Makonda anatumika kwa makusudi maalum?

Makonda anatumika kwa makusudi maalum?

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
12,152
Reaction score
44,110
Nimekuwa nikifuatilia kwa muda mrefu sana mwenendo na tabia za kisiasa za Paul Makonda, nikahisi ni mtu anaweza kuwa anatumika kwa makusudi maalum(Yaani Chambo, kijaribio(Pilot test), Kitangulizi au Kianzisha mwendo, Kivuli cha kujifichia wakubwa zake).
Wengine pia wenye hulka hizo ni Nape Nnauye, Humphrey Pole Pole, Salum Hapi, Mrisho Gambo nk.

Na haya ni baadhi ya Mambo ya msingi sana ambayo mara zote yamekuwa yakienda sambamba na Makonda

1/Kila alichokuwa akikishupalia sana, basi baadaye ilijulikana kuna Mkubwa aliyekuwa akimtuma kusema au kufanya hayo.

2/Kila tukio kubwa la ajabu ajabu alilofanya Makonda lilipelekea Kupongezwa au kuaminiwa na kupewa cheo cha juu zaidi na Wakubwa wake.

3/Mara zote amekuwa akipenda kufanya mambo kwa ubinafsi zaidi kuliko kitaasisi, na hapo hapo wakubwa wake wakifurahia na kumpongeza

4/Ni mtu anayependa Kujipendekeza na kujihusisha kwa gharama yoyote ile na wakubwa wake wakuu(Ni rafiki mkubwa sana wa Wakubwa wake).
 
Sasa mbona wanamtumia kwenye mambo ya kijinga, kwa mfano kuwashutumu bila ushahidi viongozi wa polisi
 
Wanaume kama mabinti- lady jay dee
- kawimbo kazamani sana haka[emoji3][emoji3][emoji3]

[HASHTAG]#chaumbea[/HASHTAG]

[emoji3][emoji3][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125]
 
Sasa mbona wanamtumia kwenye mambo ya kijinga, kwa mfano kuwashutumu bila ushahidi viongozi wa polisi

HUYO NI MKUU WA MKOA NA HAWASEMI UONGO KWA HIYO MAKONDA HADI KUSEMA HAYO NI KWAMBA YUKO NA USHAHIDI SASA HAWAO WATUMWA WA CCM KAMA WAMEPEWA TANO TANO WAZIRUDISHE NA WAZIRI HAJE NA HAKANUSHE KAMA KAWAIDA YAO.


swissme
 
Kila lenye mwanzo lazima litakuwa na mwisho........haya maneno siyo maono naomba nisishitakiwe.
 
HUYO NI MKUU WA MKOA NA HAWASEMI HUONGO KWA HIYO MAKONDA HADI KUSEMA HAYO NI KWAMBA YUKO NA USHAHIDI SASA HAWAO WATUMWA WA CCM KAMA WAMEPEWA TANO TANO WAZIRUDISHE NA WAZIRI HAJE NA HAKANUSHE KAMA KAWAIDA YAO.


swissme
Huongo= uongo,
 
Nafikiri hayo yote ndo yaliyomfanya awe mkuu wa mkoa pekee aliyekua na uhakika wa kuipata iyo nafasi kabla ya kuteuliwa.
 
Sasa mbona wanamtumia kwenye mambo ya kijinga, kwa mfano kuwashutumu bila ushahidi viongozi wa polisi
Huwa ndivyo inavyokuwaga kwa viongozi wa nchi zetu hizi za kinafiki kuwatumia "Vichaa" fulani kwenda mbele za watu kufanya ujinga. Wakubwa wenyewe huwa hawanaga ujasiri huo.

Kuhusu ile issue ya Juzi ya Makonda na Kamanda Siro, mbona iko wazi sana. Jaribu kuchunguza vizuri ndio utagundua nani kamtuma Makonda kwenda pale kuyasema yale. Kuna kitu behind the scene...

Majaliwa aliweza kuligundua hilo, na ndio maana akafunguka vile.....
 
HUYO NI MKUU WA MKOA NA HAWASEMI UONGO KWA HIYO MAKONDA HADI KUSEMA HAYO NI KWAMBA YUKO NA USHAHIDI SASA HAWAO WATUMWA WA CCM KAMA WAMEPEWA TANO TANO WAZIRUDISHE NA WAZIRI HAJE NA HAKANUSHE KAMA KAWAIDA YAO.


swissme
Unajifunza kiswahili ama vip
 
Mtoa mada una akili sana,hii kauli ya kupunguza watumishi nafikiri ni maagizo kutoka juu.
Mwisho linaweza tolewa tamko rasmi...
Dah!
 
Screenshot_20161119-145632.jpg
 
Back
Top Bottom