taifa unakubali tu, hebu tubadilike jamani imefika kipindi ukiwa na rafiki ambaye kazi yake hujui na ye kakudanganya anafanya kazi usalama wa taifa unajiona tofauti sana
 
Baada ya kuvuma sana kwa taarifa za kwamba CCM infikiria kumsimamisha Makongoro Nyerere kuwa mrithi wa raisi kikwete, Mh Makongoro Nyerere ameamua kuweka wazi bila kkupinga kwamba ana nia au hana nia ya kuwania uraisi.
Vyombo vingi vya habari na mitandao ilitoa taarifa za bwana makongoro kuombwa agombee nafasi hiyo katika uchaguzi ujao ili aweze kusaidi kurudisha mshikamano, umoja na nidhamu ndani ya chama cha CCM, japo wengi wanalichukulia hili kama sehemu ya muendelezo wa siasa za minyukano ndani ya chama na Mh. Makongoro anatumika kupunguza kazi ya baadhi ya wagombea ndani ya chama chake.

Alipoulizwa juu ya taarifa zilizozagaa juu yake, bwana makongoro alisema " hizo ni taarifa za watu ila mimi bado sijatangaza rasmi nia ya kugombea uraisi na muda utakapofika basi nitatamka.." aliendelea kusema " chama chetu kina utaratibu mzuri wa kupata mgombea wake na mimi naheshimu taratibu hizo".
Mh. Makongoro ambaye ni mstaafu wa jeshi na msomi mahili, kwa sasa ni mbunge wa bunge la africa mashariki na ni mtu anayesemekana kuwa na misimamo thabiti haswa juu ya vita dhidi ya rushwa, anaheshimika sana kwa misimamo isiyo ya kimakundi.

katiba maelezo yake Mh. Makongoro amesema, juu ya wanachama waliojitokeza kugombea nafasi hiyo kwa sasa, na kusema wapo baadhi wanaouwezo wa kuiongoza Tanzania yetu na chama chetu lakini wapo wengine itabidi chama kiwe makini kuhakikisha hawapati nafasi kwani hawa wakipata pamoja na kwamba chama kitashinda kwa taabu lakini uadilifu wao hautatupa matumaini ya huko tuendako, alisema wapo viongozi wengi bado hawajatangaza nia yao na ni wazuri na waadilifu na wazalendo kwa nchi yao watatufaa wakipata nafasi lakini sio hawa wanaendeleza vijembe na kushawishi watu kwamba wao ndio zaidi ya wengine na kutujengea makundi ndani ya chama chetu na kufikia kugawa watu, vijana lazima wawe makini na kuendeleza fikra za watu kwa kutumia kupita na kunadi wagombea kabla hawajajiridhisha kuwa mtu wanayempigania ni sahihi, alisema.
Kwa nchi yetu hapa tulipofika mtu yoyote anaweza kuja na kusema yeye ndio atakuwa mkombozi wetu na kuisema vibaya serikali iliyopo, hiyo ni kawaida lakini haimfanyi yeye kuwa sahihi, serikali imefanya mengi bado changamoto haziwezi kukosekana.

Akiwachambua baadhi ya wagombea ambao wameshitokeza, alisema, wagombea hawa mi naona wengi wamekurupuka sana, haswa hawa vijana wetu, bado wana kazi ya ziada ya kuijua nchi hii na kuendelea kuwepo katika system ya nchi yetu kiungozi kabla ya kutamani kuwa maraisi wa nchi hii, inashangaza sana kuona sasa kuwa raisi imekuwa rahisi hivi kiasi kila mtu anaona anaweza, ujana sio sifa bali inaweza kuwa sifa ya ziada, nawasihi wasubiri wakati wao utafika.
akiongelea kuhusu wazee, alisema katika hawa wapo ambao tuna imani nao sana, uadilifu wao na utumishi wao ndani ya serikali na chama umejidhihirisha kabisa, na wengine bado tuna mashaka nao lakni wengine wanonekana itakuwa ni sababu ya kujenga makundi ndani ya chama chetu.
Bila kutafuna maneno Mh. Makongoro amesema viongozi wanaonekana kuwa na uadilifu ndani ya chama chetu na uzalendo wakweli wanaongozwa na Mzee Wasira, Samuel Sitta, Fredrick Sumaye na wengine tu hawa wengine bado ni mashaka tu.
Akimzungumzia Mh. Wasira, Mh. Makongoro alisema huyu ni mtu ambaye anijua nchi yetu na amekuwa kwenye mifumo ya uongozi toka enzi za nyerere na ni nguzo imara ya chama na serikali yetu, ameonyesha uzalendo wa juu na kuwa kiongozi muadilifu. chama chetu kikiweka mtu kama huyu tutakuwa hatuna kazi ya kumsafisha kabisa na ushindi wetu utakuwa wa wazi kabisa, simpigii debe kwakuwa anatoka mkoa mmoja na mimi ila ni wazi tu huyu ni kiongozi mchapakazi bado anaonekana kuwa na nguvu za kuitumikia nchi.
Akimzungumzia Mzee Sumaye, alisema kweli huyu ni kiongozi pia mwenye uwezo ila tatizo linalokuja amekaa sana nje ya serikali na mfumo wa nchi, ameitumikia nchi kama waziri mkuu kwa miaka 10 kwa heshima kubwa, sasa kurudi sasa ulingoni naona kama itakuwa shida, angeendelea kuwa mshauri wetu tu, Kuhusu Samuel Sitta, anasema uimara wa kiungozi aliouonyesha Mh Sitta kwenye bunge la katibu imempa sana heshima, lakini mizozo ya suala la katiba mpya itaendelea kumfunika kwa sasa, kwani wengi wanaamini ushirikishwaji wa wananchi na baadhi ya makundi haukuzingatiwa sana.

Mh. Makongoro anaamini bado CCM itaendelea kutawala Tanzania na kushinda uchaguzi ujao, ila lazima apatikane kiongozi anayeuzika kwa wananchi kwani upinzani sasa umekuwa sana nchini.

source:Raia Tanzania
 
Kama ni ndugu yako kweli, hivi mna upendo wa kindugu au wa kubebeana mizigo?

Pili kuna mdau post #258 ameweka kile ambacho kwa yeyote nyota ikiwaka hata kama ni mpenda vimwana kuna jinsi ya kuongozwa na kusimamiwa na kufuatiliwa as Kiongozi wa nchi, so ndg Andrew Nyerere hivo ni fitina zako tu.


Indeed . Makongoro anakunywa sana pombe. Siku yoyote ukiiona gari yake imepaki pahali,utaona nyuma kuna kreti chache za bia,ambazo zinakuwa replenished zikianza kupungua. Kwenye seat ya mbele utamuona msichana mpya kila siku.
 
Ni mheshimiwa Makongoro Nyerere, mtoto wa Hayati baba wa Taifa Mwl.Julius K.Nyerere.
Nimeoteshwa ndoto hii usiku wa kuamkia leo.
NB: Jadili hii ndoto kwa kutumia uelewa wa ndoto na unabii. Mihemko haitakiwi.
 
Indeed . Makongoro anakunywa sana pombe. Siku yoyote ukiiona gari yake imepaki pahali,utaona nyuma kuna kreti chache za bia,ambazo zinakuwa replenished zikianza kupungua. Kwenye seat ya mbele utamuona msichana mpya kila siku.

Hili linatisha.
Kama ilitendwa na amiri Jeshi mtarajiwa.
Mama watoto wake siatapata Presha kwa Kauli kama hili. Mzee ebu msitiri mtu mzima fanya ulikosea/Utani vile.
 
Back
Top Bottom