Ni Ukweli usiopingika 100%
Kwanza mkuu
Mshana Jr nikushukuru na kukupongeza kwa kutuzindua ufahamu juu ya jambo hili.
Mada zako huwa zinatuelimisha sana mkuu. Hivi Kuna watu humu wanachukulia mzaha jambo hili.
Mimi binafsi ni mpenzi sana wa kujifunza na kufatilia mada na masomo mbalimbali ya kiroho (spiritual)
Ni Ukweli usiopingika kuwa Tendo la ndoa ni AGANO. Mnapokutana mwanaume na mwanamke pale kwenye Tendo maana yake mnafanya AGANO mbali na kuuburudisha mwili, kwenye ulimwengu wa roho kuna vitu mnabadilishana, ikiwemo laana, mapepo, mikosi, mabalaa, nuksi baraka~(hiyo huwa nadra sana)
Ndio maana kuna mwanamke/mwanaume ukilala nae then ukaenda kwenye mipango yako inaharibika yoote, iwe kazi, biashara, interview, n.k kwa wale wanaofanya bishara nadhani wameelewa ninachomaanisha.
Ki Ukweli jamii sasa hivi ipo kwenye hari mbaya sana hususani kwenye masuala haya ya kiroho. Ni wachache sana tuliojitambua.
Guys, unapojamiiana na Mwanaume/mwanamke tambua kua umebeba laana kuanzia ya Bibi yake+ ya babu yake+ ya mama yake+ ya baba yake+ laana yake mwenyewe. Sikwambii kwenye mapepo,, sikwambii kwenye nyota inavyo chafuka (kismat).
Jiulize umelala na wangapi? Umebeba laana ngapi?
Umebeba ma-roho (mapepo) mangapi aliyokuachia?
Badilika sasa
Hao wanaojiuza wenyewe kutwa wanabadilisha waganga wakuwatengenezea makafara ya kuwavutia wateja wao, na mazindiko yenye maagano mbalimbali.
Mbegu zako unazommwagia zinathamani sana kwà mganga wake, siku utakayogeuzwa kizimba ndo utajua hujui. Haya mambo yapo usifikiri utani.
Ndio maana watu wengi utawaona wanakimbilia sana kwa waganga wakidai mambo yao yameharibika ghafla, wengine wanadai eti wamerogwa


kumbe tabia zao ndo zimewaroga.
Unalala na mtu hata humjui anapotoka, asili yake, ukoo wake, nyota yake.


Kisa tamaa za mwili zimekutawala. Nakuombea Mungu akusaidie sana
Mungu alipo kataza zinaa hakua na maana kua anauonea donge mzigo wako hapana.
Zinaa mbaya jamani, itakuadhibu kimwili then ikumalizie kiroho.
Ushauri wangu kwa vijana na jamii kwa ujumla, tutulie kwenye ndoa zetu kama umeoa, kama bado hujaoa basi vuta subra mpaka utakapojaaliwa kuwa na mwenza sahihi.
Mungu akusaidie Sana Ufahamu