Makete Njombe: Mwanafunzi achoma moto bweni la wavulana na kuteketea kila kitu

idawa

JF-Expert Member
Jan 20, 2012
25,284
38,312
Mwanafunzi mmoja anahisiwa kuchoma bweni la wanafunzi zaidi ya 140 na kuteketea kila kitu kwenye shule ya Sekondari Mang'oto iliyopo wilayani Makete mkoani Njombe.

Tukio hilo limetokea jana muda wa saa mbili usiku wakati wanafunzi wakiendelea kujisomea madarasani.

Chanzo inasemakana, Mwanafunzi huyo kabla alihisiwa juzi usiku tarehe 11/3/2018 alivamia kibanda cha mwalimu kilicho jirani na shule hiyo na kuiba baadhi vitu vikiwemo karanga na biskuti....

Jana asubuhi ndipo Mwalimu alipogundua kibanda chake kimebomolewa usiku, katika kufanya upelelezi ikaonekana huyo mwanafunzi usiku wa jana wenzie walimuona akila biskuti na karanga ambazo zilihisiwa moja kwa moja zilitoka kibandani humo.

Baada ya kupewa kibano na walimu mwanafunzi huyo akakiri kuwa ni kweli alihusika na uvamizi huo.

Baada ya kukiri hivyo inasemekana wanafunzi wengine walimpa kipigo kando na alichopewa na walimu.

Baada ya kupewa kipigo hicho,jana mchana inasemekana alishinda porini akipanga mipango yake ya kulipa kisasi kwa wanafunzi wenzie waliompiga.

Ndio akaja na wazo la kurudi usiku mida ya saa Mbili na kukusanya kila kitu cha wanafunzi waliochangia kumpiga akakusanya magodoro, daftari, vitabu na nguo zao na kuzipiga kiberiti.


Bahati mbaya ule moto ukashika ukuta, na kuunguza bweni lote na kila kitu kilichomo ndani.
FB_IMG_1520912454056.jpg
FB_IMG_1520912462215.jpg
FB_IMG_1520912467337.jpg
 
Mwanafunzi mmoja anahisiwa kuchoma bweni la wanafunzi zaidi ya 140 na kuteketea kila kitu kwenye shule ya Sekondari Mang'oto iliyopo wilayani Makete mkoani Njombe.

Tukio hilo limetokea jana muda wa saa mbili usiku wakati wanafunzi wakiendelea kujisomea madarasani.

Chanzo inasemakana, Mwanafunzi huyo kabla alihisiwa juzi usiku tarehe 11/3/2018 alivamia kibanda cha mwalimu kilicho jirani na shule hiyo na kuiba baadhi vitu vikiwemo karanga na biskuti....

Jana asubuhi ndipo Mwalimu alipogundua kibanda chake kimebomolewa usiku, katika kufanya upelelezi ikaonekana huyo mwanafunzi usiku wa jana wenzie walimuona akila biskuti na karanga ambazo zilihisiwa moja kwa moja zilitoka kibandani humo.

Baada ya kupewa kibano na walimu mwanafunzi huyo akakiri kuwa ni kweli alihusika na uvamizi huo.

Baada ya kukiri hivyo inasemekana wanafunzi wengine walimpa kipigo kando na alichopewa na walimu.

Baada ya kupewa kipigo hicho,jana mchana inasemekana alishinda porini akipanga mipango yake ya kulipa kisasi kwa wanafunzi wenzie waliompiga.

Ndio akaja na wazo la kurudi usiku mida ya saa Mbili na kukusanya kila kitu cha wanafunzi waliochangia kumpiga akakusanya magodoro, daftari, vitabu na nguo zao na kuzipiga kiberiti.


Bahati mbaya ule moto ukashika ukuta, na kuunguza bweni lote na kila kitu kilichomo ndani.

Njaa hiyo.

Lakini pia suala la viwango vya uwezo wa kulea watato kwa walimu linatakiwa liangaliwe upya. Walimu wa zamani walisoma education psychology seriously sana. Haya yanaweza kuwa ni mchango wa kudharau taaluma na kuanza kututpia tupia tu walimu wa vodafasta,ili mradi anajua somo analofundisha. Education as a subject is more than teaching.

Tumshukuru Mungu watoto wote wako salama.
 
Nimejiweka kwenye nafasi ya mzazi wa huyo mtoto sasa ndio umepeleka kijana akasome anachoma moto bweni kama mshikaki. Ugumu wa malezi sio utani I see unaweza kujichukulia sheria mkononi tu
 
Back
Top Bottom